mbenge
JF-Expert Member
- May 15, 2019
- 4,576
- 9,816
Vijana jiepusheni sana na kunji ktk kipindi hiki tuelekeapo siku za kampeni za uchaguzi mkuu. Uwepo wa tishio la COVID-19 ndilo limewafanya ninyi sasa hivi kuwepo vyuoni. Kama isingalikuwa kuwa hivyo mngejikuta bado mpo ktk kipindi cha kusubiri kwa "finalist" kumalizia masomo yao, ama wengine wakijiandaa kuingia miaka ya mbele zaidi kwa "undergraduate studies" zao.Hamjambo wanabodi
Moja kwa moja niende kwenye mada husika, kutakuwa na maadamano ya amani dhidi ya bodi ya mkopo nchini (HESLB), maandamano haya yataanza siku ya jumatatu tarehe 27/07/2020 na kuendelea mpaka pale HESLB itakapo rejea masharti ya mkataba na kutenda haki kwenye utoaji wa pesa ya kujikimu(boom).
.
Maandamano haya yatafanyika kwa kufuata hatua zifuatazo:-
.kutoingia darasani kuanzia jumatatu na kuendelea mpaka pale pesa itakapo kuja yote kutoka HESLB
..
Kwanini maandamano?
Kwasababu mkataba ulipo kati ya mnufaikaji wa pesa ya kujikimu ni sh 2, 040, 000/=kwa mwaka ambapo hulipwa sh 510, 000/= kwa kila phase. Mwaka wa masomo huwa una phase 4 za ulipaji. Kilichotokea baadhi ya vyuo wanaambiwa wakasaini boom la sh 306, 000 /=kwa UDSM na sh 206, 3000/= kwa UDOM, vipo vyuo hadi laki moja.
Ukirejea mkataba haujawahi kusema kwamba ikitokea siku zimepungua na pesa itapungua.
.
Kama ndio hivyo basi nasi mtupunguzie ADA maana muhula umekuwa mfupi na siku zimepungua sana.
.
Vijana wa kiume na kike naomba tuungane kwa pamoja kufanikisha wazo hili najua nalo litapita lakini tunaihitaji kuwakumbusha bodi ya mikopo kwamba hatujalala na tupo hapa kupigania haki zetu kwa pamoja tunaweza.
.
Vijana ndio taifa la kesho, amka pambana dai haki yako na tekeleza wajibu wako.
......kwa UDSM tukutane 'Revolution Square' jumatatu SAA 2 asubuhi....
..
..
#MAANDAMANO YA AMANI
View attachment 1515754
"What I can say, "You have been targeted and momentumly to be provoked intentionally, you now in trap to be victims of circumstances. This cowardly plan has been purportedly initiated as means for your expected actions and certain expected consequences'.
Mtulize akili kwa kuwa baba zenu tuliwahi kuingizwa mkenge wakati wa uraisi wa UDASA ya wakati huo ya akina Ngwilimi na Mtungilehi. Lazima mkumbuke vyuo vikifungwa sasa imekula kwenu mpaka baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu.
Nyinyi ni jeshi la vijana wenye kuogopa na wasioaminika kwa chama tawala. Ila hamtambui umuhimu wa umoja wenu na kupata jukwaa rasmi la kuwakilisha maslahi yenu. Wengi wenu ni wakereketwa upande wa upinzani, lkn bado mnaabudu na ktk madhabau ya CCM ili muweze kuishi kinafiki na kuonekana, kisa eti kupata kufikiriwa ktk ajira za umma.
Naomba nihitimishe kwa kusema, tulieni vyuoni na kuongeza bidii ili mpate kufaulu mitihani yenu ya "semister" hii. Epukeni ushawishi wowote ule wa kuwataka kufanya kunji ama kususia masomo ili kuishinikiza serikali. Itakula tu kwenu, kwa sababu sisi wazazi wenu wiki ijayo tutakuwa 'busy" na mambo mawili tu ambayo yatakuwa na "public attention", pengine niwape faida kwa kuyataja;
1. Ujio wa Tundu Lissu
2. Maombolezo ya Rais Mstaafu, Hayati Benjamin William Mkapa