Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi waazimia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 unafanyika katika hali ya amani

Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi waazimia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 unafanyika katika hali ya amani

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Nchini wameazimia kuhakikisha kuwa uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 unafanyika katika hali ya amani, utulivu na usalama na kwamba hawatamuonea muhali mtu yeyote atakaye jaribu kuvunja amani ya nchi.

Azimio hilo limefikiwa baada ya kukamilika kwa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi uliofanyika kwa siku tano katika shule ya Polisi Moshi mkoani Kilimanjaro.
WhatsApp Image 2025-08-15 at 17.45.57_fb6654d3.jpg

WhatsApp Image 2025-08-15 at 17.45.58_616d6a33.jpg

WhatsApp Image 2025-08-15 at 17.45.59_5f0e7086.jpg
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Camillus Wambura, Kamishna wa Intelijensi ya Jinai (CP) Charles Mkumbo amesema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kuhakikisha kuwa wananchi wanapiga kura katika hali ya usalama na wamejipanga kudhibiti uhalifu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.

Aidha, CP Mkumbo amesema kuwa, Jeshi la Polisi lina jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika katika mazingira ya usalama, amani na utulivu, Hivyo katika kufikia azma hiyo limeazimia kwa pamoja kusimamia sheria na kanuni zote za nchi, kulinda mikutano ya kisiasa ya vyama vyote na kuweka mazingira bora ya kushirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, viongozi wa kisiasa na wananchi kwa ujumla.
WhatsApp Image 2025-08-15 at 17.45.57_a852f424.jpg

WhatsApp Image 2025-08-15 at 17.45.58_dd17514a.jpg
Akifunga mkutano huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Ally Gugu amesisitiza umuhimu wa Jeshi la Polisi kujipanga vizuri na kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika katika hali ya utulivu huku akilihimiza Jeshi la Polisi kuendelea kubaini vishiria vya uvunjifu wa amani na uchochezi kwenye mitandao ya kijamii wakati wa uchaguzi kwa kushirikiana na wadau wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ili kudhibiti makosa ya kimtandao.

Akigusia maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2025, Katibu Mkuu Gugu alilitaka Jeshi la Polisi kuendelea kusimamia kwa umakini utekelezaji wa mikakati ya kiusalama kuelekea uchaguzi huo.
Alisisitiza umuhimu wa kuhuisha mipangokazi ya uchaguzi, kutoa mafunzo kwa maafisa na askari, na kuhakikisha doria na ulinzi wa misafara ya kisiasa unafanyika kwa ufanisi ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika mazingira ya amani na usalama.
 
Jeshi gani Mpaka leo mmeshindwa kumjua kigogo
 
"Ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa na kufufuka, hivyo hivyo na wale waliolala katika Kristo Yesu Mungu atawafufua pamoja naye"
 
Back
Top Bottom