Maajabu ya daraja la Kigamboni!

Maajabu ya daraja la Kigamboni!

Kama ilivyozoeleka ..hao Wadachi wakitoa Grant basi hapo hakuna ulaji wa maana kwa makampuni Watz na wale wa 10% Miundombinu! Mtu yuko tayari kuliko asipate hapo kitu basi na daraja lisijengwe!

Kwa kifupi ni kukosa tu uzalendo na kuweka kwanza maslahi binafsi mbele!

Maana sasa miaka zaidi ya 15 kweli Tz tunashindwa kufikia maamuzi jambo dogo hivi.. je makubwa tutaweza?
 
Kama ilivyozoeleka ..hao Wadachi wakitoa Grant basi hapo hakuna ulaji wa maana kwa Watz!

Kwa kifupi ni kukosa tu uzalendo na kuweka kwanza maslahi binafsi mbele!

Maana sasa miaka zaidi ya 15 kweli Tz tunashindwa kufikia maamuzi jambo dogo hivi.. je makubwa tutaweza?


Ni kweli utata upo kwenye hiyo grant na sharti la mjenzi awe mdachi it goes without saying hakuna mlo!
 
Kama kuna ukweli sasa si bora mkoloni tuu....huu ni ulafi wa aina gani? kwanza nina uhakika wadachi watajenga vizuri kuliko hivyo vikampuni vyao vya 10%,mtaje jina huyo waziri/kigogo tufe naye hapa na wataeleza ukweli makombora yakifumuka kama kina balali na Lowassa...mwaga nyeti baba tunatetea daraja letu sio hao mafisadi,media is so powerful na ndio iliyomwangusha Lowassa kama hamjui
 
Tanzania kuna makorokoro mengi sana.
Na huku tena?
 
Nasikia kuna mpango wa kuleta mtaalamu wa kushauri umuhimu wa kujenga daraja la Kigamboni badala ya kuendelea kutegemea mitumbwi na pantoni!
 
Kwa mara ya mwisho nilipofuatia swala la daraja hili niliambiwa kuwa serikali ilikuwa imekwisha amua litajengwa Kurasini badala ya pale Kigamboni kutokana na kwamba pale Kivukoni hakuna nafasi ya kutosha kuweza kupandisha mwinuko wa daraja.
Majuzi tu nilipata habari kuwa ujenzi huo wa Kurasini umesimamishwa baada ya kuzingatiwa kuwa daraja lilitakiwa zaidi lijengwe maeneo ya mjini pale Kivukoni na sio Kurasini kutokana na sababu nyingi za kimsingi.
Bila shaka yawezekana ikawa hii ndio sababu kubwa ya usitishaji wa mpango wa ujenzi wa daraja la Kurasini kwani kama kuna mabadiliko ya kurudisha offer ama mchoro uwe wa Kivukoni badala ya Kurasini na gharama zake. Mtakumbuka kuwa niliwahi sema kuwa daraja linaweza jengwa kabisa kwa kuitumia barabara ya Ocean road kupata mwinuko na nguzo kuu za daraja.
Binafsi sioni sababu kabisa ya kuweka kivuko cha daraja Kurasini, tutakuwa hatujatatua kabisa tatizo la usafiri na nina hakika bado wananchi wataendelea kutua usafiri wa maji (Panton) kuliko kwenda hadi Kurasini.
 
viongozi Wetu Tz Wamekosa Ujasiri Wa Kutetea Maendeleo Ya Tanzania, Wanaangalia Matumbo Yao...
......ila Mjue Mnakula Moto Ktk Matumbo Yenu, Mnachokula Ni Sawa Kula Nyama Ya Mwanadamu Aliekufa!!!

salam Kwa Viongozi....mshakula Sana....hamna Hata Cha Kupendeza Ktk Macho Ya Watanzania....basi Hata Daraja? Ambalo Nanyi Mtapita?
 
Mkulu GT,

Ni kweli kuna kiwingu kikubwa kimetanda katika sakata zima la ujenzi wa daraja la Kigamboni.

Last time I checked serikali ya Holland wamekubali kutoa grant ya 50% ya cost ya daraja lote. For reasons best known to themselves, wizara ya Miundo Mbinu pamoja na wizara ya Fedha wamekuwa wakikwamisha kwa makusudi juhudi za ujenzi, inasemekana wizara ya Miundo Mbinu wapo radhi daraja lijengwe na watu wengine (mbali na wadachi) na serikali igharamie in FULL.

Sasa swali ikiwa kuna 50% grant yes GRANT sio LOAN ( condition ni kuwa kampuni za kidachi tu ndio zishindanie tenda)ni vipi watu wanang'ang'ania serikali igharamie in FULL?

Watapata wapi Ulaji wakiruhusu daraja lijengwe kizembe(na watu makini) mabingwa wa kucheza na maji ya bahari???
 
Kwa mara ya mwisho nilipofuatia swala la daraja hili niliambiwa kuwa serikali ilikuwa imekwisha amua litajengwa Kurasini badala ya pale Kigamboni kutokana na kwamba pale Kivukoni hakuna nafasi ya kutosha kuweza kupandisha mwinuko wa daraja.
Majuzi tu nilipata habari kuwa ujenzi huo wa Kurasini umesimamishwa baada ya kuzingatiwa kuwa daraja lilitakiwa zaidi lijengwe maeneo ya mjini pale Kivukoni na sio Kurasini kutokana na sababu nyingi za kimsingi.
Bila shaka yawezekana ikawa hii ndio sababu kubwa ya usitishaji wa mpango wa ujenzi wa daraja la Kurasini kwani kama kuna mabadiliko ya kurudisha offer ama mchoro uwe wa Kivukoni badala ya Kurasini na gharama zake. Mtakumbuka kuwa niliwahi sema kuwa daraja linaweza jengwa kabisa kwa kuitumia barabara ya Ocean road kupata mwinuko na nguzo kuu za daraja.
Binafsi sioni sababu kabisa ya kuweka kivuko cha daraja Kurasini, tutakuwa hatujatatua kabisa tatizo la usafiri na nina hakika bado wananchi wataendelea kutua usafiri wa maji (Panton) kuliko kwenda hadi Kurasini.

Mkandara mtazamo wako si sahihi sana...Kigamboni inakuwa sasa. in next 10 yrs kigamboni pekee yake huenda ikawa population kubwa sana ya watu. so huenda tukahitaji madaraja mengi tu. Serikali imepima viwanja vingi sana na bado zoezi laendelea...

Pia ukumbuke baadhi ya watu hadi sasa wanatokea Kigamboni thru njia ya Mbagala. Maana Kivuko cha sasa kigamboni unaweza kukaa masaa mengi tu.
Kimsingi kujengwa kwa kivuko cha Kigamboni kusudio lake Haswa ni magari, watembea kwa mguu bado wanaweza kuwa na Option Kuendelea kukitumia kivuko cha sasa.[so far watembea kwa mguu hawaathiriki sana]

Wenzetu Dubai wana madaraja 5, moja underground na moja ni FLOATING BRIGDE. Na Bado wanavivuko vya watembea kwa Mguu zaidi ya 40 (kila kimoja kinabeba watu 20), na bado wanataka kuweka WATER BUS...(sikwambii Singapore, Hongkong na kwingineko)

Hivyo on my side...kivuko popote kitakapokuwa [kigamboni ya sasa au Kurasini]kipunguza kero iliyopo sasa. next 10-20 yrs bado tunaweza jenga kingine kutegemea na fursa na wasaa uliopo.
 
Mkoloni aliyetoka maili maelfu huko batra la Ulaya haukuipenda nchi yetu lakini alijenga reli na hata Ikulu ambayo Mafisadi wanaitumia hadi leo hii.

Mmachinga au Mkwere aliye lelewa kwa kula mboga ya mchunga wa kuungwa chumvi tu leo hayuko tayari kusimama kidete kuhakikisha daraja la kigamboni linajengwa mahali ambapo ni chini ya maili 50 kutoka kijiji alicho zaliwa.

Mkoloni angekuwa na mawazo kama Viongozi wetu angejenga Reli ya kati au Ikulu??

Mwe!
 
Chuma,
Mkuu nakubaliana na wewe ikiwa unazungumzia upanuzi wa usafiri. Hili ni daraja la ngama ambalo tunalihitaji leo hii hivyo ni muhimu liwe sehemu ambayo ni muhimu zaidi kisha ktk upanuzi zaidi na jinsi population inavyozidi basi tutaweza jenga mengine.
Najua fika kuwa wapo watu wanaovuka kupitia Mbagala lakini safari ni ndefu sana ni wangapi watakuwa wakitokea mjini kama litakuwepo daraja hapo kivukoni?..Daraja hapo litaondoa traffic kubwa na nafuu kwa wakazi wa Mtoni na Temeke. Lakini likijengwa huko mkuu wangu itakuwa hatari kubwa usafiri wa njia hiyo kutokana na population ya huko hasa Mahotel na kadhalika.
Yes, linatakiwa daraja la magari na ndivyo dunia nzima hu plan madaraja ama mabarabara kwa sababu ya magari na sio waenda kwa mguu unless tunazungumzia Pavements.. Haa haaa haa!
Tanzania ya kesho inatakiwa ifikirie matumizi zaidi ya magari kuliko mwendo wa mguu, kisha basi mabus na daladala ndio usafiri wenyewe hakuna haja ya watu kutembea kwa miguu kukatiza.
Kweli mkuu tunahitaji daraja eneo hilo la mjini kwanza mwngine yatafuata kadri wakati unavyokwenda lakini sio kuliweka Kurasini kuzidisha traffic zaidi Kilwa road.
 
Hivi ni kweli tunahitaji daraja pale Kigamboni? Je, hiyo ndiyo priority yetu kwa sasa? Kama ni hivyo gharama hizo zitatoka wapi?
 
Dua soma thread...

kama wewe huoni priority sawa..ila sote tunajua Kigamboni Kivuko muhim....may be unaishi nje ya DSM au hujawahi kufika kigamboni...

Tumeweka Wizara kila moja ifanye kazi yake...kulala kwa idara moja ya serikali kusifanye idara zingine kulala, au kuamka kwa Idara moja kusifanye watu waone Gere/WIVU au hao wenzao watapata credits/UJIKO...Pesa wachangiaji wamesema zitatoka wapi so far hicho kivuko ninavyoelewa itakuwa TOLL kwa kipindi Fulani kurudisha pesa, then itakuwa FREE
 
Dua soma thread...

kama wewe huoni priority sawa..ila sote tunajua Kigamboni Kivuko muhim....may be unaishi nje ya DSM au hujawahi kufika kigamboni...

Tumeweka Wizara kila moja ifanye kazi yake...kulala kwa idara moja ya serikali kusifanye idara zingine kulala, au kuamka kwa Idara moja kusifanye watu waone Gere/WIVU au hao wenzao watapata credits/UJIKO...Pesa wachangiaji wamesema zitatoka wapi so far hicho kivuko ninavyoelewa itakuwa TOLL kwa kipindi Fulani kurudisha pesa, then itakuwa FREE

Naona wewe ndio unatakiwa kusoma, naweza kukwambia hivi sasa unaweza kuamua kujenga tunnel pale ambayo itakuwa ni rahisi kwa gharama kuliko daraja. Nimeuliza swali wewe unaona kama vile naona wivu/gere. Nione gere ya daraja? usikurupuke mkuu.
 
This is just a confused government. Kila kamradi kanageuzwa deal, sasa watazongania wee, wataanza kazi 2010 ili kuomba kura, uchaguzi ukipita wataacha!
 
QUOTE=Dua;153389]Naona wewe ndio unatakiwa kusoma, naweza kukwambia hivi sasa unaweza kuamua kujenga tunnel pale ambayo itakuwa ni rahisi kwa gharama kuliko daraja. Nimeuliza swali wewe unaona kama vile naona wivu/gere. Nione gere ya daraja? usikurupuke mkuu.[/QUOTE]

Mie si mtaalamu wa Mambo ya Ujenzi...watu wa Civil Engineering wanaweza kusema juu ya kipi kifanywe...[tunnel or bridge]kama wewe mtaalam basi andika mchanganuo maalum kuwashauri wahusika...na pia unaweza iweke hapa JF.

Sijasema issue ya wivu as per ulivyoelewa[labda uwe mtendaji ktk wizara zilizotajwa, kama haupo basi Haumo ktk WIVU]...Nilikusudia juu ya wivu ni kati ya Idara na Idara. Kuna mambo yana tegemeana kiutendaji, NSSF wamesubmit hio proposal yao ya Ujenzi, hawezi jenga hadi Wizara ya Ujenzi ipitie, na pia Wizara ya Fedha na Wizara zingine...ukiangalia NSSF wanachoangalia ni kuwekeza, wizara zingine wanaangalia maslahi..sasa ukichunguza kwa undani kuna mgongano wa ki-Maslahi!!!

Dua kama hunijui mie si mtu wa kukurupuka kama wewe, na kama sina la kuongea huwa nakaa kimya hata wiki, kuangalia wengine wanazungumza nini..sio kujiongezea posts, then nianzishe thread ya kupengezana!!!
Tumsubiri GT kama mwanzilishi ambae anasema atatuletea Faili zima
[/SIZE]
 
Kabla ya kurushiana shutuma, nani ameona design ya hilo daraja na estimates zake? Tunapozungumzia 50% tuna maana gani? Kama nakumbuka vizuri ni kampuni ya kidachi (Adecco?) iliyomtosa Kiula na barabara ya Ilala. Sidhani kama ishu hapa ni 10% maana hata wao wanatoa. Tuliangalie swali kwa undani kwanza.
 
Lawama hapa ni lazima, kwani ishu imezungumziwa miaka mingi lakini hakuna utekelezaji. Tunasubiri wakizama watu ndio tunaikumbuka.

Si lazima kutegemea msaada. Hilo daraja lijengwe kwa mfumo wa BOT (Build, Operate and Transfer). Wawekezaji, prefarably Watanzania, walijenge na wakusanye fedha toka kwa watumiaji.

Watumiaji watakuwa wengi kuliko wanaotumia feri sasa.
Kitakachohitajika ni mkataba (usio wa siri) kati ya serikali na wawekezaji. Mkataba uonyeshe nini kitajengwa, ada ya matumizi, litakuwa mali ya serikali baada ya miaka mingapi, etc.

Haiwezekani tukawa na madaraja na barabara za kutosha na kuridhisha bila kutumia hii njia ya BOT. Malaysia na Thailand wameitumia na imewawezesha kuwa na njia za mawasiliano nzuri sana.

Yajengwe madaraja Kurasini na Kivukoni kwa njia hiyo ya BOT.
Toll roads and toll bridges are things we should embrace.
 
Mie si mtaalamu wa Mambo ya Ujenzi...watu wa Civil Engineering wanaweza kusema juu ya kipi kifanywe...[tunnel or bridge]kama wewe mtaalam basi andika mchanganuo maalum kuwashauri wahusika...na pia unaweza iweke hapa JF.

Sijasema issue ya wivu as per ulivyoelewa[labda uwe mtendaji ktk wizara zilizotajwa, kama haupo basi Haumo ktk WIVU]...Nilikusudia juu ya wivu ni kati ya Idara na Idara. Kuna mambo yana tegemeana kiutendaji, NSSF wamesubmit hio proposal yao ya Ujenzi, hawezi jenga hadi Wizara ya Ujenzi ipitie, na pia Wizara ya Fedha na Wizara zingine...ukiangalia NSSF wanachoangalia ni kuwekeza, wizara zingine wanaangalia maslahi..sasa ukichunguza kwa undani kuna mgongano wa ki-Maslahi!!!

Dua kama hunijui mie si mtu wa kukurupuka kama wewe, na kama sina la kuongea huwa nakaa kimya hata wiki, kuangalia wengine wanazungumza nini..sio kujiongezea posts, then nianzishe thread ya kupengezana!!!
Tumsubiri GT kama mwanzilishi ambae anasema atatuletea Faili zima
[/SIZE]

Kama wewe sio mkurupukaji mbona hukujibu swala nililouliza hili hapa:

Hivi ni kweli tunahitaji daraja pale Kigamboni? Je, hiyo ndiyo priority yetu kwa sasa? Kama ni hivyo gharama hizo zitatoka wapi?

Kama wewe ni kweli hebu tufafanulie majibu ya swala nililouliza hapo juu. Unapoamua kufanya kitu ni lazima uangalie economic benefits hasa kwa swala kama hili ambalo utatuzi wake umekuwa kitendawili kwa miaka kadhaa, bila kusahau pesa zinavyotafunwa kila miaka kwa ajili ya kivuko hewa/daraja ambalo ukiangalia kwa undani hakuna hata mmoja ambaye amefanya study ambayo inakwenda na wakati.

Wewe endelea kumsubiri GT akuletee faili mboga. Na sina mpango wa kukujua kama unavyotaka.
 
Back
Top Bottom