Maandamano ya wanahabari Sept 11, 2012

Maandamano ya wanahabari Sept 11, 2012

Walichokionyesha Leo Wanahabari wetu katika Viwanja vya Jangwani kukataa kwao kwa Kuwepo Waziri Muhusika kupokea Hoja zao ni Udhaifu, Ujinga na Akili za Kitoto, Inaelekea wamefanya Maandamano hayo bila kujua Malengo na Makusudi ya kweli ya kufanya hivyo. Kwa hiyo inayakinisha kuwa wengi wao walikuwa hapo walikuwa Bendera fuata Upe[o!
Kilichofanywa na wanahabari, kwa kumtimua Nchimbi, ni sahihi kabisa, hebu imagine inatokea kwa mfano mtu aliyesababisha kifo cha mzazi wako, halafu anakuja siku ya mazishi, na kuigiza kuwa huo msiba, umemgusa sana, sasa mtu kama huyo wanandugu wenzako wakimtimua utasema wamekosea??!!
 
Nchi imeshauzwa na pesa wameshagawana hata tukiandamana kilio hakisikiki!!! Jamani watanzania tuungane kuudai uhuru wetu nchi haielekei pazuri. Tulopo marekani tunawaunga mkono
 
Waziri itabidi ajibebe, maana waandishi hawa wa habari walitangaza kuwa ni maandamano yao so hawataki kiongozi yeyeto wa chama cha siasa wala serikali kwenye maandamano yao
 
du! Wangetupa japo kavideo kidogo cha tukio la pale iringa ingenoga
 
Safari hii magamba wamegusa pabaya hawatoki 2015 watakoma lakini tatizo hakuna umoja wanahabari kivyao,doctors kivyao,walimu kivyao yaani divide and role.
 
"ukiona waandishi wanauliwa na askari, basi ujue kuwa askari hawataki mtu wa kushuhudia na kuripoti mauaji ya raiya yanayofanywa na askari kwa maagizo ya serikali". by Dr. Azavaeli Lwaitama.

Well said Lwaitama, Shame on them PolisiCCM!
 
Nchimbi ataendelea kujidhalilisha hadi lini na ni kwa nini ameamua kutumia muda wake mwingi ku prove beyond reasonable doubt kuwa ni HIGHLY INCOMPETENT. Hivi anafikiri nguvu za GIZA zitafanya kazi kila mahali?, Hata magadi hayawezi kumsafiki ni kutulia asubiri upepo upite ila thanks waandishi jamaa amepewe message LIVE
 
Hivi hii serikali iliyopo madarakani kwa mtindo huu inajiandaa na uchaguzi 2015,au?,mimi nadhani wajiandae kuwa wapinzani na sio watawala tena wasiotambua madai ya raia wake.
 
Naunga mkono maandamano, kama haki ya msingi ya kila raia kutoa maoni yake. Siungi mkono kitendo cha kuzomea waziri, kwa kuwa tendo la mauaji, si dhamira ya serikali wala chama chochote cha siasa, bali ni utendaji kazi mbovu wa mtu mmoja na wala si jeshi la polisi.

Ni dhamira ya serikali chini ya CCM kuua na kulinda wauaji hao. Hivyo ndio namna matendo yanavyoonyesha, kama serikali haiungi mkono mauaji wahusika wote wangekuwa wapo mahakamani na viongozi wa kisiasa wanaohusika wangejiuzuru na wangeeacha kutoa matamko yanayoonyesha kutetea udhalimu wa jeshi la polisi.
 
huyu bwana ana kashfa ya kujiita docta wakati hakuwa na phd
ndio ameisomea mzumbe sijui kama keshapata
mtu mwenye kashfa kama hizi za wizi wa elimu atawezaje kuongoza waziri nyeti kama hii ya mambo ya ndani?
hapo ndipo ninapohoji integrity ya JK kumchagua mtu kama huyu
Bora arudi kwenye vazi la taifa au apewe ukurugenzi wa TOT.
hajajua nguvu ya kalamu ya mwaandishi wa habari
 
Mie sijaelewa walimwita halafu wakamkataa au kajipendekeza mwenyewe?
 
Same time huwa nawaona channel ten wanafki wanashindwa kurusha live bila chenga sasa wanaonesha tarabu
 
Back
Top Bottom