Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Rais, Dkt. Samia ameyasema hayo tarehe 6 Oktoba 2023, alipokuwa akizungumza kwa njia ya simu na Walimu zaidi ya 2000 Wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita wakati akitoa salamu za Siku ya Walimu Duniani kwa Mwaka 2023.
Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Mwaka huu ya Siku ya Walimu Duniani, Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda amesema Serikali ya Awamu ya Sita imechukua jitihada mbalimbali ili kuboresha Sekta ya Elimu nchini.
Ametaja baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Serikali ni pamoja na kukarabati na kujenga shule mpya ili kukidhi ongezeko la wanafunzi kutokana na mafanikio ya Sera ya Elimu bure ambapo katika mwaka 2022/2023 jumla ya shule mpya 873 zimejengwa.
Pia, ameeleza ili kuhakikisha mtoto wa kike anafanya vyema katika masomo ya sayansi na hisabati, Serikali inaendelea na ujenzi wa shule 26 za kitaifa kwa kila Mkoa ambapo shule 10 zimekamilika na zimeanza kupokea wanafunzi wa kidato cha Tano.
Mizengo Pinda amempongeza, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Doto Biteko kwa kuonesha kwa vitendo jinsi anavyowajali Walimu na kuwaheshimisha na kueleza kuwa, Walimu hao wanapata faraja kuona kuwa kuna kiongozi anatambua nafasi yao katika jamii katika kujenga nchi na kuwaasa Wabunge wengine kuiga mfano huo.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt.Doto Biteko ambaye pia ni Mbunge wa Bukombe, amewaasa wadau wa Sekta ya Elimu kuthamini mchango unaotolewa na Walimu na kazi kubwa wanayoifanya kwa jamii.
Dkt. Biteko ameongeza kuwa, Walimu ndio wazazi, walezi na watoa dira kwenye maisha ya watu wanaowafundisha hivyo wanapaswa kuthaminiwa.
Amesema "Nipende kuwashukuru hawa walimu, wamefanya kazi kubwa na kutoa dira ya mwelekeo wa maisha yangu katika kipindi chote nikiwa kwenye chuo cha ualimu cha Katoke."
Walimu waliopokea tuzo hizo ni pamoja na Mwalimu Justin Temihangwa ambaye kwa sasa ni mstaafu pamoja na Martin Mwombeki ambaye pia ni mstaafu.
Sherehe hizo za Siku ya Mwalimu zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Juma Kipanga, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigella, Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Said Nkumba na baadhi ya Wabunge.