Lily Flower
JF-Expert Member
- Oct 16, 2009
- 2,553
- 1,197
Hii movie itakuwa ya mwaka ngoja nikae standby.
hawezi mwaga chochote.......anajua nini anafanya.........muulizeni walipokutana na jk siku ile kule zenji jk alimwambia nini katika yale mazungumzo yao?.........
jk ni ndumilakuwili sana na bonge la nafiki lile.........
mwisho wa ccm ni kumalizana wenyewe kwa wenyewe
Ee Mola endelea kunipa uhai ili niweze kuona madudu zaidi yaliyofanyika kumwingiza JK madarakani...Niweze kuona mwisho wa unafiki wa JK...Niweze kuona mihtasari ya mikutano ya siri iliyoongozwa na EL kupanga njama za kukwapua fedha za EPA ili JK aingie madarakani..Niweze kuona CCM ikimeguka mapande matatu..Niweze kupata ukweli wa chanzo cha chuki ya JK kwa Cigwiyemisi, Mkapa na Dr Salim..Niweze kupata ukweli kuhusu uhusiano wa JK, RA na Kagoda..........Aaamin!
Vigogo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wanaotakiwa wajiuzulu kwa tuhuma za ufisadi wamekutana na uongozi wa juu wa chama chao, na taarifa zinasema bado mvutano haujaisha kati ya pande mbili hizo. Taarifa za hakika zimeliarifu Raia mwema kwamba walikutana na makamu Mwenyekiti, Pius Msekwa, wiki iliyopita, na kwamba mmoja wao, Edward Lowassa, Bado ana donge.
Habari zinaeleza kwamba Lowassa (Mbunge wa Monduli), Rostam Aziz(Mbunge wa Igunga) na Andrew Chenge (Mbunge wa Bariadi magharibi) waliitwa ofisi ndogo ya CCM, Lumumba Dar es Salaam wakitakiwa kutekeleza uamuzi wa NEC.
Lakini habari kutoka kwa watu wa karibu na Lowassa zinaeleza kwamba mwanasiasa huyo amebainisha kwamba hakubaliani na uamuzi wa NEC. Mzee (Lowassa) amesema kwamba aliitwa na kwamba alitakiwa kuachana na suala la urais ili mambo yaishe, lakini amewaambia uamuzi wowote kisiasa ni haki yake kikatiba, na hivyo hakubaliani nao anasema Mbunge mmoja ambaye yuko katika kambi ya Lowassa akiongeza: Ila wajue kwamba wao wakimwaga mboga sisi tunamwaga ugali. Kwa mujibu wa Mbunge huyo, Rostam Aziz na Chenge wanaonekana kulegeza kamba katika suala hilo.
Anasema mbunge huyo Rostam amesema wazi kwamba hawezi kushindana na Rais aliye madarakani hata kama watakuwa wameonewa. Chenge anakubali tu kwasababu anaona hana jinsi. Lowassa bado moyo wake ni mzito .Gazeti lilipotaka Lowassa alizungumzie suala hilo alijibu No coment, No coment, No coment
Taarifa ambazo Raia mwema limezipata zinaeleza kuwa tayari viongozi hao ambao wote ni wajumbe wa NEC na walihudhuria kikao kilichoazimia wajiuzuru, wameshakabidhiwa barua rasmi za kuwataka wajiuzuru zikirejea uamuzi wa vikao vya juu vya CCM.
Source: Raia Mwema June1-June7, 2011
Jamani mbona mtandaoni bado hawajaweka toleo (June1-June7) hili?? msaada tuna hamu na hizi habari nzuri zenye dalili za kukiangamiza chama cha magamba
Mimi nadhani Lowassa kama Mwanasiasa mkongwe alitakiwa a-step down tu, kwasababu system haimtaki tena kwasababu kaichafua. sasa akimwaga ugali yeye itamsaidia nini? afanye kitu ambacho kitamfanya arudishe heshma yake na siyo kuwa na "moyo wa tukose wote"
Yanayo mkuta Kikwete ni kwamba anaandamwa kwasababu ya didi yake, yanayomkuta Lowasa ni haki yake lazima asurubiwe.
yanayo mkuta kikwete ni kwamba anaandamwa kwasababu ya dini yake, yanayomkuta lowasa ni haki yake lazima asurubiwe.
mwisho wa ccm ni kumalizana wenyewe kwa wenyewe
Eddy usikubali kabisa, yaani wewe na RA muuibe mihela yote ili badala ya kutumia na familia zenu hela mkazipeleka CCM ili JK apange pale Magogoni leo yuko pale anawabadilikia, hata msikubali kama noma na iwe noma kama jela wote muende huo ndio uana ume kama alivyokusifia SS kuwa wewe ni mwanaume wa shoka, onyesha ujabali wako.