Lowassa watajie CHADEMA mali unazomiliki

Lowassa watajie CHADEMA mali unazomiliki

Mkuu Nguruvi3
Wanaojua mali za viongozi ni viongozi wenyewe na pia taasisi iliyokabidhiwa jukumu la kujua mali za viongozi.

Umuhimu upo ndiyo maana kwa sasa wabunge wa CHADEMA wanajikuta wanamshambulia Lowassa bila kufahamu kwa sababu hawafahamu mali zake.

Hata mimi sifahamu kama linafanywa kwa kulipa kisasi lakini ninachokiona ni kuwa nyumba zinabomolewa kwa sababu sheria imevunjwa.

Kufahamu ni kisasi au siyo kisasi ni vigumu sana kama kinachofanyika kiko kisheria.

Haya maswali siwezi kuyajibu kwa sababu sihusiki na masuala unayoyauliza.

Suala la Lugumi kuna Kamati Ndogo ya Bunge inafanya kazi nani matumaini yangu mwisho wa mwezi huu itakuja na majibu ya maswali yako.
lusungo nimekusikia mkuu, ahsante kwa ushauri elekezi naufuata.
Mambo ni kama haya
 
Napata mashaka kuwa huu waweza kuwa mchezo wa kisiasa unaochezwa kisayansi na Waziri ameingia king.
Shamba kubwa kama hilo sio rahisi Mbunge na wananchi jirani wasifahamu kuwa linamilikiwa na Lowassa. Pengine Lowasa kesha ridhia lirudi serikalini ili wapewe watu, lakini waziri kutamka kuwa wanalirudisha kutokana na kauli ya Mbunge tuu basi sasa mashamba mengi ya viongozi itabidi yarudishwe kama la Lowasa pale Mbunge yeyote atakapo mention wapi kuna shamba halijaendelezwa.
Baada ya hapo ni wangapi walio madarakani wataumia?
Hatuwezi kufahamu kwa sababu siasa za Tanzania sio kama tuzijuavyo lakini kilichojitokeza ndicho hicho na mbaya zaidi hata Mbunge alionekana kushangaa baada ya kuambiwa shamba linamilikiwa na Lowassa.

Unafahamu kuna viongozi wengi tu wa serikali na CCM walijimilikisha mashamba makubwa baada ya nchi kuingia kwenye soko huria.

Migogoro kama hii ya ardhi inatufanya tufahamu wamiliki wa hayo mashamba makubwa.
 
Nyumbu katika ubora wao mkuu hawajui waendako
Inashangaza mtu anaibuka na jazba huku ametanguliza hoja za nguvu kwa sababu nimemtaja Edward Lowassa.

Inashangaza hawa ma-fanatics wanaomtetea Lowassa kwa sasa ni wale ambao walikuwa wanamtukana na kumsema ni fisadi papa kabla hajajiunga CHADEMA.
 
MsemajiUkweli,

Kauli ya Kikwete kwenye kamati kuu yenu huko CCM kwamba Lowassa bado ni tishio ni kauli inayowasumbua sana. Kutangaza mali za Lowassa sio kazi ya Chadema, kama ilivyokuwa kwa mali za Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli, hiyo sio kazi ya Chama Cha Mapinduzi. Kama ana mali ambazo mna uhakika ni mali 'haramu', zipo njia za kufuata kukabiliana na hilo, na mnazijua. Na katika njia zote, Jamiiforums sio njia sahihi.


MsemajiUkweli, Kuonyesha nyumba ya mdogo wa Lowassa ikibomolewa inaweza kuwa ni sawa tu na kuonyesha ile nyumba ya Kikwete Masaki inayojengwa na Lugumi. Haitatui tatizo lililopo.

Vinginevyo kwa akili ya kawaida, tena sana, na kwa experience ya marais waliopita huko nyuma, kilicho muhimu kwa sasa ni kwa Rais aliyepo madarakani kuonyesha kile alichowasilisha kwa tume ya maadili kuhusu mali zake. Kwanini 'yaliyomo' hayajawekwa hadharani' na badala yake yana fichwa fichwa kama kweli nia ya dhati ipo?

Vipi kuhusu makato ya kodi ya mshahara wa Rais?

Onyesheni njia, ongozeni kwa mfano.
andiko lako linaonyesha kabisa jinsi unavyotumika na mafisadi kwa kujaribu kutetea uozo na ufisadi. lakini ukweli utabaki kuwa ukweli tu. no matter what. na penye ukweli uongo hujitenga. jua hilo.
 
Hatuwezi kufahamu kwa sababu siasa za Tanzania sio kama tuzijuavyo lakini kilichojitokeza ndicho hicho na mbaya zaidi hata Mbunge alionekana kushangaa baada ya kuambiwa shamba linamilikiwa na Lowassa.

Unafahamu kuna viongozi wengi tu wa serikali na CCM walijimilisha mashamba makubwa baada ya nchi kuingia kwenye soko huria.

Migogoro kama hii ya ardhi inatufanya tufahamu wamiliki wa hayo mashamba makubwa.

Ni kweli ilikuwa ni fursa kama ile iliyotokea Urusi wakati ule kuhusu viwanda. Mie sina taabu kabisa kama ni Lowassa, Mbowe, Kiongozi yeyote wa CCM au mfanyabiashara mkubwa aliye pata shamba kihalali wakati huo na kama halitumii na kuliendeleza alirudishe kisheria na watu wapewe ardhi ili kuondoa migogoro hii ya ardhi.
Watu wanagombana na kuuana sio kwa vile ni wagomvi tuu bali kuna uhaba wa ardhi na mahitaji ni makubwa na yanaongezeka kila siku. Ardhi ni mali ya umma na haipaswi kupewa mtu halafu haiendelezi. Hata mie tule tuekari twangu tutatu kama siendelezi kwa nini wasipewe wanaohitaji? Sidhani kama hilo lina mjadala bali tuisaidie serikali na jamii inufaike.
 
Inashangaza mtu anaibuka na jazba huku ametanguliza hoja za nguvu kwa sababu nimemtaja Edward Lowassa.

Inashangaza hawa ma-fanatics wanaomtetea Lowassa kwa sasa ni wale ambao walikuwa wanamtukana na kumsema ni fisadi papa kabla hajajiunga CHADEMA.
Akitajwa Lowasa tu kosa hayo maheka yote ya nn na katika andiko lako umeeleza wazi ukiwasaidia wao
 
andiko lako linaonyesha kabisa jinsi unavyotumika na mafisadi kwa kujaribu kutetea uozo na ufisadi. lakini ukweli utabaki kuwa ukweli tu. no matter what. na penye ukweli uongo hujitenga. jua hilo.

Fisadi gani ambae yupo nje ya CCM lakini bado mmekosa namna ya kumshughulikia zaidi ya kulia lia tu kwenye vikao vya kamati kuu (CCM)?

Fisadi gani ambae mbele ya TV (live kitaifa) alisema wazi kwamba Richmond ni ya Kikwete na kwamba aliamua kufuta mkataba lakini Katibu Mkuu Kiongozi Bwana Luhanjo akasema hapana kwa sababu Rais amesema mkataba usifutwe? Lowassa akaenda mbali na kusema kama mnataka zaidi tukutane mahakamani. Hadi leo kimyaaaa. Hamuwezi thubutu kwani mnajua mtaumbuka.

Tangia wakati huo, wananchi wakaelewa pumba ziwekwe ungo upi, na mchele ungo upi. Wakaelewa kwanini Mwakyembe alisema bungeni kwamba kamati yake inalazimika kuficha mengine ili kuilinda serikali. Serikali gani hiyo inayolindwa baada ya kumtoa Waziri Mkuu, upo hapo?

Wananchi walishagutuka. Walishaelewa kwamba utawala wa awamu ya nne ulijaa fitina na nguvu za giza. Ndio maana katika uchaguzi mkuu wa Urais, wananchi walimpa Lowassa ushindi kabla hamjaleta wataalam wenu wa nje kuja kutungua takwimu angani kabla hazijateremka kwa Lubuva pale NEC. Na Lowassa amerudia mara nyingi kwamba 'hata Magufuli anajua kwamba ushindi wake ni wa kuiba kura', lakini katika hili, hadi leo, CCM na serikali yake kimyaaa.Hamuwezi thubutu kwani mnajua mtaumbuka.

Katika hili danganyeni wengine, sio wananchi waliompa kura ya ushindi Lowassa, ambao pamoja na kutoboa kibaba cha kura, zikabakia 6 million plus.
 
Lowasa kweli kiboko, msemajiukweli mnaonesha jinsi gan hamlali wala hamuendi kwa chooo kisha lowasa
Hata shetani ni kiboko kwa sababu kuna watu huwa wanakesha wala hawaendi choo.

Shetani kuwa kiboko haina maana kuwa anachokifanya ni kizuri.

Hata Lowassa kuwa kiboko haina maana anachokifanya ni kizuri.
 
Lowassa kamwe hawezi kutaja mali zake hata Mbowe na Lissu wanalijua hilo
Inabidi awasaidie wabunge wa CHADEMA na bila kufanya hivyo watakuwa wanamnanga kila mara bila wao kufahamu. Badala ya wabunge wa CHADEMA kumjenga, kwa sasa wanachofanya ni kuendelea kumuua zaidi kisiasa.
 
TUME YA MAADILI YA VIONGOZI NA KATAZO KWA MTU KUSAMBAZA TAARIFA ZA MALI ZA VIONGOZI KWA UMMA

Nipashe ilizungumza na Jaji Kaganda kujua kama Kikwete alishatoa tamko kama Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995 na kanuni zake zinavyoelekeza, lakini pia kufahamu idadi ya mali anazomiliki Rais huyo mstaafu na thamani yake.

Kaganda alisema ni kweli Kikwete aliorodhesha mali zake zote kwa tume lakini Jaji huyo alikataa katakata kumwonyesha mwandishi wa habari hizi tamko hilo.

Jaji Kaganda alisema sheria inazuia kumwonyesha mtu mwingine tamko la mali la mtu mwingine hadi kuwe na sababu ya maana ya anayehitaji, na pia kuwe na ulazima wa kufanya hivyo.

"Mwananchi anaweza kupata taarifa za mali za viongozi kwa kufuata utaratibu uliopo, lakini baada ya kupata taarifa hizo, haruhusiwi kuzitangaza au kuzichapisha kwenye vyombo vya habari,” alisema Jaji Kaganda.

Source: NIPASHE Rais mstaafu Jakaya Kikwete ametaja mali alizochuma alipokuwa madarakani

N.B
Maana yake sheria zilizopo Tanzania zinakataza kutangaza mali za viongozi na ni kosa kisheria katika matumizi ya mitandao kutangaza mali za viongozi
.
 
Monduli watu wanateseka kwa ufisadi wa mamvi kwa muda mrefu sana
Wananchi wa Monduli walikuwa wanailaani serikali kumbe kikulacho kilikuwa ndani ya nguo zao!

Pamoja na kupiga kelele huku wakilaani, lakini Lowassa alikuwa kimya kama vile hawasikii wakati alikuwa ni Mbunge wao na mbaya zaidi shamba alikuwa amejimilikisha bila hata kuliendeleza.
 
Mbunge alikuwa sahihi katika kutimiza wajibu wake lakini kwa sababu hakuwa well informed ndio maana akajikuta anamshambulia Lowassa bila kufahamu.

Ni kweli kama angekuwa anafahamu kuwa shamba nila Edward Lowassa, nadhani approach yake kuhusiana na suala hilo ingekuwa ni tofauti.
Kwa hiyo alikosea?
 
Kwani tumemkataza Lowassa kufanya yake?

Nimemuomba awaeleze CHADEMA mali zake ili kuepuka aibu inayojitokeza kwa wabunge wa CHADEMA ambao ni wazalendo wakati wa kutimiza majukumu yao.


Kumbe UDA ccm mlishaambiwa ndo mana mnamkingia kifua mkubwa flani ila si kwa maslahi ya taifa! Kwa nn usimpongeze mbunge hata kama hajui kuwa ni la lowasa kasaidia kuokoa ardhi kama lipo kinyume na utaratibu? Kwa hiyo unaunga mkono kuficha siri za wanasiasa ili raia waendelee kunyanyasika juu ya rasilimali zao?
 
Inabidi awasaidie wabunge wa CHADEMA na bila kufanya hivyo watakuwa wanamnanga kila mara bila wao kufahamu. Badala ya wabunge wa CHADEMA kumjenga, kwa sasa wanachofanya ni kuendelea kumuua zaidi kisiasa.


Kumbe kuficha maovu ndo kujengeka kisiasa ndo mana yule jamaa kalamba cheo bungeni kwa mwendo huu huko bado kuna uozo wa hali ya juu.
 
Tunataka sukari huu sio muda wa propaganda.
Kijana jufinze kuishi maisha mazuri na YENYE afya. Sukari ni mbaya kwa afya yako. Tujifunze kula vya afya asubuhi na mapema. JEE umewahi kukausha vizazi vitamu baadaye ukausaga ukawa unga, na ukatengeneza uji wa unga wa viazi vitamu. Ni mtamu, wenye afya na totally organic, na wenye gharama ndogo sana.

Tuwe wabunifu na wapenda afya.
 
Jaribu kutumia hata common sense unaposema likitamkwa jina la Lowassa eti matumbo ya wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM huwasokota. Lowassa yupi huyo unayemsema? Huyu ambaye kwa sasa hata kuongea dakika kumi ni majanga?

Lowassa huyu ambaye alikuwa anadekiwa barabara lakini jina lake likakatwa na kalamu ya shilingi mia sita halafu leo matumbo yawasokote? Hebu acha utani. Hili siyo jukwaa la utani na udaku.
Sometimes common sense isn't common to all. Jamaa kakustua kidogo and you have come out kuonesha kwamba mada yako is based on hate sio uzalendo.
 
Back
Top Bottom