Arien
JF-Expert Member
- Aug 29, 2017
- 11,245
- 11,777
yaweza kuwa kweli yote ya kwenye uzi huo. ila nina maswali mengi ambayo huo uzi haujajibu.
mfano kama Kikwete alishashtukia mikakati ya Lowasa tangu '95 ikawaje akakaa kimya mpk juzi alipokuja kumtoa kwenye uwaziri mkuu?? Kikwete alishashinda urais alikua na ulazima gani wa kutimiza ahadi ya kumpa cheo kikubwa EL?? alishindwa nini kumchinjia baharini?? halafu mbona huu uzi haujaongelea kauli ya JKN kumuita Kikwete 'bado mdogo' mwaka '95 alivyotaka pitishwa? au ni uongo hiyo kauli?
usitake kumfanya JMK aonekane alikuwa msafi ilhali inajulikana kabisa alikuwa mwizi,yeye na EL wote wezi tu!...hata Pombe pia hana tofauti na hawa wawili. na kama Pombe angekuwa na nia ya kutokomeza ufisadi angeanza na EL maana hiyo mikataba mpk leo bado inatutafuna ila mbona anamuangalia tu?? hakuna asiejua jinsi jamaa alivyo na kisasi angekua kashampeleka kwenye hiyo mahakama yake mpya. sasa watu wataaminije kuwa ni fisadi kweli ilhali hachukuliwi hatua? ni ukweli ulio dhahiri huo uzi unaleta maswali mengi kuliko majibu.
nachelea kusema kuwa inawezekana kazi ya EL sasa chadema ni kama alichoenda fanya Mrema NCCR Mageuzi miaka ile!