kwani kuna tatizo gani EL kuhitaji uongozi wa juu wa taifa letuu?? kama anazo sifa za kutushawishi basi tukimkubalia ni haki yake kidemokrsia. tuache personality katika kujadili hojaaaa...Rushwa ndo msingi wa CCM kututawalaaa sasa kama wachagua watu fulani fulani tuuu kwa hisia zako bado hujengi hoja endelevu...Kwa kweli kama ni kwa nia njema, hakuna ubaya kwa Lowassa kuanzisha TV popote iwe Dar ama Arusha. Lakini jambo moja ambalo lazima tuliangalia kwa makini ni kwamba hawa jamaa wamepania kuchukua nchi. Mind you "kuchukua nchi" na hawatanii, mnataka ama hamtaki. Kilichompata Lowassa na wenzake, wameona ni kutokana na nguvu ya media. Wameamua sasa na mumesikia ama kuona, magazeti kibao yakiongozwa na ununuzi wa New Habari. Wamenunua Channel Ten. Hatua itakayofuata na ambayo mchakato umeanza ni kuwadhibiti wamiliki wa vyombo wanavyoona itakuwa kikwazo kwao ikiwamo IPP Media.
Kwa ufupi ni kwamba kama tukiwa makini kidogo tu tutabaini kwamba, Tanzania yetu inaelekea kubaya. Tunajua kila mtu ana haki ya kutawala, lakini si urithi Mwalimu Nyerere aliotuachia kwamba uongozi ni kwa wenye fedha na vizazi vyao. Nawaambia hata ndugu zangu humu (Nawafahamu) ambao wana nia njema ya kuja kuingia katika siasa kihalali (wakiwamo wanaoshabikia EL kuanzisha TV) wajue kwamba bila fedha (za rushwa) hawatashinda kutokana na mfumo uliojikita na unaoendelea kuimarika vinginevyo wawe vibaraka wa wenye fedha. Hii ni HATARI sana na hapa tukijadili mambo tuangalie huko (2010-2020) maana wenzetu wamejipanga hivyo na kwa gharama zozote zile ikibidi hata za HATARI (nitajadili kwa wakati).
Kama tukitaka, hawatashinda. Tarime wameonyesha hivyo na Busanda wanakaribia kuonyesha hivyo. Inabidi tusonge mbele na Biharamulo MagharibiNiliposema mafisadi watashinda.... sikuwa natania.. sisi wengine ni mabingwa wa kulalamika mno; aidha tuwekeze nguvu zetu kwenye urithi wetu au tuwaache watutawale wapendavyo!
superman
hiyo ni habari njema sana.
Hiyo tv ikitumiwa vema, ni kwa maendeleo ya taifa letu.
I see,Kwa hiyo waanzishe TV, that's fine lakini wafuate maadili ya uandishi wa habari. Wakiendekeza ya New Habari Corporation then hakuna ambaye atafungua channel(s) yao.
Ok, waache wafanye hivyo. Wanaweza kudhani kuwa 'wanatupata' lakini watakuwa wanajiharibia kwa sababu watu siku hizi wameamka. See how their next moves are revealed even before they make themI see,
Watawapata "Ze Komedi" wengine na kuwatumia! Subiri uone. Vipindi vitakuwa merged na Televisheni yenu ya Taifa. Mtaangalia mtake msitake!
Wamejipanga mkuu...
Ok, waache wafanye hivyo. Wanaweza kudhani kuwa 'wanatupata' lakini watakuwa wanajiharibia kwa sababu watu siku hizi wameamka. See how their next moves are revealed even before they make them
Ok, waache wafanye hivyo. Wanaweza kudhani kuwa 'wanatupata' lakini watakuwa wanajiharibia ....
Source:
Daily News, Friday, 24th October 2008, Page 22.
Public Notice
Application for Content Services Licences (Broadcasting Licences) to TCRA.
Name of Station:
ABC Television
P.O. Box 11843
Arusha
Shareholders:
Robert Francis Lowassa (Tanzanian) - 60%
Elias Stephen Kordun Lukumay - 40%
Who is Robert Francis Lowassa and Elias Lukumay?
Source: www.parliament.go.tz/Polis/PAMS/Docs/HS-4-44-2006.pdf
BUNGE LA TANZANIASPIKA: Sina shaka mtakubaliana nami Waheshimiwa Wabunge kwamba, hiyo ni hoja kabambe ya kuahirisha Bunge. Kabla sijawahoji, kuna matangazo mafupi yafuatayo:-
________
MAJADILIANO YA BUNGE
________
MKUTANO WA NNE
Kikao cha Arobaini na Nne Tarehe 16 Agosti, 2006
(Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi)
. . . . . .
Napenda tutambue kuwepo kwa familia ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mama Regina Lowassa, Bwana Fred Lowassa, Bwana Robert Lowassa na Master, kwa hiyo, huyu ndiyo mdogo mdogo tu Richard Lowassa. Wale ambao mmeshiriki vizuri kwenye Bunge na mnahudhuria mara kwa mara, mtakumbuka kwamba, Richard si mgeni sana, hapa kwa sababu mara kwa mara tunaonana naye pale nje, sielewi Mwenyezi Mungu, mambo haya sijui yanakuwaje? Hatujui hatma ya Richard, lakini Mungu aendelee kumsaidia inaelekea anapenda sana Bunge. Pia marafiki zao Bwana John Bakilana na Bwana Elias Lukumai. Karibuni sana na ahsante kwa ushiriki wenu.
. . . . . . . . . . . .
Last week ABC Television waliitwa na Bodi ya TCRA kwa ajili ya Interview ya Kupewa Leseni . . . . .
Habari ndo hiyo . . . . . .
mwizi akikuibia ng'ombe akaenda akamtunza vizuri na hatimaye ng'ombe akawa na ndama, halafu mwizi huyo huyo akaja kukuuzia maziwa na ndama yule wakati unajua ng'ombe mwenyewe alikuwa wa kwako utashukuru kwa ukarimu wake?
majibu yanaelekea kuwa ni 'Ndiyo' kwa sababu tu hakumchinja yule ng'ombe!
- Lowassa alipokuwa Waziri Mkuu, alikuwa anahaingaika kumjibu kuanzia kwenye magazeti, mpaka humu JF kumjibu member mwenzetu Mwanakijiji, ilikuwa ni kwa sababu haaminiki, haeleweki, na hana msimamo!
- Na juzi Rostam, alikuwa anahaha kumtafuta Mwanakijiji apunguze mashambulizi, kwa sababu haeleweki, haaminiki, na hana msimamo!
- Mkulu Mwanakijiji, I hope hukatishwi tamaa wala kuogopeshwa na hizi kelele za mlango, sio siri kwamba kuna wasioweza kuelewa masilahi ya taifa na ya binafsi, lakini kwenye demokrasia hatuna jinsi ila kuwa nao tu, lakini mapambano yanaendelea. Kuna ishu ambazo sikubaliani na Mwanakijiji, lakini sio kupiga vita ufisadi, kwenye hili tupo pamoja mkuu MMJ, na job welldone keep it up!
Respect.
Wazee wa sauti ya umeme FMES!