Lowassa: Wakimwaga mboga namwaga ugali

Lowassa: Wakimwaga mboga namwaga ugali

Kampeni za kumsafishia njia zimeanza mapema, sidhani kama atafanikiwa...
 
Kweli kabisa kuna kundi kubwa la wapambe wanafanya kila njia kumsafisha na kumuandalia njia ya urais 2015. Naona huyu jamaa hafai, licha ya kashfa zote zinazomkabili kwa nini anautaka urais?? Kuna kitu nyuma ya pazia, inabidi tuwe makini!!
 
Mimi nadhani Lowassa kama Mwanasiasa mkongwe alitakiwa a-step down tu, kwasababu system haimtaki tena kwasababu kaichafua. sasa akimwaga ugali yeye itamsaidia nini? afanye kitu ambacho kitamfanya arudishe heshma yake na siyo kuwa na "moyo wa tukose wote"
Hivi nani anayejua kuwa Lowassa alifisadi nini? Samuel Sita kwa kujua EL atakuwa kikwazo kwake kwenye ndoto za kuwa PM au president kwa kushirikiana na Mwakyembe walimsaidia JK bila kujua kumtema EL. Ninasikia maneno meeengi kuhusu EL but hakuna hata mmoja anayesema kafisadi nini. Hakuna ushahidi wa wazi kuhusu rushwa aliyochukua kwenye Richmond. I swear to god bora Lowassa kuliko Hussein Mwinyi anayeandaliwa na JK. Lowassa is the best leader by far. And he has class and he is rich. That is kind of president we want. Halafu ni mcha Mungu
 
Safari njema Lowasa, sijui utatoka na chama kipi maana kwa magamba hufai na cdm ndio kabisaa
 
Mheshimiwa Lowasa hawa watu wasijione wao ndiyo walioshika mpini midhali una uhakika wewe una mboga na wao wamedhamiria kumwaga ugali, mwaga sisi huku tunatamani kweli kuviona. Please do
 
Kweli ni fighter kama Gadaffi . Tofauti yake na gaddfi ni uwa atleast gaddfi anaubalika na watu kiasii fulani. Lowasa katika mikoa yote labda wilaya yake tu na yenyewe wamuhurumie

He is not a quitter Yes but . kama hata zile mvi hazimsaidii kusoma nyakati basi People powet will quit him as the parliament did

umetumwa na samweli sitta aliyeifisadi cda dodoma.!
 
Hata wanaosema 'Olaigwanani' Lowassa anataka Urais nao pia niwapambe!Mbona yeye anayetajwa Kuutaka Urais Hajawahi Tangaza! Anautaka Urais 2015?
Kumsemea mtu nako ndio Upambe
Isitoshe Kugembea ni Haki ya Mtu yoyote ila Mwamuzi wa Nanai awe Rais ni Wa Watanzania Watakao jaaliwa Kuiona hiyo 2015 naukjitokeza siku hiyo!
 
Wala msihangaike naye huyo... JK atamchinjia baharini watu wasione mwili wala kiwiliwili chake come 2015. Yeye badala atulie ale mihela yake, anataka kushindana na mkuu wa nchi, wakati ana mikashfa kibao.... Mwacheni aingize jina aone kitachomtokea. Na kama umafia wa kimtandao, JK ndio master wa mbinu za mtandao. Hayo yaliwezekana kwa Ben Mkapa tu, kumzunguka kupitia kwa Apson, na Kingunge... Kwamba eti watamzunguka JK ili baadae ajione yupo pekeyake awasusie nchi, subutuuu!... Jamaa anamu underestimate sana JK... Pamoja na mapungufu yote ya JK lakini usije kumchezea kwenye POWER!... Na Lowassa anajua alichotaka kufanya ambacho kimetrigger all this fuss.
 
Inashangaza kwa kweli, maana hivi sasa kuna kundi la watu wameanza kampeni ya kumsafisha Lowasa.

Wote wanaomsafisha jambazi lowassa JF wako kwenye pay roll.Hii trend imenishangaza kweli
 
lowassa hasafishiki period!!!!!kwani itakuwa mtaji mzuri sna kwa wapinzani 2015.mwenyewe analijua hilo
 
mweheshimiwa wangu mwaga watu wasikupe mzigo wewe mwenyewe wakati mlikula wote,tena jamaa anayekuandama mimi namjua ni ni ni ni si nyembe! kisa uraisi 2015
 
Hapo ni patamu kweli Piganeni wenyewe mturahisishie kazi CDM tunasonga mbele zaidi unadhani Magamba masihara?😛ound:😛ound:😛ound:
 
Ee Mola endelea kunipa uhai ili niweze kuona madudu zaidi yaliyofanyika kumwingiza JK madarakani...Niweze kuona mwisho wa unafiki wa JK...Niweze kuona mihtasari ya mikutano ya siri iliyoongozwa na EL kupanga njama za kukwapua fedha za EPA ili JK aingie madarakani..Niweze kuona CCM ikimeguka mapande matatu..Niweze kupata ukweli wa chanzo cha chuki ya JK kwa Cigwiyemisi, Mkapa na Dr Salim..Niweze kupata ukweli kuhusu uhusiano wa JK, RA na Kagoda..........Aaamin!
Chenge na Rostam wanaogopa nini? wamwage tu ugali tumechoka na unafiki wa JMK, ****** aliyeshindwa kuongoza nchi. NAMUOMBA LOWASSA AFANYE HARAKA KUMWAGA UGALI ILI TURUDIE UCHAGUZI KWA SABABU JK NI MAAFA MAKUBWA KWA TAIFA AKIACHIWA AFIKE 2015. FICHUA MLIVYOSHIRIKI EPA, KAGODA, MEREREMETA, DEEP GREEN, RICHMEOND ILI WANANCHI TUANDAMANE KAMA YEMEN KUMUONDOA HUYU JAMAA. WOTE HAWANA MORAL AUTHORITY YA KUTUONGOZA. HII NCHI KILA KONA NI RUSHWA NA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA WALIPA KODI.

ALSO, FOR THIS SAGA TO BE A JUBILANT THROW AWAY SITTA, MWAKYEMBE, NAPE AND MWAMBALASA. GET RID OF THESE CALIBERS TO MAKE CAHAMA CHA MAGAMBA DIE A GOOD DEATH.
Hee Mungu nijalie uhai ili nishuhudie kifo cha chama cha magamba.
 
Si wakigawe tu chama hicho wawe na CCM asili na CCM mtandao. Kwanini kila mmoja anakomaa na CCM ya Nyerere
 
Nyie mnao msafisha Lowasa wala hamumtendei haki, kama hela yake mnakula halafu hamumuelezi ukweli kuwa hizo juhudi mnazofanya ndiyo zinazidi kumharibia. Mnajua kuwa kuna watu tulishamsahau huyu nyang'au lakini hizi kelele zenu ndiyo zinatukumbusha machungu ya ufisadi wake kwa watanzania.Hilo la kumwaga mboga nakubaliana naye kwani wote ni wezi sasa kama wamedhulumiana basi wauane wenyewe, kwani mahali wanapostahili hawa vibaka ni jela tu. Nawachukia sana nyie mnao mfagilia kuwa anafaa kuwa rais labda kama mnafikiri kwa matumbo yenu badala ya akili.
 
Kumekucha. Nakaa mkao wa kula ili kuona mechi. Nasubiri kupewa kiingilio. Mechi itakuwa kali sana. ila Mwalimu aliwahi kusema chama imara kitatoka ndani ya CCM

Kumbe mwalimu nae alikuwa ni kama Sheikh Yahaya....hebu natuone.
 
Kumbe hii thread inamuogesha Lowasa kuwa mgombea wa Rais! Chama gani? maana CCM hamtaki au atafufuwa CCM?
 
Back
Top Bottom