Lowassa: Wakimwaga mboga namwaga ugali

Lowassa: Wakimwaga mboga namwaga ugali

Jamani hivi kuna watu wako serious kabisa wanataka Lowasa awe rais wa nchi hii tena 2015 tu? Kweli? Yaani kweli kabisa mnafikiria na mnataka awe rais wa Tanzania?
Inashangaza kwa kweli, maana hivi sasa kuna kundi la watu wameanza kampeni ya kumsafisha Lowasa.
 
Nilidhani Lowasa alibanwa na bunge kwa kuwa alipindisha sheria maksudi ku-chukua chao mapema na nilidhani kumbana ili aachie ngazi ni fundisho kubwa kwa wanasiasa wasitumie vibaya nafasi zao kujitajirisha! Nilidhani akinyimwa madaraka yoyote na ikiwezekana hata haki za waziri mkuu mstaafu apokonywe itasaidia wanasiasa wengine kuacha ufisadi kwa kuogopa matokeo. Haya ya utendaji mzuri wa fisadi yametoka wapi?

Mkapa, Yona nk (wa awamu ya nne), JK, Lowasa, Ridhwan nk (wa awamu ya tano) watajutia lini ufisadi wao endapo hakuna lolote linalotokea dhidi yao? Tumebanwa ili tusiwashtaki kwa namna mbalimbali ikiwemo katika ya 1977 na utashi wa kisiasa hilo linaeleweka. Sasa mnataka hata kwenye kuchagua kwa kura zetu wenyewe tushindwe kuwaadabisha hawa wash..... hawa jamaa?

Nimeamini tanzania tuna laana.

Kama Lowasa angesema hataki urais halafu ukampigia debe ningekuelewa lakini huyu jamaa anautaka urais pengine kuliko alivyokuwa kikwete na matokeo ya wapenda urais mnayajua. Wengi wao wabinafsi sana halafu vilaza wa uongozi.

Sina hakika na wanasiasa wengi hapa nchini lakini namkubali Dr. Slaa kwa kuthubutu kusubiri watu wampendekeze badala ya kuanza na ujanja ujanja kama wa JK na Lowasa. Mara wajipendekeze kwa rost mara waibe epa mara... tabu tupu. Kina mbowe wakiacha watu waamue nani awe Mwkt CDM, nani agombee urais nk tutapata kiongozi imara lakini Lowasa hapana. Mtakuwa hamjamtendea haki, yeye, familia yake na watanzania wote kwa kumfagilia leo wakati alichofanya mnakijua.
 
baa ya tabasam nyingi za kikwete sasa tunamhitaji kiongozi mkorofi na tough kwelikweli, tanzania inahitaji speed ya kufa na kupona sasa, tumeshaachwa na dunia nzima, sasa tumwombee Mh Edward Lowassa au Mh Wilbrod Slaa, hawa ndio wanaweza kuleta maendeleo ya haraka na bila show ovyo, tunahitaji viongozi hawa waliokaa kama Kibaki na Odinga ambao sijawahi kuwaona wakicheka, na ni bora tuwaogope mpaka aingie Lowassa au Slaa, tusidhubutu kumchukua kikwete mwingine mcheshi


Mkorofi i anayefaa kurudi Ni Ben Mkapa yeye pamoja na sha zake zote walau taifa litaokoa japo Pension yake if CCM might make it. in 2015.

Lowasa sio tough kama watu wanataka kujiaminisha ni usanii wa kuficha ufisadi wake. anakromea DC kwa hotuba mbovu kufurahisha watu na kupata attention ya public but nyuma ya pazia anayofanya yeye ni worse zaidi ya wale ma DC aliokuwa anawakoromea. Taifa haliitaji msanii kama Lowasa.
 
sasa ya nin kua na wazir ama rais mvivu,ebu acheni kua watumwa wa usafi,dunia hii haina mwema,ama msafi,and curently there is no such a trustworth leaders,big deal here,is lowasa ni jasiri,mbunifu,mchapa kazi. .and anajua kua kucha kusiche atakua raisi,anachofanya ni kuitunza afya yake!
 
jiulize wewe, mtu muovu anajiuzulu? hapana anaogopa kushitakiwa, la sivyo kina Nahodha na Mwinyi mdogo, Ngeleja wangejiuzulu, nae kikwete angejiuzulu, sasa lowassa amejiuzulu kuwapeni nafasi mumchunguze kama ameiba, mbona ridhiwani na babake hawafanyi? Lowassa ni Msafi na ndio nyundo pekee ya kuokoa nchi hii, kumbuka hata mwinyi mkubwa aliwahi kustaafu uwaziri baada ya kupata skendo kama ajali hiyo ya lowassa, je urais hajaupata?

Ndugu, Aristotle once said "Do not make assumptions, not every situation is similar".

Mazingira ya kujiuzulu Mwinyi na Lowasa ni tofauti kwa hiyo tusiwafananishe. Kwenye saga ya Richmond Lowasa, kuna mambo mawili ambayo unaweza kusema, either alikuwa incompetent au aliamua kupindishia sheria na taratibu kwa makusudi. Tusimsifie mtu kwa mambo madogo kama kuwalazimisha watu wajenge shule overnight, tuangalie mambo ya msingi ali-deal nayo vp.
 
Leteni hata mwendawazimu wa mirembe lakini sio wilbroad peter slaa.
 
Huo si utawala wa sheria hata kidogo!
Kama Lowasa, RA na Chenge wana makosa basi makosa yao yawekwe adharani na pia ushahidi uperekwe mahakamani ili wapate haki yao; mahakama ndicho chombo cha kuprove mtu kuwa gilty! Lasivyo wanaonewa kwasababu ambazo Kikwete ndio anazijua mwenyewe.

Mbona Yona na Mramba walishtakiwa kwa makosa yao bila kufukwa chamani! Kama mahakama ita-prove kuwa wao wanamakosa ndipo chama kiwafukuze, hapa CCM iache kiini macho kwa kutaka kubambikiza watu watatu tu uchafu wote wa chama. Hivi katika nchni hii ukiibia taifa adhabu yake ni kufukuzwa katika chama? na Je ni hao watatu tu! kwanini hawapewi nafasi ya kujitetea na kwanini hakuna chombo kinacho tekeleza haki juu yao! wanahukumiwa kwa vigezo gani? mbona hawaperekwi mahakamani kama kweli ni mafisadi?


Arafat, umekaribia kukugusa haswa kuhusu hili suala.

Mikakati na mbinu ya kuwaengua RACHEL (Rostam Aziz, CHenge, Edward Lowassa) kutoka NEC ya CCM kwa vigezo vywa kujivua gamba, kamwe na asilani havina uhusiano wo wote na ufisadi.

Hii ni njia tu ya kujaribu kuwatoa kwenye chombo cha juu cha maamuzi ndani ya CCM. Na ndiyo maana haizungumziwi wao kuvuliwa uanachama au kuvuliwa ubunge. Msisitizo upo tu katika kuwaengua NEC.

Tujiulize kwanini.

Kuna wanaodai kuwa hii ni mvutano kuelekea uchaguzi wa u-Rais 2015, na nani kuwa mgombea wa CCM, na pia kuna wanaodai kuwa hii ni mojawapo ya njia ya CCM kujijenga upya na kurudisha imani kwa wananchi.

Kama lengo ni uchaguzi 2015, basi msukumo huu ndani ya CCM una walakini mkubwa sana. CCM kama chama kitafanya chaguzi zake za ngazi zote mwaka 2012, hiyo ikiwa takribani miaka 3 kabla ya uchaguzi wa 2015. Rostam, Chenge na Lowassa kama ni nuksi au karaha ndani ya CCM, basi CCM ina wakati mzuri tu wa kuwapiga chini 2012 huko NEC na kuondokana na nuksi hiyo.

Kwa nini CC (JK, Mukama, Msekwa, Nape) inatumia nguvu na mabavu kujaribu kuwafanya hawa 'mafisadi' watatu wajiuzulu kabla ya July 2011, wakati CCM hiyo hiyo inaweza kuwapiga chini 2012 bila purukushani?

Hilo CCM wanajua haliwezekani, na ni vigumu kulizuia kwani hawa watatu ndiyo siri ya JK kuwa Magogoni na ndiyo nguvu ya CCM ya kweli ndani ya NEC na Mkutano Mkuu. CC ya CCM haina meno. Meno yako NEC na Mkutano Mkuu, na huko ndiyo RACHEL wamejikita. CC ya CCM ilishindwa hata kumvua uanachama Nape, Bashe au Shibuda (kwa kutaja wachache tu), pamoja na majigambo yote ya "kufungiwa duniani, na hata mbinguni".


Kama suala ni ufisadi, pasi na ushahidi, basi Mramba, Yona, Chenge, Rostam, Manji, Malecela, Mkapa, Mwinyi.... kwa uchache tu hawa wangetakiwa 'kujivua gamba' kwa tuhuma zao za ufisadi (Mramba, Yona - Alex Stewart, Kiwira, Chenge - Rada, Madini, Rostam - Kagoda, Dowans, Manji - Kagoda, Quality Plaza, Ubungo EPZ, Malecela - EPA Jeetu, RITES Chande, Mkapa - ANBEM, Songas, Kiwira, Mwinyi - IPTL, Loliondo, Golden Tulip).

Katika orodha hiyo ukiwaacha Rostam na Chenge, wengine hawatajwi kwa kuwa nia hasa si kupambana na Ufisadi ndani ya CCM (hawa wote ni card-carrying, high profile members wa CCM).

Na ndiyo maana katika orodha za watuhumiwa wakuu wa ufisadi waliyotajwa Mwembeyanga (2006) na Tabora (2011), ni watu wawili tu (Rostam, Chenge) kati ya watu takribani 20 waliotajwa, ambao wanaambiwa wajitoe NEC. Ufisadi haukuwa msamiati wa CCM kwa miaka yote hiyo, na bado si msamiati wao sasa na hata kuelekea mbele.

Kwa hiyo tunarudi pale pale kuwa nia hasa ni kujaribu kuchukua control ya NEC na Mkutano Mkuu kutoka kwa RACHEL, ila sijui control itakwenda wapi, lakini nakuhakikishia siyo kwa JK.


Suala la CCM kujivua ufisadi kupitia kwa RACHEL, lingefanya hata Makinda asiupate u-Spika (na alikuwa mkweli kuwa aliombwa na Rostam kugombea), lakini kinyume na hayo JK mwenyewe alilishikia bango na kuhakikisha kuwa Makinda anaupata u-spika, ije mvua, ije jua. Na akamtuliza Sita na u-waziri mchecheto.


Suala la CCM kujivua ufisadi kupitia RACHEL, lingefanya serikali kukataa kwa dhati kuilipa Dowans Bil 94, lakini kinyume na hayo Werema alisema (akiwa Ikulu), kuwa lazima walipwe, CC ya CCM ikakutana ikulu wakasema lazima walipwe, JK hadi leo hii hajawahi kamwe kusema wasilipwe (kawahi kusema mara nyingi tu kuwa itabidi 'waangalie' badala ya kukimbilia kulipa).


Suala la CCM kujivua ufisadi kupitia RACHEL, lingefanya Ridhiwan (mwana wa mfalme) aepuke kama ukoma kukutana faragha na El-Adawi, wakati huo huo JK akituhumiwa kutumiwa na Rostam na El-Adawi kufanikisha malipo haramu ya Dowans.

Na tukirudi kwenye suala la kurudisha imani kwa wananchi kuhusu CCM, hao RACHEL walipigiwa kura na hao hao wananchi na kupewa ubunge kwa zaidi ya asilimia 90 katika majimbo yao, wakati JK alipata pungufu ya asilimia hizo katika majimbo hayo hayo. Je, hapo ni nani ambaye wananchi hawana imani naye?


Hili sakata sioni kama litakuwa na mwisho mzuri, na nikirejea kauli ya Lowassa wakati Nape anaanza safari zake za kujitambulisha ni kuwa, je , ili upate umaarufu ndani ya CCM ni lazima uonekane kuwa unapambana na Lowassa? Toka lini mapambano dhidi ya Lowassa imekuwa ni sera za Chama?
 
sasa ya nin kua na wazir ama rais mvivu,ebu acheni kua watumwa wa usafi,dunia hii haina mwema,ama msafi,and curently there is no such a trustworth leaders,big deal here,is lowasa ni jasiri,mbunifu,mchapa kazi. .and anajua kua kucha kusiche atakua raisi,anachofanya ni kuitunza afya yake!
Mkuu tunachosema sisi sio rais au waziri awe mvivu la hasha, tunataka mtu mwadilifu hiyo ni sifa namba moja katika utumishi wa umma, awe mchapakazi Lowasa inawezekana akawa ni mchapakazi kweli mie sina uhakika lakini sio mwadilifu, awe na weledi wa mambo mbalimbali yatakayomrahisishia kuplan nchi iendeje Lowasa ni kilaza uwezo huo hana, ujasiri alionao huyu mheshimiwa ni pamoja na kufisadia mali ya umma, kitendo cha kuacha uwaziri mkuu huo ni ushahidi tosha.

Sijui huyu mheshimiwa alifanya kitu gani hasa ambacho watu mnataka kutuaminisha kwamba anafaa kuwa rais, kwanza chama chake hawamtaki, inabidi ajiaminishe kwanza kwenye chama chake halafu aje kwa wananchi.
 
EL na ungana na ww mwaga mboga wa TZ wafahamu ukweli.manake naona kama hii Boat ina abiria wengi sna watakaozama.......
 
lowassa jembe hata slaa anajua huwa anamzungumzia kwa tahadhari kubwa
 
Arafat, umekaribia kukugusa haswa kuhusu hili suala.

Mikakati na mbinu ya kuwaengua RACHEL (Rostam Aziz, CHenge, Edward Lowassa) kutoka NEC ya CCM kwa vigezo vywa kujivua gamba, kamwe na asilani havina uhusiano wo wote na ufisadi.

Hii ni njia tu ya kujaribu kuwatoa kwenye chombo cha juu cha maamuzi ndani ya CCM. Na ndiyo maana haizungumziwi wao kuvuliwa uanachama au kuvuliwa ubunge. Msisitizo upo tu katika kuwaengua NEC.

Tujiulize kwanini.

Kuna wanaodai kuwa hii ni mvutano kuelekea uchaguzi wa u-Rais 2015, na nani kuwa mgombea wa CCM, na pia kuna wanaodai kuwa hii ni mojawapo ya njia ya CCM kujijenga upya na kurudisha imani kwa wananchi.

Kama lengo ni uchaguzi 2015, basi msukumo huu ndani ya CCM una walakini mkubwa sana. CCM kama chama kitafanya chaguzi zake za ngazi zote mwaka 2012, hiyo ikiwa takribani miaka 3 kabla ya uchaguzi wa 2015. Rostam, Chenge na Lowassa kama ni nuksi au karaha ndani ya CCM, basi CCM ina wakati mzuri tu wa kuwapiga chini 2012 huko NEC na kuondokana na nuksi hiyo.

Kwa nini CC (JK, Mukama, Msekwa, Nape) inatumia nguvu na mabavu kujaribu kuwafanya hawa 'mafisadi' watatu wajiuzulu kabla ya July 2011, wakati CCM hiyo hiyo inaweza kuwapiga chini 2012 bila purukushani?

Hilo CCM wanajua haliwezekani, na ni vigumu kulizuia kwani hawa watatu ndiyo siri ya JK kuwa Magogoni na ndiyo nguvu ya CCM ya kweli ndani ya NEC na Mkutano Mkuu. CC ya CCM haina meno. Meno yako NEC na Mkutano Mkuu, na huko ndiyo RACHEL wamejikita. CC ya CCM ilishindwa hata kumvua uanachama Nape, Bashe au Shibuda (kwa kutaja wachache tu), pamoja na majigambo yote ya "kufungiwa duniani, na hata mbinguni".


Kama suala ni ufisadi, pasi na ushahidi, basi Mramba, Yona, Chenge, Rostam, Manji, Malecela, Mkapa, Mwinyi.... kwa uchache tu hawa wangetakiwa 'kujivua gamba' kwa tuhuma zao za ufisadi (Mramba, Yona - Alex Stewart, Kiwira, Chenge - Rada, Madini, Rostam - Kagoda, Dowans, Manji - Kagoda, Quality Plaza, Ubungo EPZ, Malecela - EPA Jeetu, RITES Chande, Mkapa - ANBEM, Songas, Kiwira, Mwinyi - IPTL, Loliondo, Golden Tulip).

Katika orodha hiyo ukiwaacha Rostam na Chenge, wengine hawatajwi kwa kuwa nia hasa si kupambana na Ufisadi ndani ya CCM (hawa wote ni card-carrying, high profile members wa CCM).

Na ndiyo maana katika orodha za watuhumiwa wakuu wa ufisadi waliyotajwa Mwembeyanga (2006) na Tabora (2011), ni watu wawili tu (Rostam, Chenge) kati ya watu takribani 20 waliotajwa, ambao wanaambiwa wajitoe NEC. Ufisadi haukuwa msamiati wa CCM kwa miaka yote hiyo, na bado si msamiati wao sasa na hata kuelekea mbele.

Kwa hiyo tunarudi pale pale kuwa nia hasa ni kujaribu kuchukua control ya NEC na Mkutano Mkuu kutoka kwa RACHEL, ila sijui control itakwenda wapi, lakini nakuhakikishia siyo kwa JK.


Suala la CCM kujivua ufisadi kupitia kwa RACHEL, lingefanya hata Makinda asiupate u-Spika (na alikuwa mkweli kuwa aliombwa na Rostam kugombea), lakini kinyume na hayo JK mwenyewe alilishikia bango na kuhakikisha kuwa Makinda anaupata u-spika, ije mvua, ije jua. Na akamtuliza Sita na u-waziri mchecheto.


Suala la CCM kujivua ufisadi kupitia RACHEL, lingefanya serikali kukataa kwa dhati kuilipa Dowans Bil 94, lakini kinyume na hayo Werema alisema (akiwa Ikulu), kuwa lazima walipwe, CC ya CCM ikakutana ikulu wakasema lazima walipwe, JK hadi leo hii hajawahi kamwe kusema wasilipwe (kawahi kusema mara nyingi tu kuwa itabidi 'waangalie' badala ya kukimbilia kulipa).


Suala la CCM kujivua ufisadi kupitia RACHEL, lingefanya Ridhiwan (mwana wa mfalme) aepuke kama ukoma kukutana faragha na El-Adawi, wakati huo huo JK akituhumiwa kutumiwa na Rostam na El-Adawi kufanikisha malipo haramu ya Dowans.

Na tukirudi kwenye suala la kurudisha imani kwa wananchi kuhusu CCM, hao RACHEL walipigiwa kura na hao hao wananchi na kupewa ubunge kwa zaidi ya asilimia 90 katika majimbo yao, wakati JK alipata pungufu ya asilimia hizo katika majimbo hayo hayo. Je, hapo ni nani ambaye wananchi hawana imani naye?


Hili sakata sioni kama litakuwa na mwisho mzuri, na nikirejea kauli ya Lowassa wakati Nape anaanza safari zake za kujitambulisha ni kuwa, je , ili upate umaarufu ndani ya CCM ni lazima uonekane kuwa unapambana na Lowassa? Toka lini mapambano dhidi ya Lowassa imekuwa ni sera za Chama?

A well researched contribution! Wenye macho na wasome na kuelewa na wawasimulie wenye masikio.
 
Pharao inatosha babaako msafi umeridhika au unafikiri tunamsingizia tusamehe
 
Lowassa hawezi kamwe kuwa raisi, jiulize ni kwanini alijiuzulu uwaziri mkuu kwanza.

Alijiuzulu ili kumfichia aibu Mzee Mkubwa JK, au hujui mkuu anahusika zaidi kuliko Lowassa, EL ni muungwana na anatufaa sana zaidi ya huyu aliyetutoa hapa na kutupeleka hapa
 
Mmoja kati ya hao akiwa rais, itabidi vijana tuingie msituni! Wote ni mafisadi wasio na maadili na wana agenda ya ukanda!
Haa uingie msituni na nani? Nyie vijana wa Pwani pwani mna matatizo sana, taka usitake Lowassa is the next Prezidaa wa Tanzania. Mbona mnatuogopa sana? 2015 lazima Rais atoke Kaskazini kwanza we are more advanced, more educated and developed unabisha?
 
Msituletee bangi zenu hapa JF.
Kamwe huyu mhuni wa Monduli si wa kumfananisha na Dr.SLAH.
Kuliko Lowassa bora tuendelee na haya maisha ya kutokuwa na rais.
 
Haa uingie msituni na nani? Nyie vijana wa Pwani pwani mna matatizo sana, taka usitake Lowassa is the next Prezidaa wa Tanzania. Mbona mnatuogopa sana? 2015 lazima Rais atoke Kaskazini kwanza we are more advanced, more educated and developed unabisha?
Kweli Lowassa na Slaa walikuwa na wazo moja kuhusu mgogoro wa Arusha, inadhihirisha kuwa ukweli ni wa Chadema, na Lowassa hakusita kuwa upande wa haki.
Uchaguzi ujau naupenda sana Dr Slaa vs Lowassa!!! yeyote tuu.
 
huyo mmasai CCm wamemwita wampe barua ajivue uongozi sasa atagombea kwa chama gani? au inakuja tena CCJII
 
Back
Top Bottom