Lowassa, Rostam sasa kuwasha moto

Lowassa, Rostam sasa kuwasha moto

hahaha!
chenge-JOSEE MARA MUTOTO YA KIMARA

rostitamu-HAMZA KALALA JUNIOR

eddo-KHALEED CHOKORAA
 
Mwacheni Mwalimu aitwe Mwalimu. Naona yule mzee alipozungumzia suala la ubaguzi watu wengi hawakumwelewa. CCM wanawabagua CHADEMA kwa kusema wao chadema sisi CCM. Wamemaliza hapo, wamegundua ala kumbe kumbe tuna magamba. Watavua magamba yote na mwisho wa siku watagundua kuwa wana UPELE. Sasa hapo ndo ngoma itakapokuwa inogile. Jamani kutoa upele kazi sana, hiyo nadhani mpaka m/kiti atalia
 
Picha hizi ni ushahidi mzuri sana kuwa Kikwete ni mnafiki sana.

Nasikia wakati wa kampeni za uchaguzi 2010 hukuo Rombo, Kikwete alisema mtuhumiwa anabaki hana hatia mpaka ithibitishwe vingnevyo na mahakama. Akimaanisha Mramba ni shoka la zamani lenye haki sawa kupata ridhaa ya kuongoza jimbo hilo. Fast foward miezi minne baadaye kwa nini huyu mnafiki asiwe na consitency?

Sasa basi ni wajibu na dhamana yake sasa kutoa ushahidi hadharani wa hao pacha watatu. Lazima Kikwete na CCM (maana ndio waliowapitisha hao kwa majimbo yao) wawajibishwe sawa sawa. Chadema walishasema zamani hao ni mafisadi, wananchi walijua kitambo hao ni mafisadi lakini Kikwete alisimama mbele kuwatetea. Naamini alijua wazi kuwa hao na mafisadi. Huo ni ubadhirifu wa fedha na rasilimali ya umma, kwani hiyyo gharama ya kurudia uchaguzi katika majiombo hayo inapaswa ilipwe na Kikwete na CCM. Ni usanii. Ni ushenzi wa hali ya juu.

Mwisho, hili igiz/filamu ni ya kustaajabisha kwa mengi. Kwani kiuhalisia Kikwete ni mtuhumiwa mkuu namba moja wa ufisadi. Jiulize mwisho wake ukoje!
 
Chama Cha Misukule hicho hakuna haja ya kuhangaika nao....watamalizana karibuni maana wote ni misukule tu haina akili hiyo!
 
mimi niliuliza mwaka 2005 kuwa tunampa nchi mkwereeeee???????ndiyo faida yake sasa hii.hawa watu wanaotoka mikoa ya pwani ni watu wa masihara masihara.si watu makini.huyu bwna sijui alifikaje chuo kikuu.uwezo wake wa kufikiri ni sawa na kijana wa form 4 mwenye division 3 labda.
 
I say thanks for this useful post, sijui prezidaa alikuwa anafikiri nini hapo, hii ni kuwafanya watanzania wajinga wasio na uwezo wa kifikiri, ni bora hata jk angeacha wakajipigia kampeni wenyewe, sidhani kama wangeshindwa bila kikwete, pili kwani jk aliwapigia kampeni wagombea wote wa ccm, sasa kwa nini hawa. This was a big mis-calculation.
Na asiye na dhambi na awe wa kwanza kumpiga jiwe, Yesu akatazama chini na kuandika ardhini alipoinua macho wakawa wameondoka wote, nasema, JK umejipalia makaa, ndugu yangu, unawatosa watatu, wakati kunawengi, umeshau aliyekuwa MP wwa Rombo? hukumtosa, unajua ufisadi unaofanywa Maliasili umeamua vp?

Unajua nini kunaendelea TRA, bandarini, viwanja vya ndege, mipakani umechukua juhudi gani? hawa ni wa bunge watatu, je unadhani ndiyo mianya pekee inayosababisha ufisadi kukua? Unakumbuka Azimio la Arusha sababu yake kuu nini? Siyo ufisadi? japo wengine tulikuwa bado au wadogo sn, lkn hatua ya Moringe sokoine kukomaa na mafisadi kuanzia wahindi mpaka wafanya kazi wa serikali ndiyo ulikuwa msingi pekee wakuiponya nchi, lkn hii hatua ni kuosha kikombe nje ndani kuna mende japo niwadogo lkn maji hayanyweki.

Hakika nasema akina kabwela walala hoi tunakuambia kuwa ukitaka kuiponya nchi jukumu kubwa nikuwafilisi watendaji wakuu waserikali ambao unadhani au unauhakika na uporaji wamaliasili za nchi, nadhani siku hizi usalama wa taifa wamekuwa si watunza siri, hata ukiwatuma kwenye viwanja vya ndege kuwa wafanya kazi badala yake wataanza kufanya ufisadi.

Mawaziri husika hawafanyi kushtukiza kukagua utendaji wa mipaka yetu, nakumbuka kufanyiwa rusha hapo nyerere airport, lkn leo ukisema unageukiwa wewe, ndug, dhambi hii japo umesema kwa kuponya kidonda cha kujikwaa kisiasa km ulipomwambia EL, unasababisha jipu ambalo kweli kupona kwake ni kulitumbua kwa kisu na usaha ukitoka watu wote watasema haaa! kumbe ccm wako hivi!

Laiti ungesema yaliyopita si ndwele wa TZ kwaniaba ya wote tunaomba msamaha, halafu huko chinichini uchukuwe hatua ya kumwaga mboga, wao wangekula ugali bila kujua mboga inakuja hau imemwagwa, lkn unasema namwaga, wao wanasema cc ugali hatuli tunamwaga, wote mnalala njaa, ccm siyo mama, siyo baba, wakijitoa nakusema wakotayari kuwaomba msamaha wa TZ na wakakubaliwa wakirudi ulingoni kivinge, ww utakuwa unajipumnzisha ndipo watakuambia ukakalale lupango kwani hukusema ukweli kuhusu mali zako, nasema ukimaliza muhula wako ck zinaendelea, nakusikitikia hukuona mbali, utajiamaliza mwenyewe, hawa watuwakitubu nakurudisha mali walizochukua nakuomba msamaha kwa wanachi je utasmeaje?

Amani ya kweli huja kwa kusameheana nakuomba yalopita yasirudiwe, na utendaji wa serikali uboreshwe.
 
Waache waipige mkwara ccm maana jana nimesoma tazama tanzania wanasema kuwa ugomvi wa lowassa na jk ni kama wa kambona na nyerere au wa jenerali na mkapa kweli hiyooo!!!
 
Nilipe Ng'ombe wangu....! Puta na mimi nipute...! Thubutu!!!!! Niguse uone!!!
Tusubiri Suparing Ngumi za Majeba!!!!
 
Duduwasha,

Hiki Mami ni Kinyamwezi na si Kiswahili na naona umefanya direct translation tu hahahahaaa 🙂

Umenirudisha utotoni wakati watu wanachonganisha wenzao wazipige " ....Nnepile ng'ombe zyane." Hahahaa ...

Safi sana. Kuna ile ya kuchora mstari na ukiuvuka tu...... au sema Zuu!!!!
Nilipe Ng'ombe wangu....! Puta na mimi nipute...! Thubutu!!!!! Niguse uone!!!
Tusubiri Suparing Ngumi za Majeba!!!!
 
Hatma ya CCM imefika ukingoni, kwa hatua ya kuwavua EL, AC & RA ni sawa na laana kwa chama. JK katu hatoweza kuitawala nchi hii na atapata laana kali ya muumba toka kwa watanzania wote (waislamu & wakristo), nayasema haya kwani ni jambo ambalo...WAMEKUWA PAMOJA, WAMEPANGA MIPANGO PAMOJA, WAMEFAULU PAMOJA, WAMEINGIA IKULU PAMOJA leo hii uwashushie dhambi kama hii wao tu?

Ni uonevu usio kifani, mkuu wa nchi anapaswa kutazama mara mbili hayo aliyoongoza NEC kuamua kwani hata (hao watatu) wakipotezwa bado laana itaendelea kuwepo.

MY TAKE:

Ilipaswa wote wajiuzulu kuanzia mkuu wa nchi ambapo makamu wake ashike hatamu...NDIPO SALAMA ITAKUWEPO.

Mola hawezi kuwaacha viumbe wake waliokuwa pamoja na sasa wanadhulumiana ilhali walisaidiana wakiwa ni 'boyz 2 men', kwa sasa kuwatupa tena kwa kashfa nzito shauri ya fahari hizi fupi za dunia ni uonevu na kukithiri kwa kupokea majungu toka kwa wapambe,, HAPANA;JK ANAPASWA AJITAZAME NA ATAZAME HATMA YAKE IKOJE, atakuwa hatarini abadan.
TOBAAA, Hivi wewe unamshirikisha mungu kusaidia MAFISADIII, Umechanganyikiwa mwenzetu wewe tafuta mtu akuzinguwe
 
..ukimwaga ugali nami namwaga mboga, sisi ngoja tukae pembeni tuangalie chezo zima linavyochezwa

halafu hao wabunge wa ccm,mwenyekiti, spika na wengine ni vilaza wa ajabu.. sasa kama EL alikua anajulikana hata ndani ya chama kama fisadi? walimpigiaje kura ya kuwa mwenyekiti kamati ya mambo ya nje na usalama?
 
Wakirudisha kadi za CCM-Original wataenda CUF au NCCR-mageuzi(CCM-B), hakuna jipya hapo lao moja wanatuzuga tu.
 
Mambo baaaado!!!, fungukeni "mapacha watatu" tupate uhondo sie, tumeshategesha satelites tunasubiri kunasa mambo.
Mhh TZ!!! toka boyz 2 men mpaka mapacha watatu!!!!
 
..ukimwaga ugali nami namwaga mboga, sisi ngoja tukae pembeni tuangalie chezo zima linavyochezwa

halafu hao wabunge wa ccm,mwenyekiti, spika na wengine ni vilaza wa ajabu.. sasa kama EL alikua anajulikana hata ndani ya chama kama fisadi? walimpigiaje kura ya kuwa mwenyekiti kamati ya mambo ya nje na usalama?

Sasa wewe umesahau mnene mwenyewe alimshika mkono akasema huyu saaaafiiiiiii!!!! leo imegeuka imekua chafuuuu!!!
 
Huu ni kama mchezo wa kuigiza,hawa mapacha watatu ndiyo waliobeba siri zote za chama ufisadi wote waliofanya ni kwa ajili ya chama kupata fedha za kuendesha uchaguzi kuimarisha chama n.k,hawa wakiondoka tu na CCM ndiyo mwisho wake tena utakuwa mbaya sana,kwani wana watu wengi sana walio nyuma yao,na uwezo mkubwa sana wa kujieleza.siamini kabisa kuwa CCM wana nia ya dhati kuwaondoa ila wanatumia majina yao kujisafisa tu.LAKINI HAGUSWI MTU ITAKIGHARIMU CHAMA KULIKO KAWAIDA.:A S 465::A S 465:INATISHA VIBAYA.
 
Tuwapokee tu Chadema naona wanasingiziwa! Lowassa atakua mgombea wa Urais Kupitia Chadema!
 
kwa Anaeweza kuconnect the dots ni kwamba kwenye siasa hakuna adui wa kudumu, hawa mapacha watatu wakiamuwa kwa dhati kwamba anaemwaga mboga wao watamwaga ugali, ni kwamba serikali nzima ya ccm haitobaki salama, kwanza kwenye list of shame mtuhumiwa namba moja ni JK, na kuna kashfa hiyo aliosaini mkataba wa madini akiwa kwenye wizara husika, na bomu la nyuklia ni EPA, maana EPA ndio iliyomweka madarakani JK. hii ni zaidi ya movie za hollywood. watch it very closely.
Chadema hapa watapata mtaji mwingine wa dezo Rostam na Lowasa mwishowe wataamuwa kuwakabidhi CHADEMA document zote za wizi wa kimfumo ambao si kikwete wala nani atakaetoka salama kwenye mtego huo na katika movie hii starling ni Dr Slaa, ndio maana wanasema Dr Slaa anatetea mafisadi," kichekesho" leo hii muhasisi wa vita ya mafisadi eti anatuhumiwa kuwatetea mafisadi! hii si kweli, wanachokiogopa hapa Hawa magamba kinyesi ni Lowasa na Rostam wasije wakasurrender all criminal evidence kwa Dr Slaa. kwani huo ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa serikali hii kinajimu, na tutaingia kwenye uchaguzi mpya kabla hata ya 2015.
 
Back
Top Bottom