Mwanagenzi
JF-Expert Member
- Sep 11, 2006
- 694
- 212
Naona kama maajabu...
Mmiliki wa hii kampuni, kadri inavyodaiwa na polisi, anatafutwa kuhusiana na kuzama kwa meli yake, Mv Nyamageni, huko Ziwa Nyanza (Victoria!). Juzi juzi wakadai wanamwekea mitego ila anaiepa japo kwa sasa (wakati huo) alikuwa Dar. Haijapita wiki kampuni yake inapewa tenda na wakati kuna kesi ya kuzama kwa meli yake!
Ni kweli kwa sasa hana hatia kwani hajafikishwa mahakamani au kuhukumiwa hivyo, japo ripoti ya Mramba kuhusu kuzama huko kulionyesha kuwa kuna uzembe ulifanyika uliosababisha ajali hiyo, japo kama kawaida ya Bongo, ripoti haikuwekwa yote hadharani. SUMATRA wanasemaje? Idara ya Vivuko mnasemaje? Au ndiyo yale yale ya MIKATABA MIBOVU TULIYOZOEA NCHI HII?
IMALASEKO kuipa serikali mil. 100/- kila mwezi
na Agnes Yamo
KAMPUNI ya IMALASEKO imeshinda zabuni ya kusimamia makusanyo katika vivuko vya Feri, Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Umeme na Ufundi, katika Wizara ya Miundombinu, Mhandisi Mshauri John Ndunguru, alisema IMALASEKO walifanikiwa kushinda zabuni hiyo baada ya kuishinda Kampuni ya Dengard System.
IMALASEKO imefanikiwa kupata zabuni hii kwa kuilipa serikali sh milioni 100 na kuishinda Kampuni ya Dengard System iliyopanga kuilipa serikali sh milioni 80 kwa mwezi.
Makusanyo katika vivuko hivyo kwa siku ni kati ya sh milioni 3.5 na milioni 4, lakini baada ya kufunga mtambo wa kukata tiketi, ikabainika kuwa tuna uwezo wa kukusanya mpaka milioni 10 kwa siku, alisema Ndunguru.
Uamuzi wa serikali kubinafsisha ukusanyaji wa mapato katika vivuko hivyo ulikuwa na lengo la kudhibiti upotevu wa fedha uliokuwa ukifanywa na baadhi ya watendaji wa vivuko. Kampuni ya IMALASEKO ilishinda zabuni hiyo mwishoni mwa Novemba na imeanza kazi Desemba 4, mwaka huu.
Source: Tanzania Daima 17 Desemba 2006.
Mmiliki wa hii kampuni, kadri inavyodaiwa na polisi, anatafutwa kuhusiana na kuzama kwa meli yake, Mv Nyamageni, huko Ziwa Nyanza (Victoria!). Juzi juzi wakadai wanamwekea mitego ila anaiepa japo kwa sasa (wakati huo) alikuwa Dar. Haijapita wiki kampuni yake inapewa tenda na wakati kuna kesi ya kuzama kwa meli yake!
Ni kweli kwa sasa hana hatia kwani hajafikishwa mahakamani au kuhukumiwa hivyo, japo ripoti ya Mramba kuhusu kuzama huko kulionyesha kuwa kuna uzembe ulifanyika uliosababisha ajali hiyo, japo kama kawaida ya Bongo, ripoti haikuwekwa yote hadharani. SUMATRA wanasemaje? Idara ya Vivuko mnasemaje? Au ndiyo yale yale ya MIKATABA MIBOVU TULIYOZOEA NCHI HII?
IMALASEKO kuipa serikali mil. 100/- kila mwezi
na Agnes Yamo
KAMPUNI ya IMALASEKO imeshinda zabuni ya kusimamia makusanyo katika vivuko vya Feri, Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Umeme na Ufundi, katika Wizara ya Miundombinu, Mhandisi Mshauri John Ndunguru, alisema IMALASEKO walifanikiwa kushinda zabuni hiyo baada ya kuishinda Kampuni ya Dengard System.
IMALASEKO imefanikiwa kupata zabuni hii kwa kuilipa serikali sh milioni 100 na kuishinda Kampuni ya Dengard System iliyopanga kuilipa serikali sh milioni 80 kwa mwezi.
Makusanyo katika vivuko hivyo kwa siku ni kati ya sh milioni 3.5 na milioni 4, lakini baada ya kufunga mtambo wa kukata tiketi, ikabainika kuwa tuna uwezo wa kukusanya mpaka milioni 10 kwa siku, alisema Ndunguru.
Uamuzi wa serikali kubinafsisha ukusanyaji wa mapato katika vivuko hivyo ulikuwa na lengo la kudhibiti upotevu wa fedha uliokuwa ukifanywa na baadhi ya watendaji wa vivuko. Kampuni ya IMALASEKO ilishinda zabuni hiyo mwishoni mwa Novemba na imeanza kazi Desemba 4, mwaka huu.
Source: Tanzania Daima 17 Desemba 2006.