Maandamano ya wanahabari Sept 11, 2012

Kama Haya ya waandishi Yamewezekana basi Na Madaktari wana Haki ya kuandamana Kulaani ya Ulimboka!! Hii itaongeza Usalama wake wa baadae!!
 
Me nipo moshi nimekutana nao na mabango japokuwa sio wengi but ujumbe umefika, tunataka tujue kwanini baadhi ya mikoa wamezuiliwa
 
Hongereni kwa kuwezesha hili, sasa msimamie ukweli kwenye kazi zenu. Kila siku mnaambia fanyeni kazi kwa uadilifu, kuna baadhi yenu mko biased kiasi hamuwezi kuandika ukweli.
Bado kazi mnayo.
Alikuwapo mwandishi gani mkongwe zadi ya wote?
 
Nimefikiria sana, nimetafakari sana, kwa heshima ya Serikali yangu, Raisi wangu, Familia yangu na wananchi wa jimbo langu, kwa kitendo hiki cha kuzomewa hadharani kwani sijawahi kuzomewa hata siku moja nimeamua kuachia ngazi, kama suala lenyewe ni uwaziri sitaki tena kwani ni fedheha kubwa sana nimepata kwa kuzomewa huku na nafikiria kuchukua hatua nyingine ya kujivua ubunge ili nisionekane tena kwenye majukwaa ya siasa. ni mimi Waziri niliezomewa
 

huyo mtu unaomsema kafikishwa mahakamaani ndani ya masaa 24 au bado na kwa nn. jibu swali
 

Alishafanya PhD laundering pale Mzumbe University, ila inazidi kujidhihirisha kuwa haipo kabisa pale kwake.
 
Kweli maandamano haya kiboko wala si matani tena ... dahh!!!

Meena anagombaniwa na vyombo vya habari kila kona utadhani kama vile ni Rais Obama wa Marekani au Puttin wa Urusi wakiwa katika majukumu yao ya kimataifa vile?????

Na sasa iwe ni fundisho kwa serikali kutokuchezea damu za WaTanzania huku tukishinikiza viongozi kadhaa akiwemo Wasira, Nchimbi, Mwanasheria Mkuu pamoja na Waziri wa Haki na Katiba wote wajiuzulu kutokana na haya yote.
 
Nani alimwalika?au ndo kujiosha kuwa anawapenda wanahabari?Shame on him
 
ninaamini kabisa hata angeenda kiongozi wa nchi yetu watu wangezomea tu
Nchimbi haonekani sana kisiasa, angeenda JK wangempopoa na usalama wa Taifa wanajua hilo ndio maana ni ngumu kumpeleka sehemu kama hizo. Kama haamini kwamba inaweza kutokea ashawishiwe ajaribu wakati bado mambo ya moto.
 

aiseeee babaangu ha ha ha ha umeniacha hoi sana enbu 2wasiliane niku2mie mbege lita 2
 
Raisi Jakaya Khalfani Mrisho Kikwete; mauaji mengi (polisi kuua raia engi na kuua mwandisi mmoja wa habari) yametokea katika kipindi chake. Raisi aliyefanaya cabinet reshuffle mara nyingi zaidi kuliko raisi mwingine yeyote baada ya JK wa ukweli (Mwalimu JK Nyerere) ambaye alikaa madarakani kwa muda mrefu zaidi. Raisi wetu anayependwa na wanafiki wa CCM, ambaye hata sasa hajasema lolote kuhusiana na Kifo cha kihistoria cha Mwangosi, ndiye amaye amelifikisha taifa hapa, hasa kwa kushindwa kuwaaadibisha watu aliowateua yeye mwenyewe. Huyu naye apaswa kuondoka sasa na chama chake 2015.
Viva M4C
 
Dalili zinazidi kuwa wazi kuwa 2015 inaweza isifike CCM ikiwa madarakani...
Hicho haswa ndio ninachokishauri mimi maana tukifika 2015 michezo mibaya ni mingi sana na pesa itapotea nyingi sana.
 

Sio 2015, anatakiwa aondoke before 2015. Ndio njia bora kuliko zote, cha msingi tu ni njia muafaka ya kufanya hivyo.
 
tungependa kujua toka kwa wadau nin kimejiri ktk maandamano ya waandishi wa habar
 
Aiseee babaangu unajaza nafasi humu jf kuna uzi unaelezea maandamao ya mwandishi habari so hacha uvivu
 
Asante kwa updates, maandamano ndiyo njia pekee iliyobaki kwa ss tusiomiliki mitutu. Ila huyu dk(dikteta)JK anayaona haya na kunyamaza kimya, akae akijua kuwa raia ni wengi kuliko polisi na wanajeshi, ipo siku huu uvumilivu unaoitwa amani utaisha nchi hii, wao wana bunduki na mabomu, sisi hata mawe yatatufaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…