Siko hapa kumtetea Lowassa, lakini katika mambo yanayotuacha hoi wananchi ni pamoja na hili. Hakuna asiyejua jinsi viongozi wa ccm walivyozitumia nafasi zao kulihujumu taifa hili. Kila mtu anajua Lowassa pamoja na viongozi wengine wa ccm wamejimilikisha mali nyingi ya taifa hili isivyo halali kwa kutumia nafasi ya chama chao kushika dola kuhozi mali za umma isivyo halali. Na sio viongozi tu wa ccm bali hata chama chenyewe cha ccm kinamiliki vitega uchumi vingi vililetwa na wananchi wote wakati wa mfumo wa chama kimoja. Hili la shamba la Lowassa unaliongea kama mtaji wa kisiasa ili ccm ionekane iko vizuri, lakini ukweli unabaki palepale viongozi karibia wote wa ccm waliowahi kupata madaraka hasa ya serekali katika nchi hii wanamiliki mali nyingi kinyume na sheria za nchi.
Hali hiyo ndio inafanya ccm iwe tayari hata kwa machafuko kubaki madarakani ili kulinda maslahi ya viongozi wake wachache, kwani inajua pindi watakapopoteza dola wenye kumiliki mashamba kama Lowassa, viwanja vya wazi na viwanda isivyo halali watakuwa ni wengi kupita kiasi. Rais Magufuli alianza na kasi kubwa kwenye awamu yake, lakini kadiri siku zinavyokwenda anazidi kushindwa kutekeleza majukumu yake, kwani anaopaswa kuwabana ndio hao wanaojiita vigogo wa ccm. Usishangae sasa Lowassa kuanza kuibuka kwa kasi kwani ameshajua rais ameanza kuujua ukweli na hana la kufanya zaidi ya kuwa mpole. Kwa maneno marahisi hawezi kukata tawi alilokalia. Kasi yake naifananisha na jinsi alivyoanza JK, lakini akaishia kuwa mtalii wa kiwango cha guiness book of record.