Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 942
Walimu wakuu wa Shule mbalimbali za Wilaya ya Ngara kwa niaba ya Walimu wote wa Wilaya ya Ngara wamekutana Katika Kikao maalumu cha Wakuu wa Shule ambapo kwa kauli Moja wameonyesha kuridhishwa na Utendaji Kazi wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan na Kuahidi kuwachukulia Form za Kugombea nafasi zao.
"Kila Mwalimu Mkuu atatoa Shilingi 10,000. Asilimia 60 ya makusanyo itachangia Fomu ya Urais ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na Asilimia 40 itachangia fomu ya Ubunge ya Ndaisaba George Ruhoro katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025" - Mwalimu Allen Deogratius, Mwenyekiti CWT Wilaya ya Ngara.
"Walimu Wilaya ya Ngara walikuwa hawajapandishwa madaraja kwa kipindi kirefu, lakini kupitia Serikali sikivu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan walimu wameweza kupandishwa madaraja, hivyo wanamshukuru sana Rais Samia" - Mwal. Allen Deogratius, Mwenyekiti CWT Wilaya ya Ngara.
Wakuu hao wa Shule wakiongozwa na Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Ngara Mwalimu Allen Deogratias Marton wameahidi kwa kauli Moja kuwa mabalozi wa Serikali ya Awamu ya Sita Katika maeneo yote watakayofika ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Walimu hao pia wametuma Salamu kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Kumuomba awarejeshee Jembe lao Ndaisaba Ruhoro ambaye amekuwa kimbilio la walimu wa Ngara katika kupigania Masalahi yao hususani suala la Kikokotoo.
Akiwahutubia Walimu Wakuu hao kwa niaba ya Walimu wote wa Wilaya ya Ngara, Mbunge wa Jimbo la Ngara Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amewashukuru walimu hao kwa Imani kubwa waliyonayo kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Lakini pia, Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amewashukuru walimu hao kwa Upendo Mkubwa waliomuonyesha na akaahidi kuwapigania stahiki zao kadri ya uwezo wake wote.
Pamoja na hayo Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amegawa Mitungi ya gesi kwa Shule zote za Serikali Katika ngazi ya Msingi na Sekondari.
#SamiaTena2025
#NgaranaNdaisabaDamDam
"Kila Mwalimu Mkuu atatoa Shilingi 10,000. Asilimia 60 ya makusanyo itachangia Fomu ya Urais ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na Asilimia 40 itachangia fomu ya Ubunge ya Ndaisaba George Ruhoro katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025" - Mwalimu Allen Deogratius, Mwenyekiti CWT Wilaya ya Ngara.
"Walimu Wilaya ya Ngara walikuwa hawajapandishwa madaraja kwa kipindi kirefu, lakini kupitia Serikali sikivu ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan walimu wameweza kupandishwa madaraja, hivyo wanamshukuru sana Rais Samia" - Mwal. Allen Deogratius, Mwenyekiti CWT Wilaya ya Ngara.
Wakuu hao wa Shule wakiongozwa na Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Ngara Mwalimu Allen Deogratias Marton wameahidi kwa kauli Moja kuwa mabalozi wa Serikali ya Awamu ya Sita Katika maeneo yote watakayofika ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Walimu hao pia wametuma Salamu kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Kumuomba awarejeshee Jembe lao Ndaisaba Ruhoro ambaye amekuwa kimbilio la walimu wa Ngara katika kupigania Masalahi yao hususani suala la Kikokotoo.
Akiwahutubia Walimu Wakuu hao kwa niaba ya Walimu wote wa Wilaya ya Ngara, Mbunge wa Jimbo la Ngara Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amewashukuru walimu hao kwa Imani kubwa waliyonayo kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Lakini pia, Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amewashukuru walimu hao kwa Upendo Mkubwa waliomuonyesha na akaahidi kuwapigania stahiki zao kadri ya uwezo wake wote.
Pamoja na hayo Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amegawa Mitungi ya gesi kwa Shule zote za Serikali Katika ngazi ya Msingi na Sekondari.
#SamiaTena2025
#NgaranaNdaisabaDamDam