jouneGwalu
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 2,696
- 1,806
Hoja za hii sred zimenisukuma sana na nimepoteza uwezo wa kubishana, ila siku zote nimekuwa mtu kupenda kiasi kwenye kila kitu hii imenisaidia sana kutokuwa mtumwa wa interest zangu....
Naamini ninaweza kuwa na luninga chumbani na bado nikitaka kusoma nitasoma na JF nitaingia kama kawaida na majukumu ya kijamii nitahudumia kama inavyonipasa...
Ila kwa mtu usiyeweza kuwa na kiasi kwenye mambo yake nadhani umetoa ushauri wa msingi sana ni vizuri kuiepuka hii kitu!
Kuhusu suala la watoto, watafuata utaratibu wa kawaida tu Tv ya sebuleni ndio yao. Hawawezi kuwa na hoja za kushindwa kujibu eti kwanini mimi nina TV chumbani basi na wao wawe nayo, nitawajibu kwa utaratibu tu na wataelewa.
Naamini ninaweza kuwa na luninga chumbani na bado nikitaka kusoma nitasoma na JF nitaingia kama kawaida na majukumu ya kijamii nitahudumia kama inavyonipasa...
Ila kwa mtu usiyeweza kuwa na kiasi kwenye mambo yake nadhani umetoa ushauri wa msingi sana ni vizuri kuiepuka hii kitu!
Kuhusu suala la watoto, watafuata utaratibu wa kawaida tu Tv ya sebuleni ndio yao. Hawawezi kuwa na hoja za kushindwa kujibu eti kwanini mimi nina TV chumbani basi na wao wawe nayo, nitawajibu kwa utaratibu tu na wataelewa.