Maandamano ya CHADEMA Jijini Mwanza

Maandamano ya CHADEMA Jijini Mwanza

Kweli kabisa amechoka anasinzia kabisa!

kikwete+msibani.jpg
Rev Masa, wewe kiboko maana huwa unatwanga nyoka rungu ya kichwa. tehe tehe tehe!
 
ZeMakopolo Hujui kitu wewe HIVI UMEME ULIVYOKUWA UNAKATIKA HUKUONA?
AU WEWE FISADI ? MAANA MAFISADI HAWAKUJUA ADHA YA UMEME!
ZEMARCOPOLO UNAJUA MAANA YA KUDAI WEWE? WEWE FISADI MKUBWA!
HIVI UONI MISRI WATU WAMEANDAMANA MPAKA RAIS AKANGATUKA?
HIVI ZE MARCOPOLO UMETUMWA! UNAJUA NGUVU YA UMMA WEWE?
UNAKALIA TU UFISADI LAKINI HUJUI WATANZAIA WANAVYOPIGIKA KWA SASA!

WEWE ZEMARCOPOLO UNAFIKIRI SHULE ZINALETWA NA MAFISADI
AU WASHAKUHONGA WEWE?

Huo mchiriku mnaocheza Mwanza unaweza kuufananisha na kazi iliyofanyika Egypt?
Maandamano mko kwenye gari?
Maandamano mnajiandaa kwa kuingia saloon kwanza ndio mhudhurie, halafu mnajiita wapiganaji?!!!
 
Baya zaidi wakitoka hapo na njaa usiku watakuvamia wewe hata panga la shingo watakupa, shauri yako.
Ndio maana tunaandamana ili tupate uhuru wa kweli na hawa wavamizi wawe productive. Huelewi nini sasa.
 
Fedha iliyotumika kwa ajili ya haya maandamano ingewafaa sana wakazi wa GONGO LA MBOTO, maslahi ya Taifa kwanza.
Kipi bora, kuzuia mabomu yasilipuke, au kutaka yalipuke halafu uonekane wa kwanza kutoa rambirambi?
 
Bila picha mi sioni raha ya hii thread. Nashukuru lakini kwa taarifa.
 
Cha msingi sio kujua theme bali ni kujiuliza jamii itanufaika vipi na maandamano hayo na je, jitihada zinazotumika kuandaa maandamano zisingeweza kutumika kuleta manufaa zaidi? Hawa wote wanafiki tu!

Akili zako zipo matakoni? Kwani wananchi wangapi wananufaika na upupu wa kikwete kutapanya rasilimali kwa marafikize? Au unamaanisha nini kusema wananchi wanafaidikaje(labda wenye nchi ni wewe,familia yako na kikwete+familly,lowasa+familly,rosta+co..)..
 
Hatuko kwenye mipasho hapa ongea mneno yanyoeleweka sio kauli zinazonuka uozo wa fikra sisi sio watanzania wa mwaka 47 tunajua tunachofanya unaposema hamjawahi kuhamasisha ujenzi wa shule unamaanisha nini ? Ndo nyie mliosema ccm haina mafisadi na Dr akiwataja itakuwa kashfa hivyo mtamshitaki acheni uhayawani mbona hamjamshtaki sie tushachoka longolongo tunataka maendeleo ya kweli.

Hamjawahi kuhamasisha hata ujenzi wa shule ya kata, kazi yenu kuandaa maandamano tu. Huo ni unafiki wa kisiasa, hamna moyo wa kweli wa kuleta maendeleo Tanzania.
 
We Zemarcopolo, Je una cheti cha daktari kinachohusiana na akili? Kama ujui umuhimu wa maandamano kawaulize wa Tunisia, Wa Misri, n.k. Sio unapinga tu. Leo hii we ukiambiwa utoe mchango hutoi. Pia we mwenyewe ukiambiwa ujiunge hata kwenye maandamano ya kuchangia wahanga wa Mambomu huji. Kazi yako ni kuandika email na posting tu ndicho unaweza. Waache wenye uchungu waandamane. We unaona kila kitu poa unapata milo mitatu kwa siku, usafiri unao, Umefunga solar & Generator, Nyumba safi yenye kiyoyozi, TV 42 inches n.k. Sisi wengine tunapata mlo mmoja tu tena kwa sida, kila kukicha hatujui siku itaisha vipi.
 
Kama kuna anayeweza kunitajia kitu kimoja kilichopatikana kwa chama fulani cha siasa Tanzania kwa njia ya maandamano aweke hapa. Kila siku mnaandamana na kutoa hotuba zisizo na tija halafu jioni mnarudi nyumbani. Mantiki yake nini sasa?
Hivi huwa mnakaa na kuevaluate mafanikio yanayopatikana kutokana na hayo maandamano?

"To greed, all maandamano is insufficient"
 
Kwa hiyo maandamano ndio yataleta hospitali?
Vyama vinavyojifanya kujali kwa nini visihamasishe foundations zitakazofanya miradi ya maendeleo kwa mfano?
Maandamano feki ni unafiki tu!

Don't waste time by arguing with this fool, who believes development will be forged through EPA, Richmond, Dowans, Deep Green, etc...
 
Mbona haya maandamano sio live tena, tunaomba updates tafadhali mlioko Mwanza.
 
Asante kwa kutujuza, na tunategemea watu hawataanzisha zaili makusudi ili kuyapa umaarufu maandamano ya leo.
 
wewe maandamano unayoyataka ni ya mshikamano. tunawajua nyinyi, wivu tu umewajaa. mnaona nchi inawashinda mnasingiziaMaandamano. Mbona nchi za Kiarabu zimefanikiwa ktk kuandamana? Wewe subiri upepo ugeuke ndipo utakapojua nini kitawatokea. Kama mgeshinda kihalali bila ya wizi leo hii msingestuka hivi.Na kama mgechaguliwa kwa % mlizojitangazia. watu wote wangewaunga mkono. Soma alama za nyakati.Nchi imeshamwagiwa Petroli cheche tu Moto utawaka.

Msipoteze muda kujibizana na huyo ZeMarcopolo!!!! Inawezekana kabisa yuko kazini!!!!

Tiba
 
Dr is bored now afadhari asimamie MATEMBEZI YA AMANI...hivi ni nini kinategemewa kutokana na matembezi haya?

Kutolipa Dowans?
Gharama za maisha kushuka?

Je wakilipwa na gharama za maisha zikiendelea kwenda juu nini kitafanyika matembezi mengine mbeya?
 
Ndugu yangu unaepinga maandamano waonekana umekunywa maji ya bendera za kijani. unapinga bila critics point, umetumwa?
 
naona wananogewa na maandamano na speaches za President wa JMT 2o15, Dr. Slar; kiasi cha kujisahau kutuhabarisha!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mimi natoka.
Nawaachia usia.
Sisitizeni watu kufanya kazi kwa bidii.
Umasikini wote wa watanzania msiwadanganye kuwa unatokana na serikali.
Kufeli kwa form four msiwadanganye kuwa kumesababishwa na serikali.
Waambieni ukweli, bidii unashinda changamoto nyingi. Ndio maana katika umasikini uliopo kuna wanaofanikiwa.
Ndio maana katika matokeo mabaya ya form four kuna wanaofaulu.
Waambieni ukweli, kuwa bila kufanya bidii hata ikiingia Chadema madarakani wataendelea kuwa masikini.
Waambieni ukweli kama mnajali taifa hili.
Msipofanya hivyo mtakuwa mnapoteza muda wenu na wa wale mnaowadanganya, kwa sababu HUTUTAWARUHUSU kushika dola.
 
Back
Top Bottom