Fisadi gani ambae yupo nje ya CCM lakini bado mmekosa namna ya kumshughulikia zaidi ya kulia lia tu kwenye vikao vya kamati kuu (CCM)?
Fisadi gani ambae mbele ya TV (live kitaifa) alisema wazi kwamba Richmond ni ya Kikwete na kwamba aliamua kufuta mkataba lakini Katibu Mkuu Kiongozi Bwana Luhanjo akasema hapana kwa sababu Rais amese mkataba usifutwe? Lowassa akaenda mbali na kusema kama mnataka zaidi tukutane mahakamani. Hadi leo kimyaaaa. Hamuwezi thubutu kwani mnajua mtaumbuka.
Tangia wakati huo, wananchi wakaelewa pumba ziwekwe ungo upi, na mchele ungo upi. Wakaelewa kwanini Mwakyembe alisema bungeni kwamba kamati yake inalazimika kuficha mengine ili kuilinda serikali. Serikali gani hiyo inayolindwa baada ya kumtoa Waziri Mkuu, upo hapo?
Wananchi walishagutuka. Walishaelewa kwamba utawala wa awamu ya nne ulijaa fitina na nguvu za giza. Ndio maana katika uchaguzi mkuu wa Urais, wananchi walimpa Lowassa ushindi kabla hamjaleta wataalam wenu wa nje kuja kutungua takwimu angani kabla hazijateremka kwa Lubuva pale NEC. Na Lowassa amerudia mara nyingi kwamba 'hata Magufuli anajua kwamba ushindi wake ni wa kuiba kura', lakini katika hili, hadi leo, CCM na serikali yake kimyaaa.Hamuwezi thubutu kwani mnajua mtaumbuka.
Katika hili danganyeni wengine, sio wananchi waliompa kura ya ushindi Lowassa, ambao pamoja na kutoboa kibaba cha kura, zikabakia 6 million plus.