Maana ya maneno niliyoambiwa Mzee Afande

Gily Gru

JF-Expert Member
Jul 4, 2016
7,802
20,762
Kuna kipindi wakati niko Rombo nakumbuka nilienda kumuoji mzee mmoja anaitwa mzee Afande kuhusu maswala ya zamani. Yule mzee alinambia kuwa kat ka maisha yake amemwona babu yangu (nami namfahamu), baba yake babu yangu (alifariki 1983 simfahamu) na babu yake baba yake babu yangu (simfahamu). Na alidokozea kuwa wakati baba yake babu yangu alikuwa mdogo sana kwake. Niliongea sana na yule mzee mwishoni nikamnunulia bia mbili za safari nikamuaga niende zangu. .

Huyu mzee Afande alifariki mwaka jana japo umri wake ulikuwa kipengele wengine walidai alikuwa na miaka 120 mpaka 140.Kama mnavyojua mengi husewa na kila mtu husema lake. Ila vitukuu vyake huyu mzee mkubwa ana miaka 40+. Najua kuna watu watabisha ila mkoa wa Kilimanjaro una wazee wenye miaka mingi mno inatakiwa watu walichunguze hili swala.

Kuna wazee kibao ambao nawafahamu wamekufa wakiwa na miaka 100+. Mfano bibi yangu mke mdogo narudia mke mdogo wa babu wa BABA yangu ambaye mimi ni kitukuu wake alifariki akiwa na miaka 119. Ushahidi wa umri wake ulipatiakana mission (kwa wanavyotamka wachaga misheni) kwenye nyaraka za kanisa. Watoto wakizaliwa kipindi hicho walikuwa wanaenda kuwaandikisha mission. .

Kilichofanya niandike huu uzi ni kuwa mzee Afande aliniomba nikamletee ngozi ya mnyama wa mwituni. Kwa uoga wangu sikwenda kwa sababu nilipata wasiwasi usikute huyu mzee anataka kuchukua umri wangu kichawi.

Kilichonifanya niogope ni kwa sababu baba yake mzee Afande alikuwa ana tabia ya kutondokea (neno la kichaga) nikimaanisha anavua nguo zote anazama ardhini kichawi anakaa hata juma moja anarudi. Wanadai wenyewe kuwa anaenda kuzungumza na mizimu huko chini (Kuhusu story za kutondokea nitazileta siku nyingine ni habari ndefu na ni swala la kweli kabisa linatokea). .

Jana kuna mzee mwingine kaniambia maneno haya haya nimletee ngozi ya mnyama wa mwituni. Huyu mzee wala si mzee kivile ana miaka 70+ na hata hana uchawi wowote ni mzee wa kawaida. Nikawaza labda hili neno halina maana mbaya ni maneno tu ya zamani labda kuna kitu yanamaanisha. Sasa ndugu zangu najua JF ni kisima cha maarifa kama kuna mtu anajua maana ya haya maneno anielekeze. .
 
Yule mzee wa kwanza alinambia “nenda kaniletee ngozi ya mnyama wa mwituni”

Nikamuliza cha kazi gani babu?

Akanijibu “wewe nenda kaniletee ukileta nitakwambia”
 
Hizo habari nimewahi kuzisikia sana kuhusu watu ambao walikuwa na uwezo huo,Ni miaka ya zamani sana Ila inasemekana mtu anapopotea hivyo haenddi na nguo na wakirudi wanakuja na taatifa mbalimbali zinazohusu maisha haya,Ni watu ambao walikuwa na uwezo wa kutabiri matukio mbali mbali na inasemekana hawakuwa watu wenye dhambi sana.Miaka hii sidhani Kama Kuna watu wa Aina hiyo Ila all in all Mimi ninaona Kama Ni ushirikina,ukitaka detailed history ninayo ,nafahamu chimbuko la jamii nzima.
 
Hizo habari nimewahi kuzisikia sana kuhusu watu ambao walikuwa na uwezo huo,Ni miaka ya zamani sana Ila inasemekana mtu anapopotea hivyo haenddi na nguo na wakirudi wanakuja na taatifa mbalimbali zinazohusu maisha haya,Ni watu ambao walikuwa na uwezo wa kutabiri matukio mbali mbali na inasemekana hawakuwa watu wenye dhambi sana.Miaka hii sidhani Kama Kuna watu wa Aina hiyo Ila all in all Mimi ninaona Kama Ni ushirikina,ukitaka detailed history ninayo ,nafahamu chimbuko la jamii nzima.
Watu wa kutondokea walikuwapo katika kila jamii na sana sana walikuwa wanaenda kuzungumza na watu waliokufa wa kipindi hicho waliokuwa kwenye eneo hilo. Hata mimi nina mifano mingi kupitia hili swala nakumbuka niliandika hzi habari somewhere mpaka nitafute ni mda kidogo. Babu yangu alinisimulia kuwa ilikuwa ni marufuku kuokota nguo ambazo umezikuta tu ziko sehemu. Ilikuwa inamlazimu avue nguonzote aende huko sasa sijui ni kuzimu? maana kuzimu si ndio kuna mizimu!
 
Situmii kilevi cha aina yeyote labda kahawa na sijanywa kahawa siku mbili zilizopita
Acha masikhara wakati niko serious Lucha
Hayo maneno ya kukutuma ngozi ya mnyama maana yake ni "uache kutumia kilevi" siyo kufata ngozi
 
Hayo maneno ya kukutuma ngozi ya mnyama maana yake ni "uache kutumia kilevi" siyo kufata ngozi
Ndio maana yake? Mie kilevi situmii imenishangaza kwa nini aniambie niache kutumia kilevi. Huyu mzee wa pili alinambia hivyo hivyo na anajua situmii kilevi. .
 
Uchawi Kama kawaida... Usishiriki lolote. Kaa mbali na Mambo usiyoweza kuyatafsiri Wala kuyaelewa.
Hili swala nililiwaza ila nikalipotezea, sasa huyu mzee wa pili alivyoniambia haya maneno pia nikaona niulize. .
 
Hayo maneno Mara nyingi utaambiwa Kama Ni pointi ya kukupima Kama Ni mtu jasiri na mwerevu,wazee Mara nyingi hawawezi kueleza Mambo yao nyeti kwa kila mtu,Kama unaweza kupata ngozi ya mnyama wa mwituni tafsiri yake wewe Ni mtu jasiri na mwerevu na mwenye uwezo wa kutunza Siri ,hukuambiwa literally ukalete ngozi kweli ,walikuwa wanakupima Kama una ubongo unaoweza kuchakata Mambo barabara.
 
Hayo maneno Mara nyingi utaambiwa Kama Ni pointi ya kukupima Kama Ni mtu jasiri na mwerevu,wazee Mara nyingi hawawezi kueleza Mambo yao nyeti kwa kila mtu,Kama unaweza kupata ngozi ya mnyama wa mwituni tafsiri yake wewe Ni mtu jasiri na mwerevu na mwenye uwezo wa kutunza Siri ,hukuambiwa literally ukalete ngozi kweli ,walikuwa wanakupima Kama una ubongo unaoweza kuchakata Mambo barabara.
Sasa ningeenda kumletea ngozi ndio angenipa maana yake, sikwenda kwa wasiwasi. .
 
Kuna kipindi wakati niko Rombo nakumbuka nilienda kumuoji mzee mmoja anaitwa mzee Afande kuhusu maswala ya zamani. Yule mzee alinambia kuwa kat ka maisha yake amemwona babu yangu (nami namfahamu), baba yake babu yangu (alifariki 1983 simfahamu) na babu yake baba yake babu yangu (simfahamu). Na alidokozea kuwa wakati baba yake babu yangu alikuwa mdogo sana kwake. Niliongea sana na yule mzee mwishoni nikamnunulia bia mbili za safari nikamuaga niende zangu. .

Huyu mzee Afande alifariki mwaka jana japo umri wake ulikuwa kipengele wengine walidai alikuwa na miaka 120 mpaka 140.Kama mnavyojua mengi husewa na kila mtu husema lake. Ila vitukuu vyake huyu mzee mkubwa ana miaka 40+. Najua kuna watu watabisha ila mkoa wa Kilimanjaro una wazee wenye miaka mingi mno inatakiwa watu walichunguze hili swala.

Kuna wazee kibao ambao nawafahamu wamekufa wakiwa na miaka 100+. Mfano bibi yangu mke mdogo narudia mke mdogo wa babu wa BABA yangu ambaye mimi ni kitukuu wake alifariki akiwa na miaka 119. Ushahidi wa umri wake ulipatiakana mission (kwa wanavyotamka wachaga misheni) kwenye nyaraka za kanisa. Watoto wakizaliwa kipindi hicho walikuwa wanaenda kuwaandikisha mission. .

Kilichofanya niandike huu uzi ni kuwa mzee Afande aliniomba nikamletee ngozi ya mnyama wa mwituni. Kwa uoga wangu sikwenda kwa sababu nilipata wasiwasi usikute huyu mzee anataka kuchukua umri wangu kichawi.

Kilichonifanya niogope ni kwa sababu baba yake mzee Afande alikuwa ana tabia ya kutondokea (neno la kichaga) nikimaanisha anavua nguo zote anazama ardhini kichawi anakaa hata juma moja anarudi. Wanadai wenyewe kuwa anaenda kuzungumza na mizimu huko chini (Kuhusu story za kutondokea nitazileta siku nyingine ni habari ndefu na ni swala la kweli kabisa linatokea). .

Jana kuna mzee mwingine kaniambia maneno haya haya nimletee ngozi ya mnyama wa mwituni. Huyu mzee wala si mzee kivile ana miaka 70+ na hata hana uchawi wowote ni mzee wa kawaida. Nikawaza labda hili neno halina maana mbaya ni maneno tu ya zamani labda kuna kitu yanamaanisha. Sasa ndugu zangu najua JF ni kisima cha maarifa kama kuna mtu anajua maana ya haya maneno anielekeze. .
Inasisimua sana hii hoja yako. Lakini inazizimua akili kutaka kufahamu kulikoni hayo yanajiri.

Ninapenda kukushauri kuwa, kupata maana ya hitaji la ngozi ya mnyama wa mwituni inapatikana kwenye maelezo ya ziada ya wahitaji.

Nakushauri, ongea na huyo mzee akipe sababu ya hitaji hilo. Hapo haujavunja mwiko wala hautakuwa umemkosea heshima
 
Inasisimua sana hii hoja yako. Lakini inazizimua akili kutaka kufahamu kulikoni hayo yanajiri.

Ninapenda kukushauri kuwa, kupata maana ya hitaji la ngozi ya mnyama wa mwituni inapatikana kwenye maelezo ya ziada ya wahitaji.

Nakushauri, ongea na huyo mzee akipe sababu ya hitaji hilo. Hapo haujavunja mwiko wala hautakuwa umemkosea heshima
Labda nimtafute huyu mzee wa pili anifafanulie maana yake. Mzee Afande alifariki mwaka jana kwa hiyo haitawezekana kujua alimanisha nini
Ila cha kushangaza wamekuja watu wawili hapa wameleta maana tofauti. Ngoja tuone majibu watu watakuwa nayo tu. .
 
Back
Top Bottom