Lowassa: Wakimwaga mboga namwaga ugali

Lowassa: Wakimwaga mboga namwaga ugali

Kwani kuna kitu Lowasa kafanya cha ajabu bila presidaa kushirikishwa,kama vp na presidaa apewe barua ajivue gamba.

Kweli what goes around comes around. Muhusika mkuu alifikiri ame-get away with this. Naona ahadi zake hewa alimpa mpaka Lowassa i.e. matarajio yakuwa raisi sasa anamgeuka. Bad luck! sio wote wanakubali yaishe, wengine lazima watunishe misuli. Sijui na muhusika mkuu itabidi ajivue gamba?
 
muda wote alikuwa wapi asimwage huo ugali au baada ya kutoswa ndio anajifanya mwema? Mnafiki tu hana mpango wowote
 
I believe the same way too. Lowassa amemshtukia JK ni ndumilakuwili sasa anataka kumuumbua. Kambi ya Lowassa ina-question uhalali wa JK kuwazunguka wakati kwenye deal nyingi walikua pamoja. Kwa mtizamo mwingine Lowassa ana haki yakusimamia haki yake kikatiba ya kupigania uraisi -sioni kwanini wamzuie. Kama kweli hawamwogopi Lowassa si waache apiganie alafu wasipitishe jina lake? Hii yote inaonyesha jinsi CCM fears Lowassa group. JK ameumbuka na anaendelea kuumbuka. He should man up and face Lowassa. Quite frankly hii mambo ya kung'ata na kupuliza ina-work kwa watu kama kina Makamba lakini sio Lowassa. Rostam anaweza akakubali yaishe sababu hana ndoto yakuwa raisi na ameshaneemeka vyakutosha. Lakini Lowassa wants to be a president, he wants society to believe he was a victim on Richmond issue etc, he can not go down easily.
Mkuu samahani kwa maswali haya.kama Lowassa ahakuwa muhusika wa Richmond kwanini alikubali kujivua gamba la uwaziri mkuu? Na uzuri wa Lowassa tunauona leo kwasababu anapingana na kikwete?
 
Yanayo mkuta Kikwete ni kwamba anaandamwa kwasababu ya dini yake, yanayomkuta Lowasa ni haki yake lazima asurubiwe.

Mbona wakati mnasaini mikataba mibovu hamkumbuki dini? Mbona wakati mnafanya usanii na undumilakuwili/kudhulumu wengine hamkumbuki dini? Mnataka ku-play victim pale mambo yanapokua magumu? Hii inatudhibitishia Watanzania we have the wrong person in the job. Dini inatumika tu pale inapokua convinient- Shame shame shame!!
 
asilimia 60 ya wapiga kura watakaopiga kura 2015 hawatafanya jambo linalostahili na linalohitajika na tanzania

sugu for presidency 2015, vijana tunampa..hiki ni kizazi cha bongo flava
 
Mkuu samahani kwa maswali haya.kama Lowassa ahakuwa muhusika wa Richmond kwanini alikubali kujivua gamba la uwaziri mkuu? Na uzuri wa Lowassa tunauona leo kwasababu anapingana na kikwete?

Hapana mkuu samahani kama post yangu sujaieleza sawa sawa. Lowassa hana usafi wowote, naamini kabisa ameshiriki kwenye Richmond. Lakini ndugu wa karibu wa Lowassa na baadhi ya viongozi wa dini wanaamini Lowassa alitumiwa tu na mkubwa, alijiuzulu ili kumuokoa rafiki yake. Lakini ukweli ni kwamba maovu ya Lowassa na maovu ya JK ni hayo hayo, wote walikua pamoja, walifahamishana na walipeana go ahead/support. Lakini JK anataka kujionyesha safi kwa watanzania hasa wanachama wake, kwahiyo ni lazima ahakikishe RACHEL wanaondoka kwenye mawazo ya watanzania. Lowassa & grp kukubali kupotea kwenye ramani ni kukubali kosa kwamba yeye ndio gamba kuu la chama wananchi wanaolipigia kelele. Lakini Lowassa makubaliano yake na JK ni kuwa at one point na yeye aje apiganie uraisi na apewe support na JK. JK inawezekana alikua anamkubalia tu kisanii ili aingie Ikulu, au labda amebadilisha mawazo na anamtaka mtu mwingine. JK ni ndumilakuwili so ni vigumu kujua akiwa na Lowassa anamwambia nini, na akiwa na kina Msekwa anawaambia nini. However Lowassa anahaki ya katiba kuomba apendekezwe kupigania uraisi kwanini wanamuita ku-negotiate? Kama wananchi wa CCM wako-serious then hawatampitisha kwenye vikao vyao. Kwanini wasimuondoe tu bila ku-negotiate? Kama mwizi mwizi tu! Unless CCM wanataka kutuambia Lowassa ni fisadi lakini pia bila Lowassa hamna CCM.
 
sasa pinda amefenya nini,kila jambo kwake ye 'linajadilika',bt it was rarely to find ths kind of cowardenc answers kwa lowassa. .delivarance ya huyu mtu si ya kudoubt kabisa wakuu. .narudia,Dr slaa tunamwihitaji tena ver urgent bt lowasa nae tunamhitaji!
Tunamhitaji lowasa kama mfano wa kujifunza uongozi mbaya ni nini,hasara za huyu bwana kwa nchi hii ambazo amezisabisha akiwa kama kiongozi mwenye dhamana ni kubwa sana na zitaendelea kubaki kwa miaka mingi ijayo.na moja ya hasara kubwa pamoja na madudu yake yote bado kwa namna fulani kafanikiwa kukamata fahamu za wapambanaji na wanamadiliko kwamba aweza faa kuwa rais wa tz.enyi watz nani aliyewaroga? Lowasa kwa nchi kama china tungebakiwa na kumbukumbu yale nzuri sana ambayo ingesababisha watu waogope kuchezea ofis za umma wanapopewa dhamana ya kuzitumikia.EL haijalishi kafanya nini kwa urais wa tz hafai kabisa,kimsingi hatakiwi hata kuonglewa.
 
Hapana mkuu samahani kama post yangu sujaieleza sawa sawa. Lowassa hana usafi wowote, naamini kabisa ameshiriki kwenye Richmond. Lakini ndugu wa karibu wa Lowassa na baadhi ya viongozi wa dini wanaamini Lowassa alitumiwa tu na mkubwa, alijiuzulu ili kumuokoa rafiki yake. Lakini ukweli ni kwamba maovu ya Lowassa na maovu ya JK ni hayo hayo, wote walikua pamoja, walifahamishana na walipeana go ahead/support. Lakini JK anataka kujionyesha safi kwa watanzania hasa wanachama wake, kwahiyo ni lazima ahakikishe RACHEL wanaondoka kwenye mawazo ya watanzania. Lowassa & grp kukubali kupotea kwenye ramani ni kukubali kosa kwamba yeye ndio gamba kuu la chama wananchi wanaolipigia kelele. Lakini Lowassa makubaliano yake na JK ni kuwa at one point na yeye aje apiganie uraisi na apewe support na JK. JK inawezekana alikua anamkubalia tu kisanii ili aingie Ikulu, au labda amebadilisha mawazo na anamtaka mtu mwingine. JK ni ndumilakuwili so ni vigumu kujua akiwa na Lowassa anamwambia nini, na akiwa na kina Msekwa anawaambia nini. However Lowassa anahaki ya katiba kuomba apendekezwe kupigania uraisi kwanini wanamuita ku-negotiate? Kama wananchi wa CCM wako-serious then hawatampitisha kwenye vikao vyao. Kwanini wasimuondoe tu bila ku-negotiate? Kama mwizi mwizi tu! Unless CCM wanataka kutuambia Lowassa ni fisadi lakini pia bila Lowassa hamna CCM.

"Nimesikitishwa sana,, nimedhalilishwa sana, nimeonewa sana katika hili! Mnahutubia nchi nzima, kuwa waziri mkuu amefanya hivi, kuwa waziri mkuu amefanya hivi, bila kumsikiliza, mi nadhani there is a wish, the wish am going to grant, ni uwaziri mkuu. Nadhani tatizo ni uwaziri mkuu. Nimetafakkari sana, kwa niaba ya CHAMA CHANGU, KWA NIABA YA SERIKALI YANGU nimeamua kumuandikia rais barua ya kumuomba niachie ngazi"

Haya ni maneno ya kiongozi mkuu EL alivyokuwa anajiuzuru, tukamuona shujaa, mzalendo na muajibikaji. Lakini kama kawaida ya viongozi wa africa, anachokiongea mdomoni na anachofikiria moyoni ni tofauti, hilo ndilo lililomfikisha hapo alipo, ni mnafiki, angebaki kama alivyoongea siku ile, jamaa angekuwa na heshima kubwa sana leo. Ila ameruhusu heshima yake ishuke kwa kutojishusha. Ale jeuri yake na vibaraka wake
 
Tunakusubiri kwa hamu kubwa kuliongoza taifa hili 2015

We believe in you don`t let us down


Jesus bless you .
 
From a CCM member.....Hell! naaw!!!,2015 my foot.
 
Tunakusubiri kwa hamu kubwa kuliongoza taifa hili 2015

We believe in you don`t let us down


Jesus bless you .

Kweli ni fighter kama Gadaffi . Tofauti yake na gaddfi ni uwa atleast gaddfi anaubalika na watu kiasii fulani. Lowasa katika mikoa yote labda wilaya yake tu na yenyewe wamuhurumie

He is not a quitter Yes but . kama hata zile mvi hazimsaidii kusoma nyakati basi People powet will quit him as the parliament did
 
Hivi imeandikwa kwenye kitabu gani cha Biblia kuwa Lowassa lazima awe rais wa Tanzania?
 
jamani watanzania wenzangu sasa kuna watu wanataka kutuaminisha kuwa huyu ndiye anafaa kuwa next president kwamba ni mchapa kazi sana,

amini nawaambia huyu hatufai kwani tunataka rais ambaye atatusaidia kurudisha rasilimali zetu zilizoibiwa na zinazoendelea kuibiwa, na pia kuwachukulia hatua wale wote walioshiriki katika kufuja uchumi wa nchi yetu,

sasa huyu akiwa rais itakuwa ni ushindi kwa wezi wote maana kama mwizi mkuu ndio kiongozi, wale wote waliopata na wanaoendelea kuiba watapumua, watanzania tusahau kuhusu EPA, kagoda, meremeta, deep green n.k

kama nyerere alimuona Lowasa hatufai kabla ya madudu ya Richmond? angetuambiaje kuhusu lowasa kama angekuwepo wakati huu amehusika katika richmond,

Lets say no to Lowasa and his wapambe
 
Hivi imeandikwa kwenye kitabu gani cha Biblia kuwa Lowassa lazima awe rais wa Tanzania?

Ndo hapo but for the sake of kuindoa CCM madarakani Lowasa is Good candidate kama uchaguzi wasipo U-KIVIUTU.
 
Back
Top Bottom