ha haaa,
EMT kweli unajua kuchokoza watu walikojificha.......
sidhani kama nazijua hasara za kutokuwa na TV katika chumba cha kulala, ila naweza kusema najua faida za kuwa nayo.
Nakubaliana na point nying ulizoziandika, kama ukiangalia kwa mtazamo wako...... lakini mimi (sisi) tunaangalia kwa kutumia pembe nyingine.
1) Itambulike kuwa siyo sababu una TV basi utakuwa unaiangalia masaa yoote. kama huna umuhimu wa kuangalia haina haja ya kuiwasha.
2) Mimi labda niseme ni wale wa old school, kuna sinema au program kwenye TV ambazo siruhusu wanangu kuziangalia, lakini kwa wakati huo huo mimi napenda kuziangalia. huwezi kujua hiyo sinema itaanza saa ngapi. badala ya kufukuza wanangu kwenda kucheza wakati naangalia kitu roho inapenda, ni bora nikaingia chumbani kwangu nikakaa na kuangalia kwa raha zangu.
3) sidhani kama kweli kuangalia TV kunapunguza muda wa sex katika ndoa, labda niseme inategemea unaangalia vipindi gani kwenye hiyo TV ya chumbani. Mimi napenda sana kuangalia romantic movies (siyo porns), na imeshatutokea mara nyingi tu tukashindwa kuimalizia sinema na kuendelea na mambo yetu. kuna sinema nakumbuka tuliiangalia kwa siku 3 ndo tukaimaliza, siku 2 za mwanzo zote tulikuwa tunaishia njiani.
4) siyo kila program unayoiangalia unakuwa na concentration 100%, mnaweza kuongea huku mnaangalia TV na mkaelewana tu, na kama kuna kitu serious cha kuhitaji 100% basi huwa tunazima TV na kuendelea na maongezi yetu. hatujawahi kukosa/ kupunguza muda wa maongezi sababu ya TV.
5) siyo kila siku wanandoa mnakuwa pamoja katika chumba cha kulala. kuna kusafiri. mmoja akisafiri basi mwingine anakuwa mpweke sana chumbani. kwangu wanangu wanalala latest saa 2. sasa kama mtu kasafiri na mimi nilale saa 2?
6) kusoma huwa nasoma saaana..... hili pia ninalo, ninakuwa na vitabu vya kutosha beside my bed, yaani nikifungua macho kabla sijatoka kitandani lazima nasoma angalau kurasa 2 za kitabu nitakachoguswa kukisoma siku hiyo. kwa maana hiyo kuwa na TV chumbani hakumaanishi utashindwa kujisomea, kuna wakati wa kufanya kila kitu, ni kujipanga tu.
7) ha haaaa, watoto walianza kuwa na TV kabla yangu baada ya kuchoshwa na kuangalia cartoons muda wote wanaotaka kuangalia TV. wao hakuna program wanayotaka kuiangalia zaidi ya cartoon, hata kukiwa na mgeni wanamshauri aangalie cartoon. njia rahisi ya kuwafukuza ni kuwa na TV yao chumbani (NB: hapa haimaanishi wanangu wanaangalia TV muda wote. wana muda wao wa kuangalia, na muda wa kulala huwa unaheshimiwa sana, hawawashi TV wanapotakiwa kulala).
8) kama kuna watu wanayaishi maisha yao ni sisi, tuna vitu vya peke yetu kabisaaaa, hatuyaigi hayo ya kwenye TV, tunaishi ya kwetu.
9) Mimi siyo mpenzi wa kuangalia mpira, mwenzangu ndo ugonjwa wake na mara nyinga anatamani sana niangalie naye. Muda pekee ambao atani-hook kwenye mpira ni kama tutaangalia kwa kitanda, tumejilaza..... huko sebuleni, no thanx.
NB: nakubaliana nawe kila chumba kina kazi yake lakini haimaanishi haziwezi kuingiliana. ndo maana kuna siku hapa tulikuwa tunajadili kuhusu wamama kuhifadhi household stocks chumbani wakati wana stoo sababu tu ya ufujaji wa matumizi ya vitu. Ukiona nina TV chumbani ujue ina matumizi yake ambayo naona yana faida kwangu na kwa mwenzangu