asakuta same
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 14,829
- 5,039
EMT Actually inaweza ikawa nzuri au mbaya kutegemeana na matumizi.
-VE
. .Inachangia uchovu wa akili.
Sadly mimi ni mmoja wa watu ambao huwa wanaishia kulala na kuacha tv on. Ukiamka asubuhi macho yanakuwa machovu pamoja na akili kwasababu ya kelele na mwanga.
. .Inasababisha mtu achelewe kulala.
Ukiwa nayo chumbani unashawishika kuangalia na kuangalia na kuangalia hata kama muda uliopanga kulala ulishafika, kwasababu tu ipo karibu.
. . Inaweza kupunguza mawasiliano kati ya wanandoa wawapo chumbani. Badala ya kupiga story na kuchombezana wakati mnautafuta usingizi mama yuko busy na tamthilia/baba yuko busy na news BBC hata kusumbuliwa.
+VE
. . Inapunguza sababu ya mtu kuishia kulala kwenye kochi/sofa na kuambulia maumivu ya shingo na mgongo.
. . Inaweza kuongeza ukaribu kati ya wanandoa.
Badala ya mmoja kubaki sebuleni akisubiria sijui kipindi gani huku mwenzie akienda kubembeleza usingizi peke yake mnaongozana na kama mko vizuri hicho kipindi kinaweza hata kisiangalike.
. . Ukaribu + +
Kama sio wabinafsi mnaweza kujikuta kila mmoja anajenga interest na kile anachopenda mwenzake (mf movie, tamthilia, michezo, habari n.k) kwenye tv kitu ambacho kitaongeza mambo ya ninyi kuzungumzia.
. . Distraction
Bila kusahau kelele kidogo ili kuficha wakati wanandoa wanajishughulisha.
Nadhani jambo la muhimu ni watu kujiangalia tu na kujua walivyo. Wengine inafaa zaidi wawe nazo chumbani, na wengine haifai.
nimeiprnda hii , na siyo kuendekeza hofu na woga usiokuwa na maana....................