Maandamamano ya Kenya kuhamia Tanzania?

duh.. I tried to go Red Lobster twice.. I had to give up kuna watu wanagombana na miguu ya lobster utadhani wako kwenye mashindano... halafu kuna waswahili a.k.a black americans wanaiweka ile miguu kwenye sahani utadhani wanafanya presentation ya "nani kala sana"..

talking about date.. good you mentioned.. maana ya kwangu we are going to a movie and stop at a McD... for a quick Big Mac and a Double Quarter Pounder with Cheese..! Now..tell me a lobster can beat that..
 
hili siyo suala la msiba... impression ambayo nilikuwa nayo niliposikia habari hii na leo iko confirmed na baadhi ya vyombo vya habari, maandamano yalikuwa na lengo la kumuunga mkono Raila. Ni tofauti na maandamano ya kutaka amani irejee na kuwataka wahusika wote (Raila na Kibaki) wote watumie nafasi na uwezo wao kuhakikisha kuwa amani inarejea Kenya.

Kitendo cha kutaka upinzani wa TAnzania utumike kuhalalisha madai ya Raila haukuwa uamuzi wa busara hasa wakati huu ambapo hali bado haijatulia nchini. Hekima inatusukuma kuamini kuwa badala ya kujitokeza na kujaribu kuchochea madai ya upande mmoja itakuwa ni vizuri kama tungejitokeza na kuzitaja pande zote mbili zikae chini without preconditions na watafute suluhu kwanza kabisa katika kurejesha amani na utulivu na pili kuamua nini cha kufanya ambapo nothing should be off the table.

Sijatoa hukumu bali nimeelezea my own take na kama wao hawakutlia chini na kufikiri kwa makini matokeo ya maamuzi yao hayo Polisi wamesaidia kuonesha ukosefu wa hekima. Siyo kila kitu kinaenda na maandamano!

MKJJ, Na wengine anti maandamano

Huwa napenda wakati mwingine kukaa kimya ila nakereketwa. Wakati Marekani na Uingereza wanaipiga Iraq na kuua mamia kwa maelfu wote tulilaani tukaandamana (wakati bado hali ni tete Iraq).

Dafur kumekuwa sio shwari maandamano yalifanyika. Kikatuni cha Mohamed ambacho kingeweza kuvuga amani(bado watu waliandamana kwa amani na mifano meninge...) MKJJ na wengine mnaopinga maandamano mmekuwa mbele sana kutoa ,maoni jinsi uchaguzi ulivyokuwa unaendelea na kulaani Kibaki et al kwa walichokifanya. sasa mnasema maandamano yamekosa hekima

Sioni ni Hekima gani unayozungumza hapa (kama Kibaki et al walikua na hekima na wangeiba kura??? Na kama bado wangekuwa na Hekima baada ya kuona mambo yameharibika kwa nini wasijiuzulu???? Kama Kibaki hana Hekima kwa nini awe treated kama mtu mwenye hekima????

Wote tunakerwa na mauaji lakini hekima ya Kibaki iko wapi kama anajua yeye ndio chanzo cha haya yote??? Je, mtu akikutoboa jicho moja then anakuja ili akutoboe la pili, Bado utaendelea kumwita Rafiki yako?

Wengi wetu hata MMJ et al mmekuwa mkilaani wizi wa kura na mmekuwa mkishabikia jinsi wakenya wanajaribu kufuatilia haki zao.Tena mmekuwa wa kwanza kusema Serikali ya Tz itoe tamko serikali yetu imeshindwa sasa wapinzani wanataka kusema then wamekosa Hekima.

Mimi bado naona ni jambo la Busara kufanya maandamano na Polisi hawana mamlaka kuzuia utashangaa leo watakuwa wametumia nguvu nyingi kuzuia maandamano yasifanyike kuliko wangewaruhusu.

Nakereka, nakereka, nakereka jinsi watanzania wakati mwingine tulivyo na nidhamu ya woga.

nakereka, nakereka
 
bowbow;

Hivi unakumbuka kilichotokea kwenye uchaguzi wa Marekani mwaka 2000 ambapo George Bush alitangazwa Mshindi? Unakumbuka yaliyotokea Florida ya "hanging chad" na wadogo zake. Unajua jinsi gani Supreme Court ya Florida ilivyojaribu "kisheria" kumpa ushindi Gore ambapo baadaye wakawa thwarted na US Supreme Court ambayo nayo ikimpa ushindi George Bush. Unakumbuka Jaji Mkuu Rehnquist baadaye alijuta kwa Mahakama yake kuchukua kesi hiyo?

Unajua ni kwa kiasi gani Democrats walijihisi kuwa wameibiwa uchaguzi na kuna baadhi hadi leo hawatambua ushindi wa Bush wa mwaka ule? Unajua kuna watu waliangusha machozi siku ile na wengine kushindwa hata kula kutokana na kitendo cha "injustice" walichofanyiwa (au kuhisi kufanyiwa).. ?

Je ulisikia wameanza kukata mapanga na kuchomeana nyumba, magari, n.k ? Inawezekana kwa sababu wao ni "wazungu" na "wamarekani" mambo ya kuchinjana hayawezi kutokea.. au labda wenzetu wana "moral superioriy" ambayo inawafanya kujizua kufanya mambo ya kinyama kama hayo kwa sababu za kisiasa. Unajua hata Marekani pamoja na Demokrasia yao yote hawawezi kuandamna kirahisi rahisi na ni upotoshaji mkubwa wa demokrasia kudai kuwa watu wakitaka kuandamana basi waandamane tu hata kama Polisi wanawakatilia.

Hakuna taifa duniani linaloweza kuruhusu hivyo. Hata hivyo, haki ya wananchi kuonesha manung'uniko yao dhidi ya serikali yao haiwezi kuondolewa na chombo chochote kile, kwani haki ya kutawala inatoka na kubakia na watu wenyewe. Kama Wakenya wanaamini kuwa Kibai siyo rahisi halali na ni rahisi wa "bandia" kama kijana mmoja wa Chuo Kikuu alivyomwita leo, basi wanayo haki ya kuandamana hadi Ikulu na kumfukuza! Hayo yalitokea Ukraine na Georgia! Hiyo ni haki ya wananchi wa Kenya.

Sasa, kuna baadhi ya watu wanataka tuamini japo kwa mbali kuwa masuala ya mauaji hayana hisia za ukabila na ni suala la upigaji kura na uhesabuji kura. Watu hawa wanataka tuamini kuwa machafuko ya kisiasa Kenya yametokea kwenye hali tupu (vacuum); kwamba hayana historia na hayana chanzo kingine. Watu hawa wanataka tufumbe macho na tusiangalie vikolombwezo vya ukabila ambavyo vimetokea kabla ya kupiga kura, siku ya kupiga kura na baadaye baada ya kupiga kura. Watu hawa hawawatendei haki watu wa Kenya.

Machafuko haya ya kisiasa hayakutokea hewani. Kama vile machafuko ya Rwanda miaka karibu 18 huko nyuma machafuko ya Kenya yanachanzo. HIsia ya ukabila nchini Kenya ni ya zamani kama historia ya nchi hiyo. Kuna makundi ya watu ambao wanaamini tena kwa viapo kuwa Wakikuyu ni kabila lililopendelea na kujipendelea mno tangu utawala wa Mzee Kenyatta na baadaye Moi. Watu hawa wanaamini kabisa kuwa Wakikuyu walipata nafasi nyingi na kulindwa kwa kiwango kikubwa na KANU na viongozi wa juu wa nchi hiyo na matokeo yake ni resentment toward the Kikuyu.

Kwa wale ambao tumewahi kuishi Kenya au kutembelea pale mgawanyiko huu wa hisia za kikabila umejikita sana kwenye jamii ya Kenya. Kuna mahali mtu huwezi kwenda na Mkikuyu kwa sababu atasema "ni kwa Mluo" na wakati mwingine huwezi kwenda na mwenyeji wako Mluo kwenye joint ya Wakikuyu kwa sababu ni "ya Wakikuyu". Wenyewe wa Kenya labda wamezoea hilo kama "hali halisi".

Hisia hizi za manung'uniko, kufanywa duni, na kwa namna fulani kujiona bora zaidi (upande wa wa Kikuyu) zimedumu kwa muda mrefu na zimekuwa zikitafuta mahali pa kutokea.

Uchaguzi huu uliopita ilikuwa ni nafasi muafaka ya mgawanyo huu kuchorwa ardhini moja kwa moja au kuvunjwa moja kwa moja. Kibaki na wale waliomuunga mkono waliendelea kuonesha hisia ya "ubora wa Wakikuyu". Ingawa maneno mengi yametolewa kama maneno ya kisiasa lakini kauli zao kampeni zilikuwa zimejaa sentiments hizi sana. Raila na upande wake walikuwa wanajiandaa kuvunja dominance ya Wakikuyu katika serikali ya Kenya kwa kutumia sanduku la Kura.

Wakati ameenda kupiga kura Raila alishindwa kutokana na matatizo fulani ya kiutendaji. Kwa haraka akaenda kwenye vyombo vya habari na kudai "ukabila"! kuwa kuna jaribio la kuwafanya watu wa makabila fulani wasipige kura. Baada ya kura kupigwa na matokeo kuanza kucheleweshwa hisia za kuchezea kura zilianza kila pande ikihisi mwenzie anafanya mchezo mchafu.

Kosa kubwa ni kitendo cha Tume ya Uchaguzi ya Kenya kuendelea na kutangaza matokeo wakati wakiona taratibu zinakiukwa. Na kosa kubwa ambalo limeonesha udhaifu mkubwa wa Kivuitu ni kumtangaza Kibaki Rais na hivyo kuharakisha kuapishwa kwake. Kitendo hicho hakikusaidia fukuto la hasira ambalo lilikuwa limeanza kuingia nchini Kenya.

Kitendo cha Jeshi, Mahakama na Polisi kumtambua mara moja Rais Kibaki (kwa ushahidi wa uwepo wao kwenye kuapishwa) kilikuwa ni kile ambacho kinaitwa "ufito wa mwisho uliovunja mgongo wa ngamia". Watu wa Kenya hasa vijana waliona kuwa "wameibiwa" haki yao. Na hapa ndipo makosa ya Raila yalipojitokeza.

Raila alikuwa anajua passion ya watu kwenye uchaguzi huu. Uamuzi wake wa mwanzo wa kusema na yeye ataanda "kutawazwa" kwa "Rais wa Watu" ilikuwa ni kumwagilia mafuta kwenye moto wa hasira. Watu wenye sababu zao wakaona kuwa Raila lazime apewe Urais wake. Kina nani basi walimpigia kura Kibaki? BIla ya shaka Wakikuyu wenzake wengi na wale ambao bila ya shaka walinufaika na utawala wa Kibaki.

Ndipo mauaji yakaanza. Kilele cha mauaji haya ni kitendo cha kihalifu kwenye Kanisa la Pentekoste kule Eldoret ambapo watu zaidi ya 30 wa kabila la Kikuyu waliojaribu kuokoa maisha yao walipojikuta wanatiwa "kiberiti" kwa sababu ambazo wahalifu hao wanazijua. Tuliobahatika kuangalia TV unaweza kukumbuka jinsi kijana mmoja wa Kikikuyu alivyocharangwa mapanga hadi kifo akitembea mtaani kule Kibera. Matokeo yake ni kuanza kuona watu wakitembea na mabango yakitangaza "No Raila no Peace".

Raila, hakukemea hayo yote na hakujitokeza kuyakana na kutoyahusisha na kampeni yake. Jibu lake standard lilikuwa "wananchi wanatekeleza haki yao ya kidemokrasia ya maandamano ya amani". He ignored the plight of the Kikuyu people and other people who were caught in the crossfire of mapangas! He justified that by saying "the security forces are assassinating" hawa wananchi wanaotaka haki yao. Kwa maneno mengine, kama polisi wanaua wananchi kwanini na sisi tuzuie wananchi kuuawa.

Raila didnot step up to the plate and lead the nation to calm but by his mediocre actions he fanned the flame of anger and hatred.

Kuna watu wanataka tuamini kuwa Raila hakuwa na uwezo wa kutuliza passion ya watu wake. Kama vile Kibaki anavyowajibika na kitendo cha uharibu na wizi mkubwa wa kura ambao umesababisha mamia ya watu kuuawa na Raila naye anahusika moja kwa moja kwa ukimya wake katika mateso yaliyowapata watu wa Kenya. For this he is as culpable as anyone and from where I stand, he failed his nation, he failed his people.

As people demand that President Kibaki resign (and rightly so), Raila should not be given a blank check. It'll be another tragedy if the people of Kenya would overlook the actions of Raila and reward him with the presidency. He do not deserve it.

Hapa ndipo suala la maandamano ya Tanzania linapokuja. Wapinzani wa Tanzania walitaka kujitokeza kumuunga mkono Raila regardless of his actions and his inactions during this crisis. It was a wrong move and inappropriate at the time.

Kwangu mimi mauaji ya watu zaidi ya 300 yameniuma zaidi kuliko malumbano ya watu hawa wawili. The 300 or so Kenyans who died during this upheaval died unnecessarily. These were not heroes; The did not die in the quest for freedom or justice! They died because some political bigwigs in Kenya wanted to take advantage of the situation. Raila could show that Kibaki's government is responsible while Kibaki and his team could point to the situation and cry "ethnic cleansing and genocide".

Vifo vya watu hawa 300 huko Kenya still remains as the saddest part of this whole story. They did not have to die. Those children in Eldoret who thought that running ilikuwa ni kitu cha kuokoa maisha yao hakuna anayeweza kuwatabiria "ushahidi"!

Hofu yangu ya Tanzania hasa wapinzani wa Tanzania kuchukua uamuzi wa haraka wa kumtetea Raila ni kupandikiza mbegu za chuki zaidi. Leo hii kikundi cha "Mungiki" kikiwa kimejificha mahali na kuanza kupanga revenge.. Afrika ya Mashariki tujiandae. Nakumbuka vizuri Interahamwe walipanga mauaji ya kimbari kule Rwanda na jinsi walivyoamka usiku mmoja na kufanya "chinja chinja". Leo hii Mungiki wameshasambaza vikaratasi kutishia maisha ya Waluo..! Are we really ready for this?

Binafsi naamini kabisa kuwa wapinzania wangeweza kuandamana kama vile vijana wa vyuo vyetu vikuu walivyopanga kuandamana tarehe 12 (sijui kama wanajua ni siku ya Mapinduzi hiyo au wamesahau). Wao wanataka kuandamana kupinga uvunjaji wa haki za binadamu na umwagaji damu usio na sababu uliotokea Kenya. Wapinzani wangeaandaa maandamano kuishia Jangwani ambapo wangekemea uvunjwaji haki, kuikemea tume ya uchaguzi na kuwapigia kelele Kibaki na Raila na kuwataka wakae chini na kutafuta muafaka utakaowafaa watu wa Kenya.

Hata hivyo hilo lingekuwa gumu, kwani kwao Raila ni shujaa! Lakini ana ushujaa gani Raila kwenye hili? Wakati akitangaza maandamano amekuwa kama mtani wetu Seif ambaye wenzie wanaandamana yeye amejificha pembeni! Kama Raila kweli anataka kuandamana aache kuita watu wengine au yeye na viongozi wengine wawe mstari wa mbele kama walivyofanya mapema leo kina Balala kule Mombasa.

Kama Raila anataka kuonesha mfano wa kuandamana yeye awe wa kwanza kumwagiwa maji na kupigwa mabomu ya machozi, na asirudi nyuma! Asonge mbele kuelekea Uhuru Park. Kama Raila anataka kuonesha mfano asiwachombeze vijana wa Kenya ambao wanamhusudu waende na kupatwa kibano cha Polisi wakati yeye anakimbilia kwenye vyombo vya habari kuahirisha maandamano hadi "siku nyingine". Atajipatia umaarufu mkubwa na huruma kutoka kwa watu kama watamuona Raila kama Mrema kule Tanga anapigwa mabomu na kumwagiwa maji na vikosi vya Polisi akidai haki yake!

For me, siyo Raila wala Kibaki wanaostahili kukalia kiti cha Ikulu ya Kenya kwani wote wana damu mikononi mwao! Damu ambayo inalia na kuita Kenya, iponywe!
 
Hii post ipo kule na Mtanzania amejibu vizuri sana.

Lengo la maandamano wanapanga hao wanaandamana, hawawezi kupangiwa na mtu mwingine. Isitoshe lengo kubwa la maandamano ni kutoa dukuduku walilonalo waandamanaji wala sio lazima yabadilishe maamuzi au yaathiri power ya hao walizo nazo. Sioni kwa nini hawa ndugu walaaniwe kutaka kuandamana kwa ajili ya kutoa dukuduku lao juu ya Odinga kunyang'anywa ushindi. Duniani huwezi kumfurahisha au kumchukiza kila mtu. Poleni sana waliochukizwa na maandamano haya ambayo hata hivyo hayakufanyika.
 
Arguments za Mwanakijiji zimeniingia barabara. Kama alivyosema Askofu Tutu alipoulizwa kuhusu Mbeki na Zuma, wote hawafai. Vilevile kwenye hili. Wote wawili, Kibaki na Raila wameonyesha udhaifu mkubwa na damu ya waliouawa katika hizi siku za hivi karibuni hawawezi kuikwepa. Wote wawili. Lakini kwenye hili la kuandamana nyumbani natofautiana nae kidogo. Nyumbani tuna tatizo la kupenda ku'micromanage' kila kitu. Tabia hii inatuingiza katika matatizo yasiyo na haja. Kama chama cha upinzani kwa sababu zake kinataka kuandaa maandamano kumuunga mkono mmoja wa waliogombea huko kwa jirani zetu angeachiwa afanye hivyo. Misguided pengine, lakini ni haki yake. Siamini kuwa ati kwa sababu wameunga mkono mjaluo basi wajaluo watazidisha munkari wa kuwanyonga wakikuyu and viceversa. Badala yakenadhani kwa kufanya hivi kungeisukumiza serikali ambayo ndiyo inasikilizwa zaidi kutoa tamko kuhusu hali ya kwa hao wenzetu. Tungewaacha waandamane na wakuu kama nyinyi mngelaani kitendo chao kwa sauti kubwa mnavyoweza. Kwa kufanya hivi ingewaonyesha jirani zetu jinsi tunavyopaswa kuishi. Kuvumiliana hata pale tunapotofautiana kimawazo. Sio kuchinjana. Ndiyo demokrasi. Kukaa kimya hakusaidii kitu.
 
MKJJ, Na wengine anti maandamano.... nakereketwa. ........Nakereka, nakereka, nakereka jinsi watanzania wakati mwingine tulivyo na nidhamu ya woga....nakereka, nakereka

Nakubaliana nawe hapo, Ila hata mimi nakereka kwani hivi vyama vya upinzani vina mengi sana ya kuandamana ambayo yanahusu watanzania na wazawa, wao wanafanya nini?? Wanakalia tu ushambenga wa huko kenya!, kwanza wao kama tulivyosema mwanzo walitakiwa waandamane kuhusu mauaji na siyo Kibaki kumwibia Raila kura, kwani wao wana ushahidi gani?!

Kama wamekuwa wapenda haki hivyo walikuwa wapi wakati Zanzibar watu wanauwawa mchana mzima, na wizi wa kura kila mtu aliuona mbona hawakuandamana? mauaji ya mwembechai walikuwa wapi? Kila siku mabasi yanapinduka na kuua wata nchini mbona hawafanyi maandamano ya kuiuliza serikali? Je umesikia hii ishu ya Watanzania weusi kulipwa mshahara mdogo kuliko wengine je hao wa vyama vya upinzani wametoa tamko gani?
 
Hivi kwa nini Raila analaumiwa wakati yeye ndio mdhulumiwa? Nashindwa kuelewa kabisa. Mwaka 2002 Kibaki alishinda na walioshindwa wakakubali na hakukuwa na vurugu zozote. Sasa yeye kashindwa halafu akaiba halafu analaumiwa aliyeibiwa....!!!! Makes no sense at all. Don't start no shit there won't be no shit.
 
kweli sielewi kabisa kwanini alumiwe Odinga kwa wizi uliofanywa na kina kibaki,na why mnamhukumu odinga eti damu iko mikononi mwake....waafrika ndio maana hatutacha kupigana na kuwa maskini,issue iko straight lakini kina mwanakijiji na mzalendo watakuja na spin zao mpaka unashangaa why why why why,Kibaki must go ni mwizi na alishindwa uchaguzi
 
Raila analaumiwa kwa kufumbia macho mauaji ya wakikuyu..!!

Mkuu, apo hivi waliouwawa ni wakikuyu tu au na makabila mengine? Ina maana hata hao waliouwawa na polisi ni wakikuyu peke yao>? au wakikuyu wana alama usoni? najua kuwa wao ni target kwa sababu mkikuyu mwenzao amefanya rigging ya kufungia karne, lakini inaniwia vigumu kuamini kama haya mauaji yamewaathiri wakikuyu tu?
 
Wale wanaomtete kibaki na kusema Raila ni muuaji tunaomba figure wakikuyu wangapi wamekufa/wameuwawa pamoja na makabila mengine. Tufanye comparison
 
Quote:-

"For me, siyo Raila wala Kibaki wanaostahili kukalia kiti cha Ikulu ya Kenya kwani wote wana damu mikononi mwao! Damu ambayo inalia na kuita Kenya, iponywe!"


Hapa mkuu tunaongea lugha moja,

However, huyu Tutu hana credibility kabisaa zaidi ya hiyo Nobel thing ambayo hata Carter alipewa, huyu nasikia ndiye chanzo cha Mandela kuachana na mkewe Winnie, nasikia amegeuka kuwa agent wa makaburu ambao ndio hasa wasiomtak Zuma, hivi exactly ni nani aliyemtuma huko Kenya, au ni kihere here tu!
 
Wale wanaomtete kibaki na kusema Raila ni muuaji tunaomba figure wakikuyu wangapi wamekufa/wameuwawa pamoja na makabila mengine. Tufanye comparison

Bowbow.. angalia kama kuna mtu amemtetea Kibaki kwani mtu mwenye akili za kumtetea Kibaki basi akili zake hazina akili.. !
 
Mkuu, apo hivi waliouwawa ni wakikuyu tu au na makabila mengine? Ina maana hata hao waliouwawa na polisi ni wakikuyu peke yao>? au wakikuyu wana alama usoni? najua kuwa wao ni target kwa sababu mkikuyu mwenzao amefanya rigging ya kufungia karne, lakini inaniwia vigumu kuamini kama haya mauaji yamewaathiri wakikuyu tu?

that is exactly my point.. kuna watu ambao hawajaguswa na mauaji ya Kenya kwao wanacholalamikia ni kura kuibiwa tu na yale mauaji ambayo yanaendelea wameyafumbia macho au wanayatafutia udhuru.. ! Mauaji haya yamewaathiri watu wengi na bila ya shaka wakikuyu yamewapata zaidi kwa sababu uliyoisome "kwa sababu mkikuyu mwenzao amefanya rigging ya kufungia karne,"..

Kuna watu (Raila mmoja wao) ambao Wakikuyu kuuawa hakiwasumbui kichwa kwa sababu "mkikuyu mwenzao" ndiye aliyeiba kura.. kwa maneno mengine jamii nzima ya wakikuyu inatiwa hatiani kwa makosa ya mtu mmoja! NI sawa sawa na yule mtu aliyekuja na kusema "aliibiwa ng'ombe na wamasai"!
 
Jitu la kulaumiwa hapa ni Li-Kibaki lijizi. Lisingeiba wala kusingekuwepo na haya mauaji. Yaani halina hata aibu. Limetangazwa lishindi na ktk saa moja likakimbilia kuapishwa. Sijui kwa nini halikusubiri wala kufuata utaratibu uliopo. I HATE THAT MOFUCKA WITH A PASSION
 
duh.. siku nyingi sijawahi kuona mtu anatumia "li" kwa nguvu kiasi hicho.. maana ni passion for real.. are you sure that date haikuenda kombo...?
 
Wale wanaomtete kibaki na kusema Raila ni muuaji tunaomba figure wakikuyu wangapi wamekufa/wameuwawa pamoja na makabila mengine. Tufanye comparison

Oops, nimemiss sehemu ya pili.. sijui ni nani amesema Raila Muuaji.. help me out.. halafu tufanye comparison kuona watu wangapi wa kabila gani wamekufa na kama idadi inalingana..?
 
duh.. siku nyingi sijawahi kuona mtu anatumia "li" kwa nguvu kiasi hicho.. maana ni passion for real.. are you sure that date haikuenda kombo...?

How about this..."Li-Mwanakijiji"...?

About the date...let me tell you....that bi#@$ stood me up and never showed up. Tried calling her...but it went straight to voicemail...so I ended up going home and watch the Piston get their asses handed to them by the Celtics....
 
nasikia police dar wamezuia maandamano ya wapinzani,is that necessary? yaani ni upuuzi mtupu na hawa wakoloni weusi,mambo gani hayo ya kuzuia watu just kwa sababu wewe una jeshi,pumbavu sana hawa ng'ombe!
 
Back
Top Bottom