Maandamano ya Kumpinga JK Washington DC

Maandamano ya Kumpinga JK Washington DC

Status
Not open for further replies.
by Mwingereza
UPDATE:
Wana Jamii Forums. Kwanza tunanaombeni radhi kwa kuwaangusheni. Mpango mzima ulisukwa Tanzania. Wafadhili wetu wapo Tanzania na wachache nchini marekani. Hatuhusiani na CHADEMA kama wengine wanavyofikiria. Sisi ni Wana CCM waliochishwa na ufisadi wa Kikwete. Sisi ni Wana UVCCM ila waandamanaji ni watanzania ambao hawakuonysha itikadi zao za kisiasa. Ukweli ni kwamba, tumekuwa tukifuatiliwa kwa muda na watu wasiofahamika. Tulikuwa na makundi matatu, sasa jana baada ya Kufika Washington DC kutoka majimbo tofauti tofauti, tulikaa hoteli tatu tofauti. Punde wakatokea watu waliojifanya ni wenzetu wakisema kwamba, wamepata taarifa kwamba Mh. Rais angekuja siku ya Jumamosi.

Cha ajabu ni kwamba, viongozi wote wa msafara walipewa hela nyingi sana ambazo chanzo chake hazieleweki. Kati ya watu 106 waliofika na mabasi, kila mmoja alipokea siyo chini ya $25,000. Viongozi inasemekana walipewa hela nyingi sana. Haikuchukua muda mrefu tukawa tunaambiwa na viongozi wenzetu kwamba tutapelekwa sehemu tofauti tofauti kula chakula cha jioni. Kumbe muda huo ndio JK alikuwa anafika ukumbuni. Nilipopigiwa simu kutoka ukumbuni kwamba JK kafika, kuwakusanya kila mshiriki ikawa ni shida. Usiku tulipokutana ndo ukweli unafahamika. Kila mshiriki akaanza kushangaa ni kwa nini waligawiwa hela? Hakuna aliyetambua kwamba hawa walikuwa ni watu wa kikwete

Waliogawa hela muda huo walishatokomea. Hawa ni Watanzania wenzetu. Wadada wawili na Wanaume watatu ambao walijitambulisha kwamba wamepewa hela na mfadhili na mmoja wa wafadhili wetu ili kujikimu tukiwa Washington DC. Kwa hiyo hivi ndo mambo yalivyokuwa Jana. Wala msihofu, mapambano bado yanaendelea. Vita vinarudi Tanzania. Kikwete awaelezee watanzania kwamba hizo dola millioni tatu walizowanga wenzetu kiujanja zimetoka wapi?

Mwingereza

mkuu kwanza naomba niseme wazi kwamba wewe ni hatari kuliko huyu
unaye mpinga, hadithi yako ni ya mama na mwana, ina maana ukujua ni nani wafadhili wenu? wewe hukupata huo mgao?
kwa nini hukupata? hizo hela zilikuja kwenye mabox au masanduku? hapa jamii forum ulikuja kulisemea kundi husilo na control nalo kwa maana gani? una watafutia UVCCM popularity sio
mkuu hiyo ni USA uwezi kuwa na CASH yote hiyo,
Wewe ni SCAM na FRAUD una maana katika jamii na ulaaniwe wewe na kizazi chako

kwa upeo wa JK atakuwa ameusika na huu mchezo moja kwa moja hakukuwa na maandamano wa nini,
hii ni pima upepo ya JK lakini mwitikio ya shauku ya watu kutaka hayo maandamano yatokee ni salamu tosha kwa
jk na walamba kodi wenzake popote walipo,
ukombozi wa kidemocrasia utaletwa na watanzania wenyewe bila kupotoshwa na vibaraka na walafi
 
Wajinga ndio waliwao. Hapa tumeibiwa kiingilio.
 
Mwingereza

mkuu kwanza naomba niseme wazi kwamba you full of Sh.t na wewe ni hatari kuliko huyu
unaye mpinga, hadithi yako ni ya mama na mwana ina maana ukujua ni nani wafadhili wetu? wewe ukupata huo mgao?
kwa nin ukupata? hizo hela ziko kwenye mabox au masanduku?
mkuu huyo ni USA uwezi kuwa na CASH yote hiyo

Wewe ni SCAM na FRAUD una maana katika jamii na ulaaniwe wewe na kizazi chako

bora umenisaidia kumueleza. Mtaopokea vip pesa kutoka kwa mtu msiyemfahamu? Kwanini mbadilishiwd hoteli? Hapo ametudanganya. Atafute uongo mwingine.
 
Wajinga ndio waliwao. Hapa tumeibiwa kiingilio.

Ha ha ha! You said it well mkuu. Sasa sijui hao wafadhili walioko TZ ni CCJ au ni Mapacha watatu au nani hasa ambaye ameogopa kuwa wazi nyumbani (kufadhili maandamano nyumbani), akaamua kupeleka hela hizo kufanikisha maandamano US bila uangalizi makini. Ni afadhali hao wanao-ogopa kumpinga JK nyumbani watoke tu nyuma ya pazia (get out of the closet) kama mko serious na movement yenu; amasivyo mnajipotezea muda tu. Hii ni laana kwakweli hebu hizo hela wapeni maskini. Kweli kaaazi ipo!!!
 
bora umenisaidia kumueleza. Mtaopokea vip pesa kutoka kwa mtu msiyemfahamu? Kwanini mbadilishiwd hoteli? Hapo ametudanganya. Atafute uongo mwingine.

huyu mwingereza ni FRAUD/scam
mbwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa kabisa
 
halafu obama anakuja tanzania na kenya oktober, kikwete lazima atambe kutokana na safari yake hiyo ndiyo amemshawishi na obama, kumbe jamaa anakuja sijui kutembelea waanga wa mabomu wa ubalozi wa marekani, kama hayo maandamano hayakuwa trick basi mmetuangushaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
halafu obama anakuja tanzania na kenya oktober, kikwete lazima atambe kutokana na safari yake hiyo ndiyo amemshawishi na obama, kumbe jamaa anakuja sijui kutembelea waanga wa mabomu wa ubalozi wa marekani, kama hayo maandamano hayakuwa trick basi mmetuangushaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Mkuu wanamapinduzi wakweli hawakati tamaa. Kipindi hiki kila mtu ana ajenda zake. Kuna watu wanatumia kuwa-against kikwete kwa manufaa yao binafsi. Na kuhusu Obama, kumbuka Obama/Marekani wana-interest zao, na kutokana na uchumi wao ku-didimia hawana pakukimbilia zaidi ya Africa ndio kwenye free ulaji. Hii inakuonyesha tu mpambano ni mgumu sana. Unless unakielewa kikosi chako vizuri huwezi kuweka matumaini ya ukombozi (wengine wataweka silaha chini kwakurubuniwa na vizawadi).
 
Mi nilishangaa tu kwanza jina eti muingereza, wewe m@ l@ y@ at njaa kali mmbeba mabox huko unaweza kukataa dola m 3 wewe, mods mpige ban ya milele huyu kewnge kwa kushusha hadhi jf, yaani tunaconcetrate upuuz hapa
 
Walitangaza mno, ujuavyo ngoma inayolia sana haikawii kupasuka. Kumbuka Umoja wa wanawake Marekani ni wenyewe kwa ulaji, na wanajua mbinu za hali ya juu kumhifadhi, si shangai kama wameishia hewani kwani kuadhirika kwa ****** ni aibu ya Obama.
 
Watu wamekula mlungula?$25,000?Mwingireza mkuu stories zako haziko sawa.Sasa kama mlikuwa na ratiba ya mkutano mlikuwa mnamsikiliza nani tena kwamba JK anakuja mida gani?Eti mliambiwa mkale na kumbe wakati huo JK anaingia ukumbuni,what a crap!Sasa mna tofauti gani na wale wanaoenda kula wakati wa usimamizi wa kura?Hopeless!Na hayo mabasi mliyoyaandaa,umesema watu 106 waliyatumia na kwamba kila mmoja akapewa $25,000,na kwamba viongozi wa misafara walipewa pesa nyingi sana,wewe pia si kiongozi wa msafara?Unaposema walipewa ela nyingi sana kama vile ulikuwa hujui na wakati ulishasema kuhusu $3M hapo awali na kwamba mlizikataa? unatudanganya mkuu.Unachotaka kutuambia ni kwamba pesa hizo zimetoka kwa waandaaji wa maandamano walioko bongo?I doubt kama kweli ulikuwa kiongozi halafu eti hujachukua pesa.Acha hizo mkuu.Jf hapa we aint dumb.Kama unajuwa $3M zililetwa,sasa unajifanya vipi kushangaa eti pesa zimetoka wapi?Ama ni gulity consciousness?
 
Na wadau wengi tu Marekani ninaowafahamu ambao ni wabongo, kuanzia pwani ya Pacific hadi pwani ya Atlantic, wote ninaowafahamu wameniambia hawajui cho chote kinachoendelea zaidi ya kusoma hapa Jamii forums kama wewe na mimi tunavyofanya, yaekea labda kikundi cha watu fulani. Na kama kitu hicho kipo Kikwete asingefanya yote hayo, huenda angekata baadhi ya mambo ambayo yangefanyika eneo linaloongelewa kufanya maandamano. Tusubiri tuone kinachoendelea.
 
Mwingereza you are a moron, kwanza huyu dogo boya kweli hii email yake ya eliakimmalya@yahoo.com ameifungulia facebook account yenye majina Jakaya Kikwete. Sasa nashindwa kuamini kama yuko serious kweli. Kijana unatumika kwa kujua au kuto kujua. Endelea kutumika na ukimaliza kazi utatupwa kama rough rider.
 
Mwingereza you are a moron, kwanza huyu dogo boya kweli hii email yake ya eliakimmalya@yahoo.com ameifungulia facebook account yenye majina Jakaya Kikwete. Sasa nashindwa kuamini kama yuko serious kweli. Kijana unatumika kwa kujua au kuto kujua. Endelea kutumika na ukimaliza kazi utatupwa kama rough rider.

Huyo ni kikwete na watu wake kazini sasa sijui kwa misingi ipi?
au hiyo facebook walikuwa wameweka TEGO kujua nani ampendi VASCO DA DAMA
 
UPDATE:
Wana Jamii Forums. Kwanza tunanaombeni radhi kwa kuwaangusheni. Mpango mzima ulisukwa Tanzania. Wafadhili wetu wapo Tanzania na wachache nchini marekani. Hatuhusiani na CHADEMA kama wengine wanavyofikiria. Sisi ni Wana CCM waliochishwa na ufisadi wa Kikwete. Sisi ni Wana UVCCM ila waandamanaji ni watanzania ambao hawakuonysha itikadi zao za kisiasa. Ukweli ni kwamba, tumekuwa tukifuatiliwa kwa muda na watu wasiofahamika. Tulikuwa na makundi matatu, sasa jana baada ya Kufika Washington DC kutoka majimbo tofauti tofauti, tulikaa hoteli tatu tofauti. Punde wakatokea watu waliojifanya ni wenzetu wakisema kwamba, wamepata taarifa kwamba Mh. Rais angekuja siku ya Jumamosi.

Cha ajabu ni kwamba, viongozi wote wa msafara walipewa hela nyingi sana ambazo chanzo chake hazieleweki. Kati ya watu 106 waliofika na mabasi, kila mmoja alipokea siyo chini ya $25,000. Viongozi inasemekana walipewa hela nyingi sana. Haikuchukua muda mrefu tukawa tunaambiwa na viongozi wenzetu kwamba tutapelekwa sehemu tofauti tofauti kula chakula cha jioni. Kumbe muda huo ndio JK alikuwa anafika ukumbuni. Nilipopigiwa simu kutoka ukumbuni kwamba JK kafika, kuwakusanya kila mshiriki ikawa ni shida. Usiku tulipokutana ndo ukweli unafahamika. Kila mshiriki akaanza kushangaa ni kwa nini waligawiwa hela? Hakuna aliyetambua kwamba hawa walikuwa ni watu wa kikwete

Waliogawa hela muda huo walishatokomea. Hawa ni Watanzania wenzetu. Wadada wawili na Wanaume watatu ambao walijitambulisha kwamba wamepewa hela na mfadhili na mmoja wa wafadhili wetu ili kujikimu tukiwa Washington DC. Kwa hiyo hivi ndo mambo yalivyokuwa Jana. Wala msihofu, mapambano bado yanaendelea. Vita vinarudi Tanzania. Kikwete awaelezee watanzania kwamba hizo dola millioni tatu walizowanga wenzetu kiujanja zimetoka wapi?


FACEBOOK PROTEST AGAINST KIKWETE
TUNAOMBA MJIUNGE NA TUSAMBAZE HABARI KWA TANZANIA WOTE
**************************************************************************************


Tunapanga maandamano ya amani jijini Washington DC Rais Kikwete atakapowasili kwenye kikao cha DICOTA 2011. Tayari watu 150 wamekubasli kushiriki.Hii kumshinikiza kushugulikia swala la ufisadi na matatizo yanayowakabili wananchi wa kawaida. Maandamano yetu yataishia STATE DEPARTMENT. Naye apate Aibu, kwa kucheza na maisha ya watu, na kuiaca familia yake ikoroge nchi yetu. Ridhiwani anamilika robo ya uchumi wa Tanzania? Kwani Tanzania ni Tunisia....Ukitaka kushiriki tuma barua pepe kwenda eliakimmallya@yahoo.com

Tayari watu 974 wamesha confirm kujumuika katika maandamano haya ya amani....Jamani tuendeleeni, kushirikiana tumuaibishe huyu msanii , mtalii Vasco Dagama a.k.a Dr. Livingstone hadi atoke madarakani. Kadhalika tumeni barua pepe pamoja na malalamiko kwa wingi kwenda wiegertjr@state.gov ili kupinga Vasco Dagama kupewa VISA na wapambe wake. Ifahamike kwamba mimi siyo mwana CHADEMA wengine wanavyodai. Mimi ni mwana UVCCM tena ngazi ya Juu, lakini Kikwete hakufaa kuwa Rais, ndo maana Watanzania wanaumia. Mapinduzi yanakuja. Wasio na makaratasi, tunachoomba ni sala zenu tu. Watu wanaongezeka sana. Tayari tumefikisha watu 512 ambao wapo marekani ki halali na wako tayari kujiunga nasi kwa ajili ya haya mapinduzi

SERIKALI YA TANZANIA KUPITIA WATU WASIOFAHAMIKA, WAMEANZA KUTUTOLEA VITISHO PAMOJA KUJARIBU KUTUHONGA WAANDAAJI $3MILLION KUZIMA ZOEZI ZIMA LA MAANDAMANO. JIBU LETU NI KWAMBA, HATUWEZI KUUZA HUTU WETU NA UBINADAMU WETU. HIZO HELA WAPELEKE KWENYE MAHOSPITALI SIYO KUTUHONGA SISI. WAKAWAONGE WATANZANIA MILLIONI 40 WANAOKUFA NA NJAA SIYO SISI. MAANDAMANO LAZIMA, NA RAIS KIKWETE AJITAYARISHE. TUNAKUTANA NAYE MARRIOT WASHINGTON DULLES AIPORT NA HOTELINI KWAKE. TUMESHAJITAYARISHA

View attachment 37743


halafu hapa huwa tunadanganyanaga kirahi eti usalama wa taifa hawafanyi kazi!!!sasa mmeona kazi ya usalama wa taifa a.k.a.usalama wa viongozi waovu,vijana wamesambaratishwa kama kuku wa kienyeji na jk kafika dc kahutubia kapiga mpaka picha na 50.
 
Wakuu katika hali isiyo ya kawaida, kuna vijana ambao walikuwa wanaishi ghetto hapa Washington DC, leo hii wamekuwa ma-millionea. Jamaa wanaendesha Lexus GS-350.

Kuna tetesi kwamba kuna hela zimemwagwa kwa wingi na watanzania fulani. Nahisi hili n kundi la mwingereza waliokuwa dau nene na kumuachia mzee wa kaya kufanya mambo yake Dicota. Mie nilikuwepo ukumbuni, hali ilikuwa siyo ya kawaida.

Hatukuwa na taarifa ya kuja kwa JK. Ghafla tukaambiwa tukae upande mmoja, pasipo mategemeo akafika JK na milango yote kufungwa..Ila kuna uvumi kwamba kuna helza zimemwaga kwa vijana ambao walikuwa hawana kazi.. yaani ni hela nyingi.

Tutazidi kuwataarifuni mara data zikiendelea kumwagika, kwa maana siyo siri tena kwamba jamaa wamehongwa Dola millioni tatu..

Habari ndo hiyo.....

Wewe huu uchafu tumeisha ujadili sana kule kwenye maandamano ya USA yaliyokuwa yamepangwa na wana CCM
Kumbe janja yao tu kupima upepo
hizo dolla million 3 manajua ni shillingi ngapi? hayo maandamano yasiyojulikana na mtu USA nzima hela zote kama rushwa za nini?
kama kweli kuna DOLLA 3 million KUGAWANYWA USA basi haya maandamano yalikuwa ni ya kuwaibia CCM hela kwa misingi ya kwenda kuhonga waandamaji DC
Kuna wezi wa hela hapa
 
Ondoeni upumbavu wenu hapa, msifanye hili jukwaa la mataahira. Mods mnaurhusuje spams humu?
 
Haya maandamano ilikuwa ni decoyed ya kuwaibia CCM dola million 3 hakuna kitu kingine zaidi ya hicho.
hawa walamba kodi wameibiana hapa kwa kisingizio cha kwenda kuhonga waandamanaji DC
Hakukuwa na maandamano
 
Unastahili kutukanwa.
Ila kwa kuwa ukiandika upuuzi wowote wa kutunga juu ya JK mods wanafumbia macho basi mie nitakudharau na kpita tu hapa.
OTIS.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom