Kuna watu humu ukiandika mazuri ya CHADEMA na ukaandika mabaya ya CCM, wanakuona ni wa kawaida kwa kuwa unaandika wanayoyapenda wao. Lakini siku utakapoandika mabaya ya CDM na kuyasifia mazuri ya CCM, hata kama yana ukweli, watu watakujia juu. Wanadhani ukiwa CHADEMA basi unatakiwa uwe mnafiki na kusifia kila kitu hata kile chenye kutishia mstakabali wa chama.
Ninajua wengi hivi sasa wanapenda mageuzi na wanayatafuta kwa hali na mali, kiasi cha kwamba wapo tayari kuona chadema inaingia madarakani despite mapungufu yake. Lakini mageuzi ya namna hii yatatuumiza. kama hatutaclear baadhi ya weakness zetu, basi tunaweza kuingia madarakani halafu tukafanya vibaya kuliko hata hao CCM. Jifunzeni kutoka kwa Fredrick Chiluba kule Zambia.
Ni lazima tujenge utamaduni wa kukosoana. Na ni lazima tutambue kwamba CHADEMA kinaongozwa na binadamu wenye tabia kama za wale wa CCM. Kunahitajika kuonyana na kukaripiana ili kurudishana kwenye mstari na kuweza kujitofautisha na CCM. Kama tutaamini kila wafanyacho chadema ni kizuri, na hata wakikosea tunatafuta namna ya kuyapaka mafuta makosa yao, basi tutakimaliza hiki chama yumkini hata ikulu kinaweza kisiingie. Tukosoane ili tujengane.
cc.
Kdm255