'Mkutano wa demokrasia' wa Marekani wakosolewa Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
gfhfhf.jpg


Wiki hii, kile kinachoitwa "Mkutano wa tatu wa Demokrasia" unaoongozwa na serikali ya Marekani ulifanyika huku kukiwa na utata mwingi. Gazeti la "The Standard" la Kenya lilitoa tahariri yenye kichwa cha "‘Mkutano wa Demokrasia’ waonyesha kiburi cha Marekani,” likisema kwamba Marekani inachukulia demokrasia kama silaha, hatua ambayo sio tu inakwenda kinyume na maana ya demokrasia, lakini pia inadhoofisha maadali inayotetea mara kwa mara.



Katika miaka ya hivi karibuni, dunia nzima imepunguza imani na demokrasia ya Marekani, na hata watu wengi wanaiona Marekani kama tishio kubwa kwa demokrasia. Ili kujenga upya sura ya kimataifa ya Marekani ambayo iliharibiwa na mtangulizi wake, serikali inayoongozwa na rais wa sasa wa nchi hiyo Joe Biden ilifanya “Mkutano wa kwanza wa Demokrasia” mwaka 2021. Hata hivyo, katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, ushawishi wa mkutano huo umeendelea kushuka. Sababu ni rahisi kuelewa. Katika masuala mengi, Biden kimsingi ameendeleza sera za mtangulizi wake na hajatekeleza mabadiliko makubwa. Kwa mfano, serikali ya Marekani inaendelea kutekeleza sera ya "ushindani mkubwa kati ya nchi kubwa" barani Afrika, na kuzilazimisha nchi za Afrika "kuchagua upande" na kupuuza kabisa mahitaji na shida za ndani za nchi hizo. Kama baadhi ya viongozi wa kisiasa wa Afrika, wataalam na wasomi wanavyoamini, serikali ya Marekani haijawahi kuiona Afrika kama mshirika, wala haijali ustawi wa watu wa Afrika, na kutokana na hilo, ni wazi kuwa Mkutano wa "Demokrasia" ulioanzishwa na nchi hiyo hakika utashindwa.

Wakati huo huo, Marekani inatumia demokrasia kama kisingizio cha kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine, na hata kujaribu kupindua serikali halali, ambayo ni sababu nyingine inayoathiri ushawishi wake wa demokrasia barani Afrika. Kihistoria, Marekani imefanya uingiliaji wa kisiasa katika nchi nyingi za Afrika, ambao sio tu ulidhoofisha utulivu wa kisiasa wa nchi hizo, lakini pia ulidhuru maslahi ya watu, na kupelekea nchi za Afrika na watu wa kawaida kutilia mashaka na kutoamini maadili ya demokrasia ya Marekani. Takwimu zinaonyesha kuwa kutokana na vikwazo vya muda mrefu vya Marekani, Sudan imekumbwa na janga kubwa la kibinadamu kote nchini, na 38% ya watoto wamekufa kutokana na utapiamlo. Katika miaka 20 iliyopita, vikwazo vilivyowekwa na Marekani na nchi za Magharibi dhidi ya Zimbabwe vimesababisha nchi hiyo kupata hasara ya kiuchumi ya zaidi ya dola bilioni 40 za Marekani. "Demokrasia" imekuwa "silaha ya maangamizi makubwa" mikononi mwa Marekani, inayotumiwa kudhibiti nchi nyingine na kudumisha utawala wake.

Hakuna demokrasia iliyo bora kabisa duniani, na hakuna mtindo mmoja wa demokrasia unaofaa nchi zote. Hali halisi ni kuwa nchi nyingi za Afrika zilitumia mitindo ya kidemokrasia ya Magharibi katika siku za mwanzo za uhuru. Hata hivyo, kwa zaidi ya nusu karne, njia hii ya kidemokrasia imekumbana na changamoto mara kwa mara barani Afrika. Moja ya dalili muhimu ni mapinduzi ya mara kwa mara na ukosefu wa utulivu wa kisiasa katika baadhi ya nchi. Takwimu zinaonyesha kuwa kuanzia 1950 hadi 2021, kulikuwa na zaidi ya mapinduzi 200 barani Afrika, na wastani wa karibu 3 kwa mwaka. Tatizo ni kwamba hii ni demokrasia iliyowekwa kwa Afrika na nchi za Magharibi, badala ya chaguo huru la watu wa Afrika.

Je, kama kuna hitaji kwamba nchi mbalimbali kubadilishana na kufunzana kuhusu uzoefu wa kujenga siasa za kidemokrasia? Bila shaka ipo, lakini ikiwa Marekani itajaribu kugawanya dunia katika kambi mbalimbali kwa jina la demokrasia, maana halisi ya demokrasia itakuwa mbali zaidi na zaidi kutoka kwake. Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na maendeleo ya uchumi na kuongezeka kwa mwamko wa uhuru katika nchi za Kusini, nchi nyingi zaidi za Afrika zinatambua kwamba watu wa Afrika wana haki ya kutafuta njia yao ya maendeleo na kuacha kutegemea sana nchi za Magharibi.
 
US inataka kulazimisha dunia nzima ifuate model yake ya siasa na uongozi. Kitu ambacho sio sahihi. Uarabu, sababu ya tamaduni na tabia zao, kupeleka demokrasia ni kujitakia kuungua na moto.
Hata sisi pia, tuwe na namna bora ya kuwezesha mambo yetu kufanyika
 
Back
Top Bottom