Maandamano ya CHADEMA Jijini Mwanza

Maandamano ya CHADEMA Jijini Mwanza

Ndio maana tunaandamana ili tupate uhuru wa kweli na hawa wavamizi wawe productive. Huelewi nini sasa.

Teh teh teh, sijaelewa ,baada ya maandamano then watakuwaje productive? Masanilo sijui amepita JKT lakini jeshini kuna sheria ya kwamba huwezi peleka jeshi vitani wakati unafahamu kabisa hiyo vita hushindi.
 
na polisi wamo humo sasa inakuwa kama tunisia, pale polisi walipogundua kuwa hata wao wanahusika na hali mbaya ya maisha...wakatumwa wakapige, wakajiunga na waangamanaji!!

viva chadema!
 
Jamani nina wasiwasi na hiyo picha. Picha hii siyo ya mwanza!!
Mji wa mwanza na vilima vyake vinafahamika vizuri sana. Naomba niwe wa kwanza kuikataa picha hiyo na klusema wazi kuwa imechakachuliwa!!!!
nikweli mkuu hiyopicha tunadanganyana,buzuruga kama unakuja town kulia kuna stend kubwa ya mabasi nakulia kunakituo kikubwa chamafuta cha gbp ambapo eneolote lina lami namajengo hakuna barabara ya vumbi,labda hapo nimaeneo yakasulu au mpanda,nakataa katakata hapo sio buzuruga mwanza.tusidanganyane.
 
chadema you rock the rock city, tupo pamoja wazee
 
Jamani tunalo Bunge lenye Kamati mbalimbali kufuatilia na kutetea mambo haya! Kweli maandamano kama haya ni kupoteza muda wa kazi, kusumbua wananchi, kuleta uchochezi na vurugu tu! Wengine wasiokwenda shule hawaelewi, wanawekwa tu kuandamana kufuata mkumbo na kupotezewa muda wa kutafuta Riziki. Uvunjaji wa Amani huanzia hapa kwenye maandamono. CDM be careful. Tumieni BUNGE P'se. Mkinyimwa kibali cha maandamano pia inakuwa nongwa. Muelewe nin muelewe? Do you know the meaning of Piece?
 
Mimi natoka.
Nawaachia usia.
Sisitizeni watu kufanya kazi kwa bidii.
Umasikini wote wa watanzania msiwadanganye kuwa unatokana na serikali.
Kufeli kwa form four msiwadanganye kuwa kumesababishwa na serikali.
Waambieni ukweli, bidii unashinda changamoto nyingi. Ndio maana katika umasikini uliopo kuna wanaofanikiwa.
Ndio maana katika matokeo mabaya ya form four kuna wanaofaulu.
Waambieni ukweli, kuwa bila kufanya bidii hata ikiingia Chadema madarakani wataendelea kuwa masikini.
Waambieni ukweli kama mnajali taifa hili.
Msipofanya hivyo mtakuwa mnapoteza muda wenu na wa wale mnaowadanganya, kwa sababu HUTUTAWARUHUSU kushika dola.

Toka kwani wakati unaingia hapa kuna mtu ulimpa taarifa,nenda zako .
 
Mnapoeza muda wa watu kufanya kazi. Watu wanataka barabara, hospitali, shule bora n.k. Hawataki maandamano.
Acheni uzushi, kahamasisheni shughuli za maendeleo.

Maandamano ya CDM ni kupinga Bei ya umeme na kulipwa DOWANS. wewe unasema watu wanataka Barabara, Hospitali na shule Swali je tukae gizani? hujui Pesa za barabara ndo hizo zinazoenda DOWANS. Tafakari kabla ya kusema.
 
Huo mchiriku mnaocheza Mwanza unaweza kuufananisha na kazi iliyofanyika Egypt?
Maandamano mko kwenye gari?
Maandamano mnajiandaa kwa kuingia saloon kwanza ndio mhudhurie, halafu mnajiita wapiganaji?!!!

Mkuu mbona kuna picha hapo ya maandamano watu wanatembea kwa miguu? kwani sio Mwanza hapo? wamechakachua?
 
Mnapoeza muda wa watu kufanya kazi. Watu wanataka barabara, hospitali, shule bora n.k. Hawataki maandamano.
Acheni uzushi, kahamasisheni shughuli za maendeleo.

Maendeleo hayawezi kuja katikati ya serikali ya kidharimu na kifisadi. Kinachofanywa sasa ni kuwaandaa wananchi kisaikolojia ili muda muafaka wa ukombozi ukifika mambo yawe rahisi. Muda wenyewe ni 2015.
 
Kwa hiyo maandamano ndio yataleta hospitali?
Vyama vinavyojifanya kujali kwa nini visihamasishe foundations zitakazofanya miradi ya maendeleo kwa mfano?
Maandamano feki ni unafiki tu!

Mimi nadhani unaushabiki wa kijinga, serikali iliyopo madarakani ni ya chama kipi? Unadhani bila ya kuiamsha serikali ya ccm hayo mahospitali na barabara zitajengwa??

Wewe shida huna, kitambi kimekushuka kwa ufisadi, hivyo tulia acha wanyonge walio wengi wadai haki zao
 
Jamani tunalo Bunge lenye Kamati mbalimbali kufuatilia na kutetea mambo haya! Kweli maandamano kama haya ni kupoteza muda wa kazi, kusumbua wananchi, kuleta uchochezi na vurugu tu! Wengine wasiokwenda shule hawaelewi, wanawekwa tu kuandamana kufuata mkumbo na kupotezewa muda wa kutafuta Riziki. Uvunjaji wa Amani huanzia hapa kwenye maandamono. CDM be careful. Tumieni BUNGE P'se. Mkinyimwa kibali cha maandamano pia inakuwa nongwa. Muelewe nin muelewe? Do you know the meaning of Piece?

Ni kweli Bunge lina kamati mbalimbali lakini walio wengi kwenye hizo ni wa Chama gani? Wanachotetea chama "B" siyo kilicho kenye sera ya chama "A"
 
Hamjawahi kuhamasisha hata ujenzi wa shule ya kata, kazi yenu kuandaa maandamano tu. Huo ni unafiki wa kisiasa, hamna moyo wa kweli wa kuleta maendeleo Tanzania.

Acha uvivu wa kufikiria, watu wanataka huduma bora umeme, maji na barabara, Ni kweli kabisa lakini pesa za kufanyia mambo hayo inachukuliwa kinyemela na watu wachache kama wewe, au waliokutuma wewe hapa JF. tumesema hatutaki.

mfano ni pale serikali inapokuwa haina pesa za kununua mitambo ya kudumu ya umeme, lakini ina pesa za mchezo kama kuilipa Dowans hii hikubaliki tumeshakaa majumbani tangu 1961, lakini hakuna kinachofanyika zaidi ya watu kutuibia.

Hatutaki peoples power!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kweli kabisa amechoka anasinzia kabisa!

kikwete+msibani.jpg

Umenicha hoi kabisa. Mbavu sasa zinauma kwa kucheka.....................!! We Rev kiboko!!
 
Mnapoeza muda wa watu kufanya kazi. Watu wanataka barabara, hospitali, shule bora n.k. Hawataki maandamano.
Acheni uzushi, kahamasisheni shughuli za maendeleo.

Nawe hufanyi kazi unasoma thread zisizo kuhusu. Chapa kazi achana na JF.
 
Niwekee kwenye PM best.....hata ile ya wafahidhina uligoma! Kila laheri usiache kuandamana siku yakiwa kwenye maeneo yako....Pipoz Pouwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
mimi leo nipo mwanza nipo hapa kwa biashara zangu,ila namimi baada ya kuwaona viongozi wetu wako ktk magari wanakula kiyoyozi wanyonge wanaungua najua nimekodi taksi nawasubiria viwanja vya furahisha,ila kwahakika watu niwengisanasana,nasubiri viongozi watatoa hotubagani,kwangu hilo ndio kubwa kulikoyote.
 
Maandamano ni mojawapo ya shughuli kama kujenga barabara, kwani ujumbe utakaotolewa na waheshimiwa ktk hotuba ya leo utaihamasisha serkali ilioko madarakani kubadilika au kufanya vizuri ktk utawala wake.
 
Hata Egypt, Tunisia, na Libya kuna watu wa aina ya ZeMacorporo na wanafaidika pia na mabadiliko ya mfumo wa utawala kwahiyo asamehewe bure tu. Huwezi ukahamasisha shughuli za maendeleo wakati serikali iko busy na ufisadi, ubabe na ukandamizaji wa haki za binadamu! Maandamano ni njia ya amani (kama polisi wa CCM hawataleta vurugu) ya kufikisha ujumbe kwa serikali iliyopo madarakani (hasa yenye kiburi kama ya CCM).
 
Andamaneni halafu kesho asubuhi au wiki ijayo mtuambie hayo maandamano yameleta mabadiriko gani?
Sio mnaandamana kila siku na hakuna kinachobadiria lakini bado mnaandamana tena na tena na tena.
Kuwa insane maana yake ni " to do the same thing again and again and then somehow expect different results". Mkiandamana kila siku na hakuna kinachobadirika mjue mko insane.

Kama watanzania wanavyochagua ccm kila mwaka na hakuna mabadiliko??
 
Back
Top Bottom