Lowassa na Drunken Master Kungfuu style

Lowassa na Drunken Master Kungfuu style

Nyamsusa JB

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2015
Posts
567
Reaction score
1,565
Kwa wale wapenzi wa picha za kichina hususani za Kunfuu mtakua mnaikumbuka ile Style ya Drunken Kunfuu.
Katika hii Style ya Drunken mtu anapigana na adui kwa style ya kilevi, ambapo adui huona anapigana na mtu alielewa sana na dhaifu hivyo huja kichwakichwa akiwa na uhikika wa kushinda kilaini kumbe sivyo kwani Drunken Style iko makini vibaya mno.

Yaani, kama mtu anaanguka vile kumbe ndio anasimama
kama anapepesuka vile kumbe ndio anabalance
kama hakuoni vile kumbe ndio upo kwenye target
kama ana kwepa vile kumbe ndio anashoot
Kama anarudi nyuma vile kumbe ndo anasonga mbele.
kama anajitega vile kumbe ndio anajitegua
kama anatekenya vile kumbe ndio anamenya
kama anahitaji adui mwingine kumbe ndio kafinish mchezo.

Kwa kifupi ni kastyle fulani hivi kanafulaisha sana kukaona ukipenda angalia Move ya Jack Chen "Drunken Master"

Sasa tukirudi kwa Mtaalamu Lowassa anatumia Style hii kwenye Siasa na hapa sasa ndo mtampenda.


Yaani, kama haendi vile kumbe ndio anaondoka.
kama hajibu vile kumbe ndio kaelezea.
kama CCM hawamuogopi vile kumbe ndio full kuufyata.
kama mjinga vile kumbe ndio full Genius.
kama hajuijui vile kumbe ndio full Brain.
kama hapendwipendwi hivi kumbe ndo full mahaba
kama anaanza kuongea vile kumbe ndio kamaliza.

kwa hikika Style ya Kampeni za Lowassa ni kama Drunken Master Kunfuu Style nimeipenda sana.
 
Sio kunfuu.. ni kungfuu...
na pia anachanganya na drunken taichii…
 
Magamba wanachukua tifuz za mbavu tu. Full kukemaa hadi huruma aiseee.
 
Umeweza kueleza uhalisia wa lowassa kwa ufasaha sana dah nililiona iyo ila sikujuwa yote hayo hii inawasumbu magamba kweli kweli walisha zusha Rais lowassa kaanguka kumbe ndio ana ondoka hahaha raha sana
 
Lowasa hajamshambulia mtu ye yote kama wanavyomshambulia yeye.Impact ya mashambulizi inarudi kwa washambuliaji na kuwamaliza kabisa
 
Nimeupenda uandishi wa hadithi wa huyu kamanda Nyamsusa JB. Hii hadithi yako nimeipenda, sinema hii ninaipenda sana na nitafanya upload hap kama kuna mtu anaihitaji. Kwa utangulizi naweka hapa trailer yake, ni very commic but educative and interesting.


<strong>

Starring

Jackie Chan
Yuen Siu-tien
Hwang Jang Lee
Dean Shek


 
Last edited by a moderator:
Wapeeenzi watazamaji picha yetu ya leo inaitwa Operation Mabadiliko iliyochezwa na Edward Lowasa akishirikiana na yule Kamanda machachari Freeman Mbowe, inaletwa kwenu moja kwa moja na yule mtaalamu wenu Luufuufuu Lukomambeija Nakoma Byalelemba Nasika Nakuguta Mkandala,kutoka hapa Mbagala kwa Mangaya.
 
Nimecheka sana baada ya kusoma kipengele hiki; "kama anaanza kuongea vile kumbe ndio kamaliza."
 
haahaahhahahhaaah...yani kama hawaoni wananchi vle kumbe ndo kawatarget...
yani kama kama ananza kutoa speech kumbe ndo kamaliza..hahhaah
 
Back
Top Bottom