KERO Ucheleweshwaji wa malipo ya pesa za kujikimu (boom) kwa wanachuo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

mjandwasafi

Member
Jun 6, 2023
10
19
Hello habari za majukumu.

Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha kikatoliki Ruaha (RUCU) kilichopo Iringa.

Kwasasa changamoto ambayo wanafunzi wengi tunaipotia ni ucheleweshwaji wa pesa za kujikimu (meals and accomodations) ambayo ni sehemu ya boom.

Kitu kinachotushangaza na kutusikitisha wanafunzi wengi ni kwamba baadhi ya wanafunzi hususan waliopo mwaka wa kwanza na baadhi ya wale waliopo mwaka wa pili tayari wamepokea pesa hizo na wengi wao wapo field (na hawa ni wale ambao husaini fedha hizo kwa kupitia HESLB app) na kundi kubwa la wale tuliobaki chuoni mwaka wa tatu na nne ( Kwa upande wa sheria) ndio tunakumbana na changamoto hii. (tunaosaini pesa hizo kwa alama za vidole)

Kwa kawaida pesa hii huingia baada ya siku 60 ambapo ni sawa na miezi 2 kwa semester na kwa mara ya mwisho pesa hii iliingia tarehe 20/12/2023 lakini cha kushangaza mpaka wakati huu naandika haya pesa hii haijaingia ikiwa ni tarehe 18/03/2024. Na hakuna taarifa yoyote ya kuridhisha kutoka kwa viongozi wanaohusika na suala hilo chuoni.

Kimsingi hali za watu ni mbaya sana, uendeshaji wa maisha umekuwa mgumu mno. Na wengi wetu ukizingatia tumetoka familia ambazo siyo imara sana upande wa uchumi kwani pesa hizo ndizo hutuwezesha kujikimu kwa muda wote tunaokuwa chuoni.

Ninaomba mamlaka husika ziingilie kati suala hili kunusuru hali za maisha yetu.

Asante.
 
Hello habari za majukumu.

Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha kikatoliki Ruaha (RUCU) kilichopo Iringa.

Kwasasa changamoto ambayo wanafunzi wengi tunaipotia ni ucheleweshwaji wa pesa za kujikimu (meals and accomodations) ambayo ni sehemu ya boom.

Kitu kinachotushangaza na kutusikitisha wanafunzi wengi ni kwamba baadhi ya wanafunzi hususan waliopo mwaka wa kwanza na baadhi ya wale waliopo mwaka wa pili tayari wamepokea pesa hizo na wengi wao wapo field (na hawa ni wale ambao husaini fedha hizo kwa kupitia HESLB app) na kundi kubwa la wale tuliobaki chuoni mwaka wa tatu na nne ( Kwa upande wa sheria) ndio tunakumbana na changamoto hii. (tunaosaini pesa hizo kwa alama za vidole)

Kwa kawaida pesa hii huingia baada ya siku 60 ambapo ni sawa na miezi 2 kwa semester na kwa mara ya mwisho pesa hii iliingia tarehe 20/12/2023 lakini cha kushangaza mpaka wakati huu naandika haya pesa hii haijaingia ikiwa ni tarehe 18/03/2024. Na hakuna taarifa yoyote ya kuridhisha kutoka kwa viongozi wanaohusika na suala hilo chuoni.

Kimsingi hali za watu ni mbaya sana, uendeshaji wa maisha umekuwa mgumu mno. Na wengi wetu ukizingatia tumetoka familia ambazo siyo imara sana upande wa uchumi kwani pesa hizo ndizo hutuwezesha kujikimu kwa muda wote tunaokuwa chuoni.

Ninaomba mamlaka husika ziingilie kati suala hili kunusuru hali za maisha yetu.

Asante.
Post jukwaa la habari na hoja mchanganyiko.
 
Haya mambo wahusika wanayakalia kimya tu kimsingi huku hali ni mbaya mno
Nimeshangaa uliposema baadhi ya wanachuo wa mwaka wa kwanza na wa pili wameshasaini boom kitu ambacho sio kweli.

Hakuna aliyesaini boom la tatu kila mahali madogo wanalia kuchelewa kwa boom sasa sijui chuo gani wameanza kupokea boom.

Kwamba this time boom linatoka kwa mafungu kwamba baadhi ya vyuo waanze kupokea halafu vyuo vingine bado?
 
Nimeshangaa uliposema baadhi ya wanachuo wa mwaka wa kwanza na wa pili wameshasaini boom kitu ambacho sio kweli.

Hakuna aliyesaini boom la tatu kila mahali madogo wanalia kuchelewa kwa boom sasa sijui chuo gani wameanza kupokea boom.

Kwamba this time boom linatoka kwa mafungu kwamba baadhi ya vyuo waanze kupokea halafu vyuo vingine bado?
Usinibishie na wala sipo hapa kwasababu ya kutafuta kuwa famous mimi nipo pale na ninachokwambia ndio uhalisia kwasababu nipo pale
 
Ni kweli kabisa kiongozi lakini changamoto iliyopo mazingira ya familia tunazotoka siyo rafiki sana kiasi kwamba tunaweza kukaa muda mrefu bila utegemezi wa pesa za serikali ni zaidi ya miezi miwili sasa kama ambavyo utaratibu wa pesa hizo inavyoelekeza




Serikali inafatilia na mtaingiziwa hela muda sio mrefu.

Kuwa na subra wiki haizidi.

Naelewa maisha ya chuo hasa kwa familia zetu za kimasikini.
 
Serikali inafatilia na mtaingiziwa hela muda sio mrefu.

Kuwa na subra wiki haizidi.

Naelewa maisha ya chuo hasa kwa familia zetu za kimasikini.
Kinachonisikitisha ni kwamba kwenye taasisi yetu wanafunzi waliopo mwaka wa kwanza na baadhi ya wale waliopo mwaka wa pili (wanaotumia HELSB APP) wamepata tayari tangu week iliyopita changamoto ni upande wetu ambao tunatumia finger print kusaini pesa hizo
 
Wala hatufikirii kufanya fujo ama uchochezi wa aina yoyote Ile jambo la msingi hapa wahusika ni kuelewa kuwa sisi pia ni binadamu na ukiona tunatokea mpaka mitandaoni basi ni wazi kuwa hali ni mbaya
Haki yako haiombwi, unaidai , ikiwezekana unalazimisha upewe.

Hayo malalamiko mtalalamika, boom lijalo watawafanyia hayo hayo..
Unadhani hao watu wanajali huo ubinadamu?
 
Back
Top Bottom