Maalim Seif awaponza viongozi wa Jeshi la Polisi Pemba, yaamriwa wavuliwe vyeo

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,670
218,173
Naibu Waziri wa mambo ya ndani Hamad Masauni amemwagiza IGP Sirro kuwavua vyeo RPC wa Kusini pemba Hassan Nasir Ally na RPC wa Kaskazini Pemba Shekhan Mohamed kwa kosa la kumwacha Jabali Maalim Seif kuhutubia wananchi wa Pemba , huku siasa za majukwaani zikiwa zimekatazwa
---
mm.png

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, Hamad Masauni amemuagiza Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro kuwaondoa makamanda wawili wa polisi kisiwani Pemba kwa kushindwa kuzuia mikutano ya Mshauri wa chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad.

Masauni ametoa agizo hilo leo Alhamisi Desemba 12, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Unguja.

Amesema kwa muda mrefu kisiwa cha Pemba kimekuwa na matukio yasioridhisha jambo linaloashiria kuwa wameshindwa kazi.

Makamanda hao ni Hassan Nassir Ally wa Mkoa wa Kusini Pemba na Sheikhan Mohamed Sheikhan wa Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Akitoa mfano wa matukio hayo, Masauni amesema Maalim Seif anafanya mikutano kila kona huku ikijulikana kuwa imezuiwa.

Amesema sababu nyingine ni kutojengwa nyumba za polisi kisiwani humo licha ya Serikali kutoa maagizo.
 
Kwahiyo Marpc sasa ni dhahiri wana fanya kazi kwa maagizo ya chama cha mapinduzi.. Huu ni ulevi wa madafaka
Naibu Waziri wa mambo ya ndani Hamad Masauni amemwagiza IGP Sirro kuwavua vyeo RPC wa Kusini pemba Hassan Nasir Ally na RPC wa Kaskazini Pemba Shekhan Mohamed kwa kosa la kumwacha Jabali Maalim Seif kuhutubia wananchi wa Pemba , huku siasa za majukwaani zikiwa zimekatazwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania, Hamad Masauni amemuagiza Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro kuwaondoa makamanda wawili wa polisi kisiwani Pemba kwa kushindwa kuzuia mikutano ya Mshauri wa chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad.

Masauni ametoa agizo hilo leo Alhamisi Desemba 12, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Unguja.

Amesema kwa muda mrefu kisiwa cha Pemba kimekuwa na matukio yasioridhisha jambo linaloashiria kuwa wameshindwa kazi.

Makamanda hao ni Hassan Nassir Ally wa Mkoa wa Kusini Pemba na Sheikhan Mohamed Sheikhan wa Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Akitoa mfano wa matukio hayo, Masauni amesema Maalim Seif anafanya mikutano kila kona huku ikijulikana kuwa imezuiwa.

Amesema sababu nyingine ni kutojengwa nyumba za polisi kisiwani humo licha ya Serikali kutoa maagizo.

3E8D183D-6D88-4589-A774-82EB8E75239A.jpeg

798A2798-5BCE-4645-BBB6-D68620743D70.jpeg
 
Huyu Maalim seif ubabe wake umesababisha watu wafukuzwe kazi


Huyu Mzee akamatwe akahojiwe sasa
 
Yule Dk Kigeugeu alipokuwa anafanya mikutano na masweta yake ya migomba hakuwa anafanya siasa? Hawa wanaishi kwa vitisho na mwisho wa kila mmoja umewadia.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndio maana tunasema ccm kwa sasa inategemea nguvu ya dola tu kufanya siasa. Na hii ndio inayopelekea jeshi la polisi kuvunja sheria kwa kuwakandamiza wapinzani ili kulinda vyeo.
 
Huyu Maalim seif ubabe wake umesababisha watu wafukuzwe kazi


Huyu Mzee akamatwe akahojiwe sasa

Huo ni udhibitisho kuwa nguvu pekee ya ccm ni matumizi ya vyombo vya dola. Hizo hofu anazopandikiza huyo waziri, ndio huwafanya viongozi wengine wa jeshi la polisi kutii lolote wanaloogizwa dhidi ya haki za wapinzani, na wengine huenda mbali mpaka kufanya mauaji au kuleta vilema ili kulinda vyeo. Hivyo vyombo vya dola ndio pekee vinavyoendelea kulinda uwepo wa ccm hapa nchini.
 
Back
Top Bottom