Lowassa could've done better...

kila mtu ana uzuri na ubaya wake ilakwa hili la ufisadi lowasa asingeweza kabisa na hata kwa hili suala la madini mzee asingeweza kwa mambo ya demokrasia huru nalo bado nina shaka ila labda angekuwa nafuu
 
Ukweli ni KUWA LOWASA ni fisadi kama walivyo wana CCM wengine..and so magu...Common denominator kwao wote ni Ufisadi.so usitegemee wakachukuliana hatua.

Mimi nawalaumu CHADEMA kujichanganyana sana na hatimaye kusababisha wananchi waende katika uchaguzi kushindanisha wana CCM wawili.

Kosa ambalo kila siku chadema wanafanya ni kutokuwa na Malengo ya Muda mrefu ,ya kati na muda mfupi.Succession Plan ikiwa ni jambo la msingi sana.

chadema walipaswa kumweka mtu aliyeshiba filosofia na itikadi ya chama chake.mtu ambaye amejitambulisha na kubeba taswira ya Chadema.Kimsingi ilikuwa ni kosa sana kumsimamisha lowasa kama mgombea wa urais wa Chadema.Ila wangempokea na kusuport mtu mwingine Let say Slaa.Leo tungeonea mambo mengine hapa.

Na kosa lingine wanalofanya ni kutojipanga kwa chaguzi zijazo.Hata huyo lowasa amekuwa na faida kwao kwa short run.in long run anawagharimu.Calliber yake haiwapi uhai wananchi na kuona future ya taifa ndni yake.

Chadema wasitegemee kupata mteremko.waache kulalamika.haiwasaidiii.wakomae

cc Nguruvi3 Mzee Mwanakijiji
 
Unaweza ukaongea sna mkuu hawata kuelewa sababu watz wengi ni static not dynamic.
sipendi.kuongea mengi nna sbabu zangu .....mpe mda.JPM
 
Mkuuu JF kuna depended mind ......too static and rigidilly...idea.Ukisema hayo utapngwa tu.
 
Jaribu kuwa makini unapojibu hoja ya mtu. Jina tu linakushinda. Hayo mengine inakuwaje?
You asked a question (Is it plagiarized work? and I answered your question.

Hoja gani ya mtu unayoongelea? Huko kulikosea spelling jina lako la kizungu linahusianaje na swali lako? Au hata maana ya plagiarism huijui, unanakiri kama kasuku? Jibu nililotoa is 100% correct for your plagiarized question, Mr Invincible.
 

Unatoa jibu halafu unajisahihisha mwenyewe.
 
Mkuu nadhani kuna namna inatakiwa tuangalie issue hii kwa jicho la tatu.

Kwanza utambuwe kuwa hizo kashfa zilitoka ndani ya serikali kwa wana ccm wenyewe.

Kwa mantiki hiyo, kuna mawili

1) waliowapa siri chadema wana malengo yao binafsi na ya kisiasa. Nina imani kwamba vita ndani ya ccm ndo inapelekea hizo siri kuvuja. Na wanaozivujisha, pengine wakiwa na malengo ya binafsi ya kisiasa nk.

2) Kwamba walivujisha siri kwasababu ya uzalendo. Hii pointi nina mashaka nayo sana. Kwasababu kama bado wamo humo humo, hawataki kutoka, zaidi zaidi wanazidi kuji position kwa madaraka zaidi, ulaji nk, basi nasita kusema ni uzalendo. Naona kama ni malengo binafsi zaidi na ya kisiasa.

Hilo nimegunduwa kwasababu hadi sasa yule aliyekuwa akipigiwa makelele kama fisadi mkuu, hayuko kwenye kashfa kuu za kifisadi. Hapo unaweza kuona pengine wapiga kelele wale walikuwa wanataka wawachafue baadhi ya wanasiasa wanaowaona ni kizingiti kwa malengo yao binafsi ya kifisadi pamoja na yale ya kisiasa.

Inawezekana kabisa hao watu waliwaingiza chaka chadema. Hilo sikatai.
 
Ndo maana sa hivi tuache mambo ya siasa tuangalie Taifa letu humo kwenye siasa hao watu wanajua wao wanachokitaka hivi vyama vilificha watu wengi ambao wapo kwa ajili ya manufaa yao wenyewe na si taifa wamekua wanatumia nguvu ya vyama na support ya wananchi kwa ajili ya manufaa yao wenyewe na ndio maana tulihitaji rais kwanza asie na mambo ya siasa na uhuni wa humo ili kufikia tunapopataka huyo mzee mimi naona tungepigwa tu changa la macho baadae tena tuje na hadithi nyingine
 
Lowassa angekuwa mbinafsi, angebaki ccm kama hao wengine? Unadhani hajui madhara ya kuwa upinzani? Siasa ni kazi yake lakini kazuiwa.

Mhalifu anapelekwa mahakamani au anazuiwa siasa?
 
1) waliowapa siri chadema wana malengo yao binafsi na ya kisiasa. Nina imani kwamba vita ndani ya ccm ndo inapelekea hizo siri kuvuja. Na wanaozivujisha, pengine wakiwa na malengo ya binafsi ya kisiasa nk.
Mkuu.huhitaji kupewa siri kujua kuwa lowasa alihudumu kama waziri kwa miaka mingi sana.akiwa kwenye baraza ameshiriki kuidhinisha mambo mengi ambayo yameitia nchi hasara.Vile vile magufuli.

Tena lowasa yuko kwenye Cabinet toka miaka ya tisini mwanzoni .magufuli mwaka 1995.wote kwa pamoja wameshiriki kuleta madudu mengu tu.kwa hio huhitaji kupewa siri yoyote
Lowasa ni fisadi mkuu.bado tu hutaki kuamini.Pona yake ni kwa sababu yeye ni CCM kama CCM wenzake.Ufisadi kwao ni jadi.kamwe hawawezi kuchukuliana hatua
 
JPM japo ana dosari ila amejitahidi kupita kiasi kwa yale mazuri
 
Mkuu, since we have to work with what we have, lazima ujuwe kuchambuwa kati ya mchele na chuya.

Hadi usawa huu, ninaamini chadema waliingizwa mkenge na ccm kwakuwapatia "taarifa za ufisadi" zenye malengo yao binafsi. Tatizo ni kwamba chadema hawajakubali ku admit hiyo kitu.

Unaposema pona yake ni kwasababu yeye ni ccm hata sikuelewi.

Nasema we gotta work with what we have kwasababu karibia wote wanaotaka urais washakuwa kwenye cabinets.

Na kwa jinsi ambavyo wanajali kuhusu "collective responsibility ", wote wanakuwa responsible. Na anayekwenda kinyume ni msaliti wa serikali na atafukuzwa. Haijalishi kwamba issue yenyewe ni mbaya kwa maslahi ya Taifa. Na kwahivyo ccm hapo wako responsible.

Mimi nimepima na kuangalia siasa ambazo zimetuletea rais aliyeko madarakani, nikatizama nyuma. Nikaona where and what went wrong, ndo maana hata sasa wananchi wengi wako confused kuhusu chadema, na wao hawajachukuwa hatua yoyote kutoa maelezo na kuwataka radhi wananchi. Kwa namna nyingine nashindwa kuwalaumu moja kwa moja kwasababu wamezuiwa kufanya siasa.
 
kila mtu ana uzuri na ubaya wake ilakwa hili la ufisadi lowasa asingeweza kabisa na hata kwa hili suala la madini mzee asingeweza kwa mambo ya demokrasia huru nalo bado nina shaka ila labda angekuwa nafuu
Kwani la ufisadi nani ameweza hadi usawa huu?

Na hata hiyo ya madini si ni hao hao walioko madarakani walisaini hiyo mikataba?

Afadhali Lowassa yuko kwenye timu ya Tundu Lissu ambaye alipingana na hiyo mikataba toka enzi na enzi. Afadhali ni nani kati ya hao wawili hao wawili kama si aliyeko kwenye timu inayopinga mikataba mibovu kusainiwa? Upande ambao hautaki tupate hasara kwa maamuzi mabovu?

Huyu wa sasa bado anakumbatia chama kilekile chenye watu walewale.

Usidanganywe na siasa za kuitana wasaliti. Kuwa makini usijekuta unaicheza ngoma yao kama walivyofanya chadema.
 
Magufuli ni rais bora kabisa kuwai kutokea. Acheni akili fupi za kiafrika, huyo lowassa kwa mfano angefanya nini ambacho magu hafanyi zaidi ya wizi yeye na genge lake la kina rostam karamagi

Hilo genge limefikishwa Mahakama ya mafisadi au bado linarandaranda mtaani?
 
Mimi ni muhanga wa ajira lakini bado nampenda
Me ni muhanga wa bomoa bomoa lakn bado nampenda. Najua anafanya haya kwa manufaa ya wengi
Naona kuna huruma huruma kama vile Raisi anaonewa. Ukweli ni kwamba ni Magufuli mwenyewe kajitakia haya matatizo pasipo ulazma.

Kuzuia wapinzania kufanya mikutano, kuzuia bunge kuenda live, watu kufa kufa kiajabu, wanasiasa kuwekwa ndani bila sababu ya maana, wanasiasa kupigwa risasi, visasi mpaka kwa mawakili kuvunjiwa maofisi an Manji anavyofanyiwa.., kubomolea watu nyumba kinyume na sheria... .

Kusema unapenda nchi halafu ukiletewa wala rushwa husemi lolote mpaka wawe maaduni wako.

Kusema hupendi vyeti feki wakati huohuo unaajiri watu wenye vyeti feki.

Kusema hapa kazi tu wakati unafanya mikutano ya CCM ikulu....

Wivu wa kikanda kuzuia Moshi kuwa jiji bila sababu ya kimsingi...

Hizi ndiyo sababu watu wanamatatizo na Magufuli. Hakuna Mtanzania asiyependa maendeleo lakini watu hawatampa raisi maisha yao kwa kisingizio cha uzalendo wakati hafuati hata anayosema mwenyewe
Source: Kamundu
 
Labda tuseme "Maghufuli ni mtu mzuri", lakini sisi watanzania ndo tumefanya makosa kumpa kazi asiyoiweza?

Au makosa ni yake kujaribisha kuomba kazi iliyomzidi uwezo?
 
I second this...

Uncle Magu anaweza akawa ni mtu mzuri tu.

Lakini pia nakubali wenye makosa ni partially sisi wananchi na partially yeye Magu mwenyewe.

Sisi tuliompigia kura kwa kumpa majukumu ambayo hayawezi, tulifanya kosa kubwa....

On the other side, na yeye yuko responsible kwa makosa kwa kujaribisha kazi ambayo haiwezi na haitakiwi kujaribishwa, Bali inatakiwa uwe na maono kwa Taifa.

Hayo aliyaweka wazi yeye mwenyewe. Kwamba alijaribu tu, hakuwa anafikiri kuwa atashinda, na siyo kazi aliyokuwa ana uhakika anaweza kuifanya.

Haitakiwi uwe genius kujuwa kuwa sumu haionjwi.
 
Unadhani nick name ya "mtu mwenye maamuzi magumu" ilianzia wapi?

Na uwajibikaji haukuwepo alipojiuzulu?

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.



TUJIKUMBUSHE: Vita ya Lowassa Urais na Rais Kikwete
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…