Lowassa watajie CHADEMA mali unazomiliki

Lowassa watajie CHADEMA mali unazomiliki

Kinachonishangaza ukitamka jina la Lowassa kwenye thread, wanajeshi wake wanaibuka kutoka mafichoni na kuanza kurusha risasi bila kuangalia hata sababu za jina lake kutamkwa.

Wengi hawatumii nguvu za hoja bali wanatumia jaziba na hoja za nguvu.


Unalitamka jina unafahamu kabisa iptl wanapokea pesa za bure toka tanesco serikali yako inachekacheka nae tu kwa nn hawaokoi pesa za umma wakat wanajua kuna upigaji ktk mkataba wa richmond? kamata mafisad peleka mahakaman fungia jela wakibainika sio mnakuja kujaza maupupu huku wakat kila kitu kipo wazi.

Ni muda wa serikali kuwa wazi sio kutumia huo mwanya kupaka bila kuchukua hatua tunaweza kusema chadema walikuwa hawana nguvu ya kumuwajibisha lowasa kwa kuwa alikuwa ccm sasa nanyie mmegeuka wale wale wakat kila kitu kipo waz. Mtu mmoja anasura mbili.

Kwa mlolongo huo kwa nn lowasa asitetewe ikiwa serikali ipo kimya toka 2008? Mtu mwenye hatia hana hata uwezo wa kuchukua fom ya kugombea uongoz mkubwa ikiwa tayar yupo nje ya maadili ya utumish wa umma unafikir yeye alipokuwa anajitangaza kuutaka urais hakufiria kama angedakwa kiurahis na serikali ya ccm kama yupo nje ya maadili?
 
Wabunge wa ccm ambao ni wajumbe wa kamati kuu wanamjua Magufuli?
Siwezi kufahamu kama hawamfahamu lakini mpaka sasa hakuna hata dalili inayoonyesha kama hawamfahamu kama ilivyotokea kwa wabunge wa CHADEMA ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu kuhusu Edward Lowassa.
 
Ni lkn lowasa ni mmojawapo!!;xo kukaa kimya ujue mfumo taratibu uanaanza kukolea hasa baada ya kunyoosha mlimopinda!!

Kama sikuelewi, kama ni mfumo unaanza kukaa vyema ilitakiwa hilo kutajwa mapema na sio kungoja mpaka mbunge wa upinzani aseme halafu tofauti za kisiasa zitumike kuweka mfumo sawa. Kuna majengo na mashamba mengi yanamilikiwa na viongozi waliowahi kukamata madaraka ya nchi hii kinyume na sheria lakini wanakaliwa kimya mpaka sasa, na wasipoenda upinzani ukijaribu kusema utaambiwa ni uchochezi. Hatuna tatizo iwapo Lowassa kajimilikisha shamba kinyume na sheria basi sheria ifuate mkondo wake, lakini isiwe kwake tu kwani wengi wanaomiliki kwa jinsi hiyo huko ndani ya ccm ni wengi kuliko huyo Lowassa mmoja. Narudia tena, kinachoanza kupunguza kasi ya Magufuli ni huo uchafu unaofanywa ama uliofanywa na wanaccm kiasi kwamba hana analoweza kufanya bila kujikuta katika wakati mgumu.
 
Inaonekana bila kumtaja mwanaume Lowasa mnapata homa eeee, fanyeni kazi kwa bidii au ndo mmesha kunywa kinywaji cha aina ya Kitwanga!!
 
Siwezi kufahamu kama hawamfahamu lakini mpaka sasa hakuna hata dalili inayoonyesha kama hawamfahamu kama ilivyotokea kwa wabunge wa CHADEMA ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu kuhusu Edward Lowassa.

Hapa ni kama kwa mada hii umeiabisha ccm na kuiacha uchi japo unadhani unaichafua cdm. Sasa ndio tumejua ukweli ulivyo, ukiwa ccm ni halali kumiliki mali kinyume na sheria na hakuna atakayekutaja, ila ukihama tu ndio makosa yako yatatajwa. Pia nitakuwa sijakosea iwapo nitasema kama unataka mabaya yako yafichwe basi baki ccm lakini ukiwa upinzani kila kitu kitakuwa hadharani.
 
Napata mashaka kuwa huu waweza kuwa mchezo wa kisiasa unaochezwa kisayansi na Waziri ameingia king.
Shamba kubwa kama hilo sio rahisi Mbunge na wananchi jirani wasifahamu kuwa linamilikiwa na Lowassa. Pengine Lowasa kesha ridhia lirudi serikalini ili wapewe watu, lakini waziri kutamka kuwa wanalirudisha kutokana na kauli ya Mbunge tuu basi sasa mashamba mengi ya viongozi itabidi yarudishwe kama la Lowasa pale Mbunge yeyote atakapo mention wapi kuna shamba halijaendelezwa.
Baada ya hapo ni wangapi walio madarakani wataumia?

Unajua kuna upumbavu flani unafanyika hapa, kuna watu wanaishi nje ya siasa na wanapenda kusikia na kuona yale mazuri yakifanywa na serikali..sasa Lukuvi anapokuja na hati iliyosainiwa na aliewai kuwa waziri wa ardhi kisiasa bila ya kufanya hivyo kwa nyakati zote na sehemu zote ambazo ameweza kutatua matatizo ya ardhi ni kama anasanifu wananchi.

Ni kwanini ajaweza kuonesha ata saini ya maafisa ardhi kwingine alikopata kuna matatizo ya ardhi? acheni kufanya siasa kwa kujifurahisha! siasa ni maendeleo kwa dunia ya sasa, wala haingii akilini kua miaka yote eneo lilikua limekaa bila kuendelezwa na wananchi wanayo shida ya ardhi alafu leo unakuja na hati kisiasa bila aibu utafikiri ukuwai kusikia kilio cha wananchi juu ya ardhi hiyo wala serikali haikuwepo, mnafanya matani sana kwa wananchi.
 
Udaku upo kwenye bandiko namba moja. Jibu swali, acha kujiuma uma:

Kwanini Magufuli hatangazii CCM na wananchi wa ujumla ana miliki mali gani???
Hoja yako ni nini?

Mimi sijasema Lowassa awatangazie wananchi mali zake. Soma vizuri mada yangu ili uelewe vizuri.

Unalazimisha kunipeleka kwenye hoja ambazo hazikuwa msingi wa hoja yangu.
 
Hoja yako ni nini?

Mimi sijasema Lowassa awatangazie wananchi mali zake. Soma vizuri mada yangu ili uelewe vizuri.

Unalazimisha kunipeleka kwenye hoja ambazo hazikuwa msingi wa hoja yangu.
Hoja yako ni kwamba Lowassa awatangazie chadema Mali zake. Nimeuliza swali rahisi tu, je Kwanini Magufuli asifanye hivyo kwa CCM? Hauna majibu.

Ukiwa kama MwanaDiwani ulimtetea Kikwete na udhaifu wake kama Kiongozi, udhaifu uliotuingiza kwenye shimo refu. Kikwete kuondoka, unakuja kama MsemajiUkweli. Ukweli upi huo kama hata Swali langu dogo tu la JPM linakushinda?

Na kwanini unaendelea kukwepa maswali ya Nguruvi3 huko juu?

Sent from my SM-G530H using JamiiForums mobile app
 
Tangu nimeona yule Mnywa Viroba ndo Waziri hawa makenge wanaolipwa buku 7 hawanipi tabu. Huwa wakishakunywa Kibuku kama mawaziri wao KITWANGA To be specific Huwa wanakurupuka kama Nguruwe na kuja JF. Hakuna haja ya kupambana nao kuwaelewesha ni sawa na kufuga Nguruwe kama PET animal. *Cuk
 
Siwezi kufahamu kama hawamfahamu lakini mpaka sasa hakuna hata dalili inayoonyesha kama hawamfahamu kama ilivyotokea kwa wabunge wa CHADEMA ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu kuhusu Edward Lowassa.

Sasa huu si upumbavu ndo unatuletea hapa, unataka watu wasimtete Lowasa wakati serikali haijamwajibisha miaka nenda miaka rudi...........pereka ujinga wako huko,kumwajibisha hamtaki..kumtetea hamtaki...kunyamaza kimya hamtaki...kumbeba hamyaki...
 
Ndugu yangu Mchambuzi, Tafadhali sana... Unajinajisi mno kubishana na haya mazalia ya laana!! Ufahamu wao upo ktk robot system!! Kwa uwezo na hadhi yako si viumbe wa kufanya nao mjadala!! Please achana nao hao vinyaa.
Tatizo lako huelewi hata mantiki ya kile unachokifanya.

Unawaambia wengine wasifanye mjadala wakati wewe unafanya mjadala. Tumia hata common sense ili ufahamu kuwa kutoa komenti ni moja ya kufanya mjadala.

Ili usionekane unafanya mjadala na haya unayoita mazalia ya laana, usingetoa comment yoyote kwenye thread ya mazalia ya laana, otherwise, wewe ni zaidi ya mazalia ya laana.
 
Mkuu Nguruvi3 heshima yako.... Kubishana na hivyo viumbe ni sawa na kuweka dhahabu kwenye pua ya nguruwe... Nafikiri umenielewa.
Wewe kama unafahamu hayo unayoyasema, kiherehere gani na unafiki wa aina gani unakufanya uingie kwenye thread ya hawa viumbe?

Kama hufahamu hata mantiki ya kile unachokifanya utaweza kutoa ushauri sahihi kwa watu wengine hasa wenye fikra pana.

Unachokifanya ni kusambaza ujinga wako katika msingi wa ushauri na ninaamini mtu mwenye fikra pana hawezi kupokea ujinga.
 
Monduli pale kuna mtu anaitwa Kadogoo ndo mwenyekiti wa Halmashauri ile ni kibaraka mzuri wa lowassa nadhan chadema wamtumie huyu atwasaidia kumjua lowassa maana fact ni kwmba kumpokea lowasa chadema kulifanyikaga kw kukurupuka tu bila uchunguzi wa kina kuhusu huyu mtu
 
Hapa ishu sio ukongwe JF, kituko ni Mbunge wa Chadema alieteuliwa na Chadema na kupitishwa na Chadema kwa ushawishi wa Lowasa kwenda bungeni kulalamikia shamba lilliporwa na Lowasa.

Sidhani kama angejua lile shamba ni miliki ya Lowasa angethubutu hata kufungua mdomo bungeni kuhoji umiliki wa hilo shamba.!
Mbunge alikuwa sahihi katika kutimiza wajibu wake lakini kwa sababu hakuwa well informed ndio maana akajikuta anamshambulia Lowassa bila kufahamu.

Ni kweli kama angekuwa anafahamu kuwa shamba nila Edward Lowassa, nadhani approach yake kuhusiana na suala hilo ingekuwa ni tofauti.
 
Mimi huwa sielewi watu kila Mara kumsema Lowassa wakasahau kuwa ufisadi ni kila kona ya CCM.

Lowassa sidhani kama aliuza nyumba za serikali, aliyeuza yupo lakini haguswi

Baada ya Lowassa kujiengua toka serikalini tumeona EPA, Escrow, mikataba mibovu ya Gas na madini, Lugumi na mengine mengi. Ni kwa nini yote haya yanafumbiwa macho na badala yake anatajwa lLowassa? CCM mnataka kutuaminisha nini Watanzania? Mwenye macho haambiwi tazama!

Wabunge pamoja na mawaziri ndo wanaomiliki shule za binafsi, biashara kubwa na makàmpuni ambayo ndo uzao wa ufisadi katika nchi hii, lakini hao hao ndo viongozi wa nchi, tutegemee nini? Kama tunategemea mabadiliko nadhani ni ndoto ya alinacha.

Kwa namna nchi inavyokwenda, kama tunataka kuona madiliko ya kweli sio Leo wala kesho, labda miaka hamsini ijayo, lakini kwa sasa tusjidanganye
Maelezo yako ni marefu lakini yako nje ya mada!

Soma vizuri mada yangu ili uelewe mantiki ya hoja zangu!
 
HIVI KAMA LUKUVI AKISAINI HATI ZA VIWANJA NA MASHAMBA YATAKUWA YA LUKUVI? NAONA MWANADIWANI ANATOKWA POVU KISA LOWASSA ALISAINI HATI YA SHAMBA NA HILO SHAMBA UMILIKI UMEBADILISHWA? MSITULETEE UKENGE HAPA MWACHENI LOWASSA AFANYE YAKE
Kwani tumemkataza Lowassa kufanya yake?

Nimemuomba awaeleze CHADEMA mali zake ili kuepuka aibu inayojitokeza kwa wabunge wa CHADEMA ambao ni wazalendo wakati wa kutimiza majukumu yao.
 
Wabunge wa ccm ambao ni wajumbe wa kamati kuu wanamjua Magufuli?
Pengine wanamjua kwa sababu hakuna siku wamesimama kuongea mambo ya magufuli hadharani bila ya kujua kama wafanyavyo hao wa upande wa pili kwa kutamka baadhi ya mambo wakidhani wanaisema serikali kabla ya baadaye kung'amua waliyemsema ni Edo.
 
Back
Top Bottom