BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,032
- 3,944
to his wife, maybe.
...Nimeipenda Hii. Thanks Jerusalem!...and JF!:clap2:
to his wife, maybe.
fataki data zako ni za kifataki. They are not true. Hata ulivyoandika tu bado umechakachua. Kama kitu hujui usiandike
mimi siungi mkono ufisadi bali pia siungi mkono uchafuzi kwa kutumia uongo
tunaomba data kwamba lowassa kachukua shs ngapi na wapi
tumesoma akina chenge na rada, akina manji na kagoda, akina ra na deep green
hebu tuache unafiki tuseme kile ambacho mtu amechukua na tuwe na records kama zingine vinginevyo tunapiga kelele ambazo hata kwa mwananchi wa kawaida huwezi kumwambia huyu mtu mbaya.
Watu wote waliochukuwa fedha za umma wameandikwa sana na wote sasa hivi wala hatuwasemi kila siku tunapoteza muda kwa lowassa
kama vipi huyu mtu tumpotezee lakini siyo kwa maneno ya giliba yasiyo ya kweli maana kwa hilo hakika twatenda dhambi sisi weneyewe na itaendelea kututafuna
huyu mzee mnamwekea maneno mdomoni kila siku, kwanini hayo makombora mliyonayo msiyaweka tuyatoe wakati ukifika akisema anataka urais
kwani kama yeye ni mbaya na ccm ikamsimamisha si ndiyo vizuri kwa chadema, cuf au nccr mageuzi ili tuinyang'anye ccm hati miliki ya utawala wa tanzania?
Hebu tuongeleeni tunayotaka kikwete na serikali yake watufanyie sasa watanzania, maana kwa njia moja au nyingine maneno yatamfikia tu, watu wake wa tiss ambao wamo humu ndani watamfikishia na itatusaidia!!
Siyo sikio la kufa mkuu. Huyu na wapambe wake ni watu wenye ufinyu wa kujua sentiments za watu na kudhani kwamba utajiri wao haramu utawafikisha kwenye utukufu na ndiyo maana hawaishi kuleta thread za kuchokonoa na kupima upepo humu JF. Ndiyo maana mtu na akili zake anaweza kuibukia humu akidai kwamba Lowassa hana hatia na kwamba alijiuzulu kuiokoa serikali wakati tunajua kwamba hakuwa na hoja za kutetea aliyoyafanya pale mjengoni. Jamaa huyu hajawahi kukutana na changamoto zozote za kupima uwezo wake wa kujieleza au kujenga hoja na ndiyo maana huwa anaogopa kuwakabili hata waandishi wa habari wa ndani na nje zaidi ya wale wa Habari Corporation au magazeti aliyoyanunua kama Tanzania Daima ya akina Kibanda, Katabazi na Mullinda.
naunga mkono hoja,na ndio anayewatia homa CDM,na ndio maana cdm wakilala wakiamka ni lowasa,huyu jamaa akisimama chadema chali coz lowasa anajua siasa za kisasa,ni msomi na ni msikivu na si mropokaji kama padri slaa! sasa wanachofanya cdm ni kumchafua kwa kashfa ambazo hawawezi kuthibitisha,wanabase kwenye rumours only! cdm need to be realistic with people na waambie sera zao na mipango yao,politics of critizing others imeshapitwa na wakati!
UMEKATIWA NGAPI NA HUYU RA?
Nimekuwa nikifuatilia sana vyombo vya habari vinavyopinga Lowassa(Mwanahalisi na Raiamwema) na vinavyo msapoti(Rai na Mtanzania). Nimefuatilia sana wanasiasa wanaompinga na kumsapoti. Mwisho nimebaini kuwa Lowassa ni tishio kubwa kwa wanaoutaka urais wa muungano ndani ya chama chake na kwa upande wa upinzani. Ana nguvu kubwa sana serikalini na katika chama. Ni bingwa wa kuratibu mtandao kisomi. Ni mtendaji na haogopi. Na iwapo ataamua kugombea, hatakuwa na mpinzani mwenye nguvu ndani ya chama chake na hata ktk uchaguzi mkuu. Sote tumeshuhudia jinsi alivyoweza kuukwaa uenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje, ulinzi na usalama bila mtu yeyote kutia mguu kumpinga. Na sasa tumeshuhudia jinsi anavyopata sapoti kutoka kwa Mhe Beatrice Shelukindo na mumewe William Shelukindo. LOWASSA NI TISHIO
Mkuu vipi tena mbona unaingia kimugongo mugongo huku ukitaja majina hovyo hovyo? Mbona unaleta maajabu ya sisimizi kumeza dafu?Nani anaitaka CCM, mafisadi? yes, vitoto vyao vilivyoko uvccm? yes, wapambe wanaokula makombo ya ufisadi kama Anold, Nanu, Salimia, Majimshindo, Nduka,Kaumza, Kashaga, itahwa et al? yeeeeeeeeeees!
Wananchi? HELL NNOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
CCM Mpitisheni Lowasa kugombea urais 2015, wananchi tupate nafasi ya kumhukumu, kumsulubu, kumrudi jambazi, fisadi, nyang'anyi, jangili lililomshinda JK na CCM yake.
nawaonea huruma kambi ya rowasa sababu hata adui yenu hamumfahamu poleni sana! najua mnalipwa pesa nyingi ila mjue adui yenu mkubwa yumo ndani ya ccm VILAZA NINYI!
LOWASSA TISHIO?!
Tusiandike kwa mate wakati wino upo:
1972 - 1973 Milambo High School (combi: Swahili, History na English - SHE) Division III
1975 - 1970 University of Dar es Salaam (B.A. Theatre Arts "Sanaa ya maigizo") Pass
AMA KWELI TISHIO!
Hivi ni lini Watanzania tutakuwa serious..???hivi unaweza kusimama mbela ya jukwaa na kumtetea Lowasa?????????
Najiuliza kwa nini iwe hivyo kwa mtu ambaye amejiuzuru kwa fedheha kiasi hicho! mtu ambaye amekuwa madarakani siku nyingi bila mafanikio kwa nchi tunayoweza kuyakumbuka.
Wale muliouliza ufisadi wake;
1. Hebu tuachane na matendo yake pale AICC
2. Alianza na pesa ya mafuriko ya Tanga.
3. Baadaye akauza viwanja vya mnazi mmoja.
4. Baadaye anasifika kwa Richmond na dowans.
5. Wizara ya maji pia hakupita hivi hivi maana nasikia kila mwezi akaunti yake ilinona kwa kipato toka kwa kila injinia wa maji wa mkoa.
6. Hapo Arusha vipi vioski vya stationery vinavyolazimisha kila mkutano ununue kwake?
7. Hapo Dar kwa wenye mahoteli vipi vurugu za kulazimishwa kupeleka mashuka kwenye laundry zake? Nasikia musipofanya hivyo TRA wanawazonga.
Lazima kama hizo kwa sasa, je, vipi akipewa U-rais itakuwaje? Mbona tutalawitiwa kwa nguvu!
Hitimisho dogo kwangu kwamba anaweza kuwa tishio kwa CCM lakini siyo kwa wa-Tz wote na hasa walio timamu. Tatizo ni mpangilio wa CCM na kamati zake. Hebu angalia viwango vya ufahamu vya wajumbe wa kamati kuu ya CCM. Ni ndogo kiasi kwamba bado mtu kama Kingunge ndo thinkers wao. Enzi hizi za dot com. Engine ya chama huanzia kwa katibu wake, vipi huyo katibu wa CCM? Vijana wanasema kama ni moto, kuni mbichi. Hauwaki hata siku moja.
Sasa waangalie vijana wa CCM. Nani wa kutumainiwa kwa ufahamu wa mambo ya nchi na Dunia? Hao ni vijana wa wakati ambao nchi ina vijana zaidi ya laki moja ktk vyuo vya elimu ya juu. Enzi za mkongo wa mawasiliano ili kila mtu aione dunia nyumbani kwake. Kwa nini hakuna kijana mwelevu huko UVCCM?
Ukisha iona structure kama hiyo huyu mtu hawezi kutoa bilioni mbili wakagoma kutoa support.
Ni Tishio lao huko huko CCM.