Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Labda kama tafsiri yako ya kumsema mtu iko narrow na kufikiria kwamba mtu hawezi kusemwa mpaka atajwe jina. Huyu bwana amekuwa akishutumiwa kwa maneno na parables mbalimbali, labda kwa vile na yeye ana mtizamo marrow kama wewe, kwa kudhani kwa sababu jina lake halitamkwi wazi basi hasemwi, na hii pengine ndiyo inayomfanya hata yeye afikirie kwamba ni kipenzi cha watanzania. Kumbe anachotakiwa kukifahamu ni kwamba kila neno fisadi au mafisadi linapotajwa ametamkwa yeye. Ajue kwamba Fisadi na Lowassa ni synonimous na aelewe kwamba kila wakati linapotamkwa moja basi ajue limetajwa lingine na yote hayo yanafanya reference kwake.
Kwa hiyo ndugu yangu kama ulikuwa na wasiwasi kwamba anaogopwa basi ujue anatajwa sana kuliko mtu yeyote na kama ulikuwa unajipa moyo kwamba anaogopwa basi ujue pia kwamba kutokana na kulichukia sana jina lake basi hata kulitaja watu hawataki. Wameamua kutumia jina lake lingine i.e. FISADI.
We mchokozi sema unachotaka kusema , usiume ume, ebu eleza ulichonacho na wape watu ukweli!
Haya...au unataka tukubembeleze??
au nikusaidie??
unahitimu lini class 7 this year or next yearnimekuwa nkifuatilia kwa makini hoja za wanasiasa wa nchi hii kuanzia chama tawala mpaka vya upinzani nkagundua kuwa wote wanamuogopa lowassa.si mbowe,padri dk slaa ,prof lipumba ,mbatia.hata mwakyembe na sitta.huwa wanazungumzia ufisadi na kuponda watu wengine lakini sijawai sikia wakimsema jamaa hadharani kwanin?
Siyo kwamba hasemwi. Mwenzenu huyu ni sikio la kufa!
Sijui umetumia vigezo gani kujua ulicjhokiandika kwani kwa kumbukumbu zangu kati ya hao uliowataja hakuna anayemuogopa lowasa na wote huwa na wana ujasili wa kuymtaja bila woga..............ila nahisi mafisadi wapo kazini kwa style tofauti
Labda kama tafsiri yako ya kumsema mtu iko narrow na kufikiria kwamba mtu hawezi kusemwa mpaka atajwe jina. Huyu bwana amekuwa akishutumiwa kwa maneno na parables mbalimbali, labda kwa vile na yeye ana mtizamo marrow kama wewe, kwa kudhani kwa sababu jina lake halitamkwi wazi basi hasemwi, na hii pengine ndiyo inayomfanya hata yeye afikirie kwamba ni kipenzi cha watanzania. Kumbe anachotakiwa kukifahamu ni kwamba kila neno fisadi au mafisadi linapotajwa ametamkwa yeye. Ajue kwamba Fisadi na Lowassa ni synonimous na aelewe kwamba kila wakati linapotamkwa moja basi ajue limetajwa lingine na yote hayo yanafanya reference kwake.
Kwa hiyo ndugu yangu kama ulikuwa na wasiwasi kwamba anaogopwa basi ujue anatajwa sana kuliko mtu yeyote na kama ulikuwa unajipa moyo kwamba anaogopwa basi ujue pia kwamba kutokana na kulichukia sana jina lake basi hata kulitaja watu hawataki. Wameamua kutumia jina lake lingine i.e. FISADI.
mh mh si kweli akiongewa fisadi basi ujue ni r.a ndo mwakyembe huwa anamtamka hata kwenye vikao vy a cc
Kwani RA si ni mifuko ya suruali ya Lowassa. Au wewe hujui hilo? kwani utajiri wa RA anautumia wapi kwingine kama siyo kufanikisha safari ya Lowassa? Fungua macho!
Nilijua tu Mbopo aka Mwambene katika thread hii ungekuja kumfurahisha bosi wako anayekutumikisha kazi binafsi za kampeni hadi unasahau majukumu yako kama mtumishi wa umma. Subiri tutakuletea taarifa za fedha alizochukua Membe kwa RA kisha zikakufikia wewe ukazila sijui utafungua kimywa kwa kutumia ID ipi tena.
Baba wenzio hawatumiki kijinga hivi! Tumeshakwambia kwamba kama bifu lako ni Mwambene kuchukua nafasi yako basi utaendelea kupiga kelele na kukasirika sana lakini haitakusaidia, na ndiyo maana tulikushauri uombe nafasi kama hiyo Vodacom au NSSF ambako mkubwa wake na wewe mnachangia siri moja ya kutia aibu sana. Njoo tu na hizo habari zako za kuunga unga na wenye akili zao watajua kwamba huo ni mwendelezo wa chuki zako kwa kitumbua kilichotiwa mchanga na hasira za wakubwa zako kukosa dili la ujenzi wa minara pacha ya ubalozi wa Tanzania kule Nairobi. Kwa kasi sana sasa unawafanya watu wamtoe paka kwenye gunia ili wakujue wewe ni nani na mienendendo yako ya kimaisha. Tutapasua bomu hivi karibuni. Watch this space!
Jamani fungueni macho Lowassa atakuwa Rais na nyote mtafunga midomo yenu. Hii nchi si yenu wana JF ni ya watanzania wote ambao asilimia 80 ni majuha, yaani wanaganga njaa tu. Huwezi kumwambia mtu mwenye njaa usile kama ana njaa na anaitwa kula! Hili ndo taifa leo wana JF, Vungueni macho