Amemwagiwa maji ya baridi mida hii
Kweli kabisa kabisa kwani maji na mafuta haviwi pamoja, yeye wa hovyo analeta mambo ya hovyo yaani hili chemba ni bure kabisa halifai kwa kila pahala.
Amemwagiwa maji ya baridi mida hii
Kinachotufanya tushangilie ni kwamba CCM hawataweza tena kukiita CHADEMA chama cha kigaidi. Maana mahakama imeshatoa hukumu kwamba hakuna ugaidi. Kwahiyo ile single ya ugaidi dhidi ya CHADEMA haina mvuto tena. Itabidi watafute single nyingine, bile kujali kama Lwakatare anapata dhamana au hapati.
Mwigulu njoo na project mpya, hii imeshafeli...
By Tundu Lissu![]()
![]()
Hivi tunavyoandika humu ndani Wilfred Lwakatare yuko mahabusu ya Segerea kwa sababu amenyimwa dhamana kwa makosa ya kutunga ya ugaidi aliyoshtakiwa nayo. Na kwa wasiomfahamu, basi niseme kwamba hali yake ya kiafya sio nzuri kwa sababu anasumbuliwa sana na ugonjwa wa kisukari. Kwa mazingira aliyo nayo, dhana kwamba alitumwa na maCCM ili aihujumu CHADEMA is a bit far-fetched, to say the least. Kwanza kabisa, angekuwa ametumwa basi angetoa kauli ambazo ni more damaging kwa CHADEMA kuliko ilivyo sasa. Nimeisikiliza sana hiyo video clip na narudia kusema kwamba there's nothing in there inayothibitisha chochote kati ya makosa aliyotuhumiwa nayo. Nothing!!! Na hiyo ni kama tuna-assume kwamba video clip yenyewe inaweza kukubalika.mahakamani Kama ushahidi, kitu ambacho sheria ninayoifahamu mie inaniambia hapana. Pili, angekuwa ametumwa basi video hiyo ingemwonyesha yeye pamoja na 'mtumwa' mwenzake Joseph Ludovick Rwezaura ili kukamilisha ushahidi wa njama. Kwa hali ilivyo, video clip hiyo haimwonyeshi mla njama mwenzake na kwa hiyo haiwezi ikawa ushahidi wa kuthibitisha njama zozote. Kosa la kula njama linahitaji wakosaji wawili au zaidi. Aidha, kosa la kufanya mkutano wa kigaidi linahitaji 'magaidi' watatu au zaidi, sio wawili Kama inavyodaiwa katika kesi ya Lwakatare. Kama hakuna mkutano wa kigaidi hakuwezi kuwa na njama ya kufanya makosa ya kigaidi na wala hakuwezi kuwa uhamasishaji wa ugaidi, ambayo ni makosa mengine anayotuhumiwa nayo Lwakatare. Tatu, Ludovick na Dennis Msaki walikuwa na mawasiliano makubwa kati yao kwa zaidi ya mwezi mzima kabla ya tarehe 28 Desemba, siku ya kufanyika kwa makosa yanayodaiwa. In brief, katika kipindi hicho, Ludovick aliongea muda mrefu na Msaki kuliko alivyoongea na mie wake mwenyewe!!! Na hayo ni mbali na mawasiliano kati yake na Mwigulu Nchemba na kale ka-payment ka shilingi 50000 kwa M-Pesa wiki mbili baada ya Mwigulu Nchemba kuutangazia ulimwengu kuwa ana video ya mipango ya mauaji ya viongozi wa CHADEMA!!! Kitu kikubwa inachokithibitisha video clip hii, ukiachia njama dhidi ya CHADEMA na viongozi, ni jinsi ambavyo wahusika ni amateurs kwenye mambo hay a!!! Kwa maneno ya Sugu, 'wanahitaji kurudi studio', maana hii picha imeharibika!!!! !!!!
Nyongeza na magamba wote popote walipo.
kwa hiyo yuko nje kwa dhamana au bado yuo rumande.
Sasa unasomeka.Ameedit sana hii habari. Habari original iliyoletwa hapa ilikuwa na sentensi moja tu. Nashukuru kwamba mods wameondoa post yangu maana kwa sasa haina maana tena. Lakini kwa wakati huo ilikuwa ni mhimu sana.
Hili ni pigo lingine kwa CCM. Tunamshukuru Mungu kwa kuwa upande wa wapigania haki.