Luninga kwenye chumba cha kulala

Luninga kwenye chumba cha kulala

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,356
couples+who+have+a+TV+in+the+bedroom+have+less+sex+dr+heckle+funny+wtf+facebook+comments.jpg


Kuna baadhi ya watu wa mujini waliobahatika kumiliki au kupanga nyumba yenye vyumba zaidi ya kimoja wanapenda sana kuwa na luninga kwenye chumba cha kulala aka kile chumba chenye nanii ya sita kwa sita. Watu kama Fixed Point watakwambia wazi kwamba:
sijui kwa nini chumba cha kulala napenda kiwe na kitanda na TV ya ukutani tu......

Kwa hiyo, hapo unawezakuta subuleni kuna luninga, chumbani kuna luninga na baadhi ya wale waliobahatika kupata watoto nao wanawawekea luninga kwenye nyumba vya watoto. Watu kama akina Fixed Point watatupa hasara za kutokuwa na luninga kwenye chumba cha kulala. Mie nitaweka hapa faida za kutokuwa na luninga kwenye chumba cha kulala.
  1. Kutokuwepo na luninga kwenye chumba cha kulala ina maana kutakuwa na mazungumzo zaidi baina ya wanaokitumia chumba hicho. Kwa wale ambao wanakitumia chumba hicho peke yao, bado kuna faida nyingi tuu hapo chini.
  2. Kila chumba kwenye nyumba kina shughuli yake. Chumba cha kulala ni mahususi kwa ajili ya shughuli mbili kuu. Wengi mnazijia, sina haja ya kuzitaja hapa.
  3. Maisha ni kuyaishi. Badala ya kupoteza muda wako kuangalia maisha ya watu wengine kwenye luninga ishi maisha yako. Usifanye maisha ya watu wengine kuwa ndiyo burudani ndani ya chumba chako cha kulala. Of course, ni vigumu kuepuka kufuatilia maisha ya watu wengine kwenye luninga lakini weka mipaka hasa ukiwa kwenye chumba chako cha kulala. Don't faill in the trap of watching other people living their lives. Instead live your life: T.I ft. Usher - My Life Your Entertainment Lyrics - YouTube
  4. Kuongezea namba 4 hapo juu, kuyaishi maisha yako ni pamoja na kuwa na muda kutafakari jinsi siku yako ilivyokwenda, ikiwa ni pamoja na kujifunza kutokana na makosa uliyoyafanya siku hiyo. Badala ya kuangalia luninga tumia muda huo chumbani wakati kumetulia na tafakari wapi unaweza kufanya vizuri zaidi kwenye maisha yako. Wanadai kinacho-matter zaidi ni kile unachofikiria mwishoni.
  5. Kama una watoto kuwa mfano kwa watoto wako. Kama nao wakitaka kuwa na luninga kwenye vyumba vyao kama ilivyo kwenye chumba chako utawakatalia kwa kigezo gani?
  6. Kama unasumbuliwa na kutolala kusoma ukiwa kwenye chumba chako hata kama ni threads za JF ni vizuri zaidi kuliko kuangalia luninga. Kusoma ni kuzuri sana kwa ubongo wako. Faida za kusoma zinazidi faida za kuangalia luninga.
  7. Kwa wanandoa kutokuwa na luninga kwenye chumba mean more sex. Inasemekana kuwa wanandoa walio na luninga kwenye vyumba vya kulala wanafanya sex nusu ya wa wanandoa wasiokuwa na luninga. Piga mahesabu mwenyewe hapo.
  8. Hata kama luninga inakaa ukutani bado inachukua nafasi ya chumba. Kama ilivyo kwa vyombo vingi vya kieletroniki, luninga inaleta vumbi chumbani. Luninga inakula umeme pia.
Kwa msaada wa 18 Good Reasons to Get the TV Out of Your Bedroom | Becoming Minimalist

N.B. Huu uzi hauwahusu wale ambao wanamiliki au wamepanga chumba kimoja tuu ambacho wanakitumia kama chumba cha kulala, sebule, jiko, n.k.
 
Utani huuu noma sanaaaa!!
=================
N.B. Huu uzi hauwahusu wale ambao
wanamiliki au wamepanga chumba kimoja tuu
ambacho wanakitumia kama chumba cha
kulala, sebule, jiko, n.k.

N.B. Huu uzi hauwahusu wale
ambao wanamiliki au
wamepanga chumba kimoja tuu
ambacho wanakitumia kama
chumba cha kulala, sebule, jiko,
n.k.

Nikae kando.

Siyo utani bali bali ni reality

Bila kuweka hiyo, baadhi wangeuliza "vipi na sie ambao tunamiliki/tumepanga chumba kimoja tuu?"

Baadhi ya watu wamepitia huko huko mpaka kuwa na uwezo wa kumiliki au kupanga zaidi ya chumba.
 
Kuna ukweli kabisa, ukiwa huna luninga chumbani unalala mapema, ukiwa nayo chineke, utasubiri Fashion Police saa tano usiku hadi saa sita. Ole wake mtu akuguse wakati Joan Rivers anaongea, lazima utamlambua makofi.

Kwa watoto ndio sithubutu hata kugusia kuweka luninga, wanaweza kukesha na top gear.
 
If you want a good sex life, get the TV out of your bedroom!

It can act as a distracting mechanism sometimes...

If you have some evidence based practice you can share with us will be very much appreciated.
 
Kuna ukweli kabisa, ukiwa huna luninga chumbani unalala mapema, ukiwa nayo chineke, utasubiri Fashion Police saa tano usiku hadi saa sita. Ole wake mtu akuguse wakati Joan Rivers anaongea, lazima utamlambua makofi. Kwa watoto ndio sithubutu hata kugusia kuweka luninga, wanaweza kukesha na top gear.

Noma wengine wakiwa hawana luninga chumbani wanalala subuleni kwenye sofa.

Mwisho wanasinzia na kulala fofofo huku TV ikuwa on.
 
inategemea na matumizi ya hiyo luninga humo chumbani mkuu............

wengine huweka kwa matumizi ya kuimarisha pendo na kupata stimu za sex.............

kwa mfano; unawatoto ambao ukikaa sebuleni huwezi kumpakata , kumpapasa , kumkumbatia ile ya kimahaba , kumpetipeti , kumchokoza (romantic teasing) n.k mama yao , ila wewe na mkeo inawalazimu kuangalia baadhi ya vipindi vya tv................ sasa kinyume chake ukiwa na mkeo chumbani pamoja na umuhimu wa kuangalia hivyo vipindi , pia mnaweza kufanya mambo yenu ya mahaba sambamba.
 
If you want a good sex life, get the TV out of your bedroom!


It can act as a distracting mechanism sometimes...

Kuna ukweli kabisa, ukiwa huna luninga chumbani unalala mapema, ukiwa nayo chineke, utasubiri Fashion Police saa tano usiku hadi saa sita. Ole wake mtu akuguse wakati Joan Rivers anaongea, lazima utamlambua makofi.

Kwa watoto ndio sithubutu hata kugusia kuweka luninga, wanaweza kukesha na top gear.

ukiiangalia kwa jicho la pili , hamuwezi kuitumia kuimarisha mahusiano/pendo lenu?
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Hivi enzi za zamani kabla ya TV, wakubwa walikuwa hawafurahii mahabati?

Mie naona mahaba ya kudesa yanachosha kuliko ya kutunga wenyewe, au ni old fasheni?

inategemea na matumizi ya hiyo luninga humo chumbani mkuu............

wengine huweka kwa matumizi ya kuimarisha pendo na kupata stimu za sex.............

kwa mfano; unawatoto ambao ukikaa sebuleni huwezi kumpakata , kumpapasa , kumkumbatia ile ya kimahaba , kumpetipeti , kumchokoza (romantic teasing) n.k mama yao , ila wewe na mkeo inawalazimu kuangalia baadhi ya vipindi vya tv................ sasa kinyume chake ukiwa na mkeo chumbani pamoja na umuhimu wa kuangalia hivyo vipindi , pia mnaweza kufanya mambo yenu ya mahaba sambamba.
 
Kule NAMNAANI mbona runinga ndio mhamasishaji mkuu?

Daah kule ni noma....miaka ya nyuma nilimpeleka mgeni wangu pale nikamsindikiza chumbani...sasa kwenye kypigapiga stori mbili tatu si nikawasha tvii!!!daah almanusura nivunje tv yao!!nilikutana na sarakasi za kufa mtu...imagine mgeni mwenyewe tulikuwa tunaheshmiana ile mbaya
 
inategemea na matumizi ya hiyo luninga humo chumbani mkuu............

wengine huweka kwa matumizi ya kuimarisha pendo na kupata stimu za sex.............

kwa mfano; unawatoto ambao ukikaa sebuleni huwezi kumpakata , kumpapasa , kumkumbatia ile ya kimahaba , kumpetipeti , kumchokoza (romantic teasing) n.k mama yao , ila wewe na mkeo inawalazimu kuangalia baadhi ya vipindi vya tv................ sasa kinyume chake ukiwa na mkeo chumbani pamoja na umuhimu wa kuangalia hivyo vipindi , pia mnaweza kufanya mambo yenu ya mahaba sambamba.

Of course kuna faida za kuwa na TV in the bedroom kama kuangalia chochote unachotaka bila bugudha.

At the end of the day ni kupima faida na hasara za kuwa na luninga in the bedroom.

Kuna uwezekano wa hizo faida kuja na price yake.
 
Back
Top Bottom