Lowassa anasafishwa!

Jamani sasa tumeanza kuona wale waliohongwa na lowassa ila wamtetee.UNAJUA WATU WENGI HAWAJASOMA ILE RIPOTIsasa wanasikiliza tu mtaani kumesemwa nini jamani someni na uzuri iko humuhumu jfs
 
Jamani sasa tumeanza kuona wale waliohongwa na lowassa ila wamtetee.UNAJUA WATU WENGI HAWAJASOMA ILE RIPOTIsasa wanasikiliza tu mtaani kumesemwa nini jamani someni na uzuri iko humuhumu jfs


Jana usiku nimesema hila na ghilba za wana CCM, system na JK mwenyewe kutumia watu na vyombo kumsafisha Edo. Leo mmeanza kuona nadhani Pope hajasoma mabandiko yangu . Wakati niko mtaani naona Pope kaja na yale niliyo yasema .Haya kazi kwenu .
 
Jana usiku nimesema hila na ghilba za wana CCM, system na JK mwenyewe kutumia watu na vyombo kumsafisha Edo. Leo mmeanza kuona nadhani Pope hajasoma mabandiko yangu . Wakati niko mtaani naona Pope kaja na yale niliyo yasema .Haya kazi kwenu .

Bila shaka Mkuu Lunyungu!
Tuachie kazi hiyo, tunaamini na kukuhakikishia kwamba tutahangaika nao hawa watetezi kwa hoja hadi wanywee. Bado tunasisitiza kwamba ripoti ya tume ya Mwakyembe ipo hapa Jf, na nimeweka kiungo chake hapo juu. Waisome kwa makini na kuielewa kabla ya kuandika bila kujua wanachostahili kukitetea!
Long Live JF
 
Jana usiku nimesema hila na ghilba za wana CCM, system na JK mwenyewe kutumia watu na vyombo kumsafisha Edo. Leo mmeanza kuona nadhani Pope hajasoma mabandiko yangu . Wakati niko mtaani naona Pope kaja na yale niliyo yasema .Haya kazi kwenu .
LUNYUNGU ushindi ni lazima kwa gharama yoote ile.Sasa tumeanza kuwaona na bado wale wa magazet yani waandishi wenye tamaa wataandika maajabu huko yetu macho.jamani kama kuna mwenye kufahamu site ya mwanahalisi anisaidie wakuu
 

Kishaju highlight unachotaka kunukuu kwanza , halafu fuata maelekezo hapo juu
 
Kaka Idimi hakuna wakumtetea mtu.
Kumbuka kuna kusoma na kusoma na kutafakari.
watu hofautiana uelewa wa jambo.
si kwamba nabishana na wewe la hasha lakini naamini wapo wanaoendelea kuelimika kuhusu suala hili zaidi yangu mimi, Tafsiri ya maneno ya mtu inatofautiana pia. kwangu mimi sioni kosa kuhoji hili kwani JF ni jukwaa la kusemea na ni hapa ndio naweza pata jibu la swali langu ni kwa watu kama wewe, sio mwenye maono tofauti kapotoka lahasha!!

Saluti kaka Mkandara.
 
Tunachotaka wananchi kusikia ni majibu yake ktk sehemu tu ya madai ya kamati teule ya uchunguzi..Kama angeweza jibu kipande hiki labda ningeweza kumpa pumzi za muda kabla ya kusulubiwa.

Nacho kinasema hivi:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyodokeza awali, Kamati Teule ilishindwa kubaini moja kwa moja chanzo cha ujasiri wa kiburi ndani ya Wizara ya Nishati na Madini kiasi cha kupindisha maamuzi ya Baraza la Mawaziri bila wasiwasi wowote, kukaidi ushauri wa kitaalamu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma mara tatu mfululizo na kinyume na maagizo ya Baraza la Mawaziri yaliyotaka Sheria ya Ununuzi wa Umma izingatiwe, kukiuka sheria kwa makusudi kwa kuingilia mchakato wa zabuni wa taasisi nyingine ya ununuzi, kuvipuuza vyombo vya ndani vya maamuzi vya TANESCO (Bodi ya Wakurugenzi, Bodi ya Zabuni n.k), kuilazimisha Bodi ya Menejimenti ya TANESCO kuridhia maamuzi yaliyofanywa na Wizara ya kuibeba Richmond Development Company LLC kinyume cha sheria na taratibu, n.k. Aidha Kamati Teule ilishangazwa na Ofisi ya Waziri Mkuu iliyokuwa ikifuatilia kwa karibu mchakato huo, kushindwa kukemea ukaidi huo wa Wizara ya Nishati na Madini.

Baadhi ya mashahidi, wakiwemo waandishi wa habari mashuhuri nchini, waliinyooshea kidole Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa msingi wa ubabe uliokithiri wa Wizara ya Nishati na Madini katika kuibeba Richmond. Aidha baadhi ya nyaraka ambazo Kamati Teule ilipata katika uchunguzi wake zilionesha kuwa maelekezo na maamuzi mengi ya msingi yalikuwa yanafanywa na Waziri Mkuu badala ya Wizara. Mfano ni barua kutoka Wizara ya Nishati na Madini kwenda kwa Waziri Mkuu tuliyoinukuu ukurasa wa 31 wa taarifa hii, ikitamka wazi kuwa GNT ilifanya majadiliano na Richmond Development Company LLC tarehe 8 hadi 16 Juni 2006 "kwa kuzingatia maelekezo" ya Waziri Mkuu.

Vilevile, Mheshimiwa Spika, tarehe 13 Julai 2006 Waziri wa Nishati na Madini akamwandikia Katibu Mkuu wake kuwa, "Nimezungumza tena na Mheshimiwa Waziri Mkuu leo juu ya bei ya mitambo ya Aggreko. Msimamo ni ule ule niliokueleza awali na ameagiza tuulizie Richmond kama anaweza kutoa 40 MW kwa bei isiyozidi ile ile ya 4.99 cents per kWh na kama tunaweza kuipata basi achukuliwe Richmond".

Mheshimiwa Spika, ushiriki huu wa karibu wa Waziri Mkuu katika kila hatua ya zabuni ya umeme wa dharura, si lazima uwe ushahidi wa kwamba kiongozi huyo wa kitaifa alihusika katika kuibeba Richmond. Unaweza pia ukawa ushahidi wa staili yake ya kawaida kabisa ya uongozi katika kufuatilia masuala yote ya kitaifa kwa karibu sana tukizingatia kwamba nchi wakati huo ilikuwa katika kipindi kigumu sana cha ukosefu wa umeme. Watu pekee waliokuwa wanaujua ukweli wenyewe, ukweli ambao ungeipa Kamati Teule msingi wa kumhoji Waziri Mkuu kwa kiapo, walikuwa watatu: Waziri Dk. Msabaha (Mb), Katibu Mkuu Mwakapugi na Mwenyekiti wa Bodi Balozi Kazaura.

Mheshimiwa Spika, Kamati Teule ikawaita kwa mara ya pili Dk. Msabaha (Mb) na Ndugu Mwakapugi kwa mahojiano zaidi. Wote wawili, wakiwa ndani ya kiapo, walikataa katakata kupokea maagizo kutoka kwa Waziri Mkuu ya kuipa Richmond upendeleo. Lakini Mhe. Dk. Msabaha (Mb), baada ya mahojiano chini ya kiapo, akaiuma sikio Kamati Teule kuwa katika suala hilo yeye atakuwa kondoo wa kafara tu au, kwa maneno yake mwenyewe, "Bangusilo" kwa lugha ya Kizaramo. Maelezo hayo ya ziada nje ya kiapo ya Mheshimiwa Waziri yaliyotoa ujumbe kuwa "si yeye ila mkuu wake wa kazi", yalioana na maelezo aliyoyatoa Balozi Kazaura nje ya kiapo tarehe 30 Novemba, 2007. Mara baada ya kumaliza mahojiano kwa kiapo na Kamati Teule, Balozi akatoa maelezo ya ziada kuwa Richmond ilikuwa mradi wa "Bwana Mkubwa" na "mshiriki wake mkubwa kibiashara", akimaanisha Mhe. Waziri Mkuu na Mhe. Rostam Aziz (Mb).


Sikuona maelezo yoyote ya Lowassa yanayopingana na taarifa hizo!
 
Kama nilivyosema huko nyuma, Mwakyembe ilibidi amhoji Lowassa.Sababu zilizotolewa katika ripoti haziridhishi.

Naelewa Lowassa anahusika kama sio moja kwa moja katika rushwa basi anawajibika kama Waziri Mkuu, mtu aliyetakiwa kuhakikisha mambo yanaenda sawa.Kwa hiyo kusema "Lowasa kaonewa" inakuwa kwenda mbali kwa sababu inatoa picha kwamba Lowassa hakuhusika kabisa, au hakupewa nafasi ya kujitetea hata bungeni, which is not the case.

Tatizo ni kwamba kutomhoji kwa Mwakyembe na wenzake kumepelekea ripoti kutolewa bila input yake.Lowassa anaweza kusema kuwa ripoti ile ambayo ndiyo ime influence yeye kutoka uwaziri mkuu ilikuwa biased na yeye hakupata nafasi ya kujitetea as far as that report is concerned.It is important that justice not only be dispensed, but also that justice appears to be dispensed.The fact that in this case at least in the context of the report there is room for justice to appear as not dispensed is troubling. Mimi naona Mwakyembe angemhoji Lowassa, halafu Lowassa angejitetea kwamba "nilijaribu kuvunja mkataba lakini watendaji walinishauri vinginevyo" na ripoti ingeyafanyia uchunguzi zaidi madai hayo, ripoti ingetoka ikiwa imekamilika zaidi.

Tatizo linalojitokeza sasa ni kuwa Lowassa anasema alishauriwa vibaya na watendaji, watendaji wanasema walikuwa pressured na Lowassa, moja kati ya pande mbili hizi haisemi kweli.Mwakyembe alikuwa na nafasi nzuri sana ya kuangalia mambo kama timeline na vitu vingine muhimu kwa kuzihoji pande mbili zote.Inawezekana kabisa Lowassa anajikosha tu na kutaka kwake kuuvunja mkataba kulikuja baadaye sana alipoona mambo yanaenda arijojo.

Mwakyembe angemhoji Lowassa leo hii tungejua vitu kwa mwanga mzuri zaidi na pengine Lowassa angekosa cha kusema to the point ya kukubali guilt ya kuwa pressure watendaji.

Hoja kwamba Lowassa alikuwa na nafasi ya kujitetea bungeni ni nzuri lakini kama mtu anaipotray ripoti ya Mwakyembe kama a well concocted witch hunt iliyokuwa na nia moja tu ya kumtoa Lowassa kwa kukusanya circumstantial evidence nyingi sana na kuchukua public opinion miongoni mwa wabunge, then regardless ya utetezi wa Lowasa alikuwa ameshamalizwa kisiasa na ripoti na utetezi zaidi ungeweza hata kukigawa chama na serikali, so in principle angeweza kujitetea lakini in reality ilibidi awajibike at least kwa uongozi mbovu au hata kwa involvement, lakini hata kama hakuwa involved directly utetezi zaidi ungelipua mgawanyiko zaidi.

Kamati ya Mwakyembe ilifanya kazi nzuri.Ingefanya kazi nzuri zaidi kama ingemhoji Lowassa kabla ya kuwakilisha ripoti bungeni.
 
Hivi Lowassa hana washauri? kama anao basi wamwambie anyamaze anatuchefua. kila nikikumbuka milioni 152 kwa siku namkumbuka yeye hata kama alikuwa hachukui yeye lakini kafanya uzembe usiovumilika. Asiendelee kuongea anatupandisha hasira.
 
Hivi kwa nini hiyo tume ya Mwakyembe haikumhoji Lowassa..? I thought that would've been a no-brainer...
 


Mpaka muda huu bado Lowasa hajachelewa.Namshauri kwa kuwa Kamati wa a legal thing basi na yeye anaweza kwenda Mahakamani kusafisha jina lake .Haki hii anayo kabisa na ya kimsingi .Lakini Wakili itabidi amuulize juu ya madai yake ya Natural Justice .Maana anaililia yeye lakini alio wahi kuwafukuza kazi tena kujwaani kwa aibu kubwa sijui hawakuwa entitled na hilo ?
 
Hivi Lowassa hana washauri? kama anao basi wamwambie anyamaze anatuchefua. kila nikikumbuka milioni 152 kwa siku namkumbuka yeye hata kama alikuwa hachukui yeye lakini kafanya uzembe usiovumilika. Asiendelee kuongea anatupandisha hasira.


Kizito,

Hii ni kweli kabisa.Kwa kuzidi kuongea Lowassa anajichimbia kaburi zaidi.Anaweza kuwa anataka kujisafisha na kuweka elements za doubt kwenye process nzima iliyosababisha kujiuzulu kwake.Lakini ni vizuri ajieleze zaidi, hapo tunapata majibu ya mambo au hata kama sio majibu tunaona spin zake zikoje.

Ingekuwa vizuri zaidi kama angejieleza kortini baada ya kula kiapo huku akijibu mashtaka.
 

Na ndio ilikuwa hoja yangu mimi sikatai kuhusika kwake hata kidogo lakini input yake haimo ina fanya yeye awe na base ya kuseme.
 
Ni kweli pengine angelihojiwa angelitoa maelezo kuhusu kilichojiri. Kwa kusikiliza maelezo yake TVT kupitia KLHNews, kumhoji kusingelibadilisha ulazima wa yeye kuwajibika. Nikimnukuu H.Truman "The buck stops here", yeye ndiye aliyeichagua kamati hivyo, muwajibikaji kwa mazuri(misifa) na mabaya anabakia yeye wala si akina Mgonja au Mwanyika. Kushituka baada ya mkataba kutiwa sahihi lazima kuwe na vipengere vinavyoruhusu. Kosa la kutokuwa na vipengere hivyo ni la Mwanyika kiutekelezaji. My dear Lowassa you have to bear your political responsibility with humility.
 
.........kwa kuwa yeye mwenyewe EL alidai ripoti ya tume ingekuwa tofauti kama angeitwa na kujieleza.................

sasa tumeona maelezo yake TvT.................hivi wandugu mnafikiri maelezo yake yangebadilisha kitu gani katika ripoti ile??????..........ABSOLUTELY NOTHING!!,

......walio wavivu wa kusoma ndio watakuja na kila sababu za kutaka kuosha huu uovu wa Richmond.............

Bob Mkandara you have said it all my brother............!!!

Process ya ku-procure the so called Richmond ndio TATIZO ambalo lilipata baraka za EL....thats where the PROBLEM IS......................maelezo mengine yooote ni kufurahisha jamvi................na hapa ndio watu waelewe ni kwa jinsi gani WANASIASA WANAVYOWABURUZA WATAALAMU!!!

Imagine this.......kampuni iliyokuwa rated low if not the lowest in the evaluation of tender ndiyo ikachukuliwa kupewa zabuni under EL Influence.................halafu baadaye unakuja kuwauliza makatibu wakuu and senior officers ili hali wakijua kabisa mpaka kufikia hatua hiyo ni wewe EL uliyesababisha........unafikiri wangekuambia nini BOSS wakati wanajua wewe mwenyewe ulikuwa forefront ili Richmond ipate Zabuni.......halafu funny enough swali lako kwao hao makatibu wakuu lilikuwa extremely WEAK.......na wao kujiweka on safe side...."only at that particular moment" (ofcourse not now......because they got to go as well).....na wakakujibu kirahisi within AN HOUR kuwa the CONTRACT is CLEAN!!!.....very funny indeed.................in other words walikuwa (PSs and senior Officers) wanakuambia "....thats your ball BOSS...."

na sasa tunasema hao makatibu wakuu, mwanasheria mkuu, DG PCCB na other senior officers waliohusika wawajibishwe....kwa sababu walishindwa kumshauri BOSS wao amabye tayari keshawajibika........wao wanasubiri nini?.....hatuataki WATU WAOGA WA KUSHAURI SERIKALINI.....ndio maana tunaishia shimoni kila siku kwa sababu za UWOGA
 

Mzee Lunyungu kula tano!

What goes around comes around.Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu.Niilishamuua sana Lowassa kwa umangimeza, now that he is getting a sip of his own medicine he is crying.I wonder what all the DC's and region/distict level executives he used to bully are thinking.Nakumbuka not long ago alimkatisha DC Mongella speech na kuanza kumuua mbele ya hadhara, sijui alikuwa anafuata "natural justice" hapo

It's karmic repercussions at play.

Nevertheless, two wrongs do not make a right, he should have been questioned by Mwakyembe.
 

Ogah
Plan A ya richmonduli imeshakataa sasa aangalie plan B lakini awe mtulivu maana katumbukia mwaka 2008 ambao JF hatulali .Watatuona wabaya lakini we need Tanzania yenye neema ya kweli .
 

Msavila,

Naelewa mtiririko wako kuhusu uwajibikaji wa Lowassa.Lakini mimi nilifikiri kina Mgonja na Mwanyika pia walihitaji kuwajibika/kuwajibishwa.Kwa nini unafikiri akiwajibika Mkuu wadogo wasiwajibike?

Hii sasa si inakuwa "reverse bangusilo" tu? Tunataka kila aliyeshiriki kupitisha mikataba feki awajibike.Mimi ningemuheshimu sana, na hata kuomba arudishwe kazini katibu mkuu au mtendaji mwingine yeyote yeyote ambaye angejiuzulu kwa sababu alikuwa pressured ku sign mikataba feki, hakuna aliyejiuzulu.
 
Richmond bomu zito

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…