Lowassa anasafishwa!

Lowassa anasafishwa!

Njaa zao zitatufikisha mahari pabaya...ebu wahandishi wa habari mlio safi na kama mnawajuwa wenzenu wanaofanya vitendo hivyo wakemee kwa nguvu zote waache kabisa hizo tabia.

Wakumbuke wanayoyafanya leo ni wajukuu wao na wa kwetu watakaopata shida sana...si muda si mrefu sana wote tutakuwa mavumbini na kuacha vyote tulivyopanda hapa hapa duniani...iwe tulivipata kwa jasho letu au kwa ufisadi...

Tujiulize wote nani atakuwepo miaka 30 ijayo....kama si watoto na wajukuu zetu. Sasa waheshimiwa mafisadi tafadhalini sana badili hizo tabia zenu...na nyinyi baadhi ya wahandishi msiokuwa na maadili msikubali njaa zenu ziwafanye kuwa watumwa...

Mungu tuapushe na haya mafisadi yasiyo na aibu....
 
Njaa zao zitatufikisha mahari pabaya...ebu wahandishi wa habari mlio safi na kama mnawajuwa wenzenu wanaofanya vitendo hivyo wakemee kwa nguvu zote waache kabisa hizo tabia.

Wakumbuke wanayoyafanya leo ni wajukuu wao na wa kwetu watakaopata shida sana...si muda si mrefu sana wote tutakuwa mavumbini na kuacha vyote tulivyopanda hapa hapa duniani...iwe tulivipata kwa jasho letu au kwa ufisadi...

Tujiulize wote nani atakuwepo miaka 30 ijayo....kama si watoto na wajukuu zetu. Sasa waheshimiwa mafisadi tafadhalini sana badili hizo tabia zenu...na nyinyi baadhi ya wahandishi msiokuwa na maadili msikubali njaa zenu ziwafanye kuwa watumwa...

Mungu tuapushe na haya mafisadi yasiyo na aibu....

Napata wasi wasi kuna wanaJF wengine hapa wanafanya kila wanachoweza kumsafisha mzee Mamvi tupo makini tutapamba tuweke wazi ukweli...Lowassa akae kimya atumikie wananchi wake wa Monduli, hata aje kivipi amechafuka...mwandishi alimhoji kwenye TV ni bomu kweli kwanini hakuumuuliza Mwal Nyerere aliisha mwona kama EL hafai sababu ya kujilimbikizia mali? Alimwacha EL akifanya fani yake ya usanii jukwaani TVT bila break...Please EL rest in peace Monduli usitafute namna ya kutoka
 
Ninacho sisitiza mimi mkubwa ingekuwa bora sana kama Ng'ombe huyu angechinjwa kwa kugeiziwa Kibra ili kuhalalishwa uchinjani wake...

kwa akili ya kawaida hebu msikilize hapa....

"Nikaanza kusikia minong'ono nikamwita Waziri mwenye dhamana(Hakumtaja kwa jina) nikamuuliza mbona naanza kusikia harufu mbaya kuhusu Richmond lakini Waziri akanihakikishia kila kitu kiko sawa," alisema.

Kadri siku zilivyozidi kelele juu ya Richmond zikazidi hivyo akaamua kuwaita wakubwa wote serikalini wakiongozwa na katibu mkuu kiongozi, Philemon Luhanjo na kuwambia waangalie uwezekano wa kuvunja mkataba huo.

Lowassa alijitetea kuwa, wakubwa hao wakaomba awape muda wa saa moja kupitia vipengele vya mkataba huo na baada ya hapo walikuja na maneno kuwa isingewezekana kuvunja mkataba huo kwani serikali ingepata hasara.

"Lakini mimi niliwauliza mbona tumevunja mkataba na City water wakaniambia aah mzee achana na hilo jambo kwa sababu liko mahakamani, hii ndio hali halisi ya mkataba wa Richmond,"alisema Lowassa.
 
Huyu jamaa alishajimaliza mwenyewe kisiasa kabla hata hili balaa halijamkuta. Staili yake ya ufanyaji kazi kwa pupa, kufanya maamuzi ya njia za mkato bila kufuata utaratibu na wakati mwingine kuwaumbua viongozi wenzake kwenye mikutano ya hadhara yalikuwa yanatosha kuwafanya hata CCM wenyewe wamchukie.

Lowassa alichafuka zamani kabla ya Richmond
Waandishi Wetu Februari 20, 2008

  • Kikwete alijulishwa, akapuuza
HATA kama tuhuma za kampuni hewa ya Richmond zingemnusuru, aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, asingefika mbali, kwa vile alikwisha kujitengenezea maadui wengi ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), bungeni na serikalini, Raia Mwema imefahamishwa.

Hatua ya Lowassa ya kujiuzulu kiasi cha wiki mbili zilizopita, ilikuwa inahitimisha tu mlolongo wa matukio ndani ya CCM, bungeni na serikalini na hata katika nyanja za kibiashara na kijamii, yanayokwenda nyuma katika wakati wa mchakato wa kutafuta mgombea urais ndani ya chama hicho, na baadaye katika utendaji wa kila siku akiwa Waziri Mkuu.

Endelea na story hapa RAIAMWEMA
 
Nimeisoma Riport Ile...
Ninachosema Kama Hakuewa Fursa Ile Anahaki Ya Kujitetea Kwani Hakuwa Na Pakuongelea Jamani!!

halafu ktk JF tafuta posts za augustoos ukizisoma basi naamini utaweza kujenga hoja nzuri tukuelewe kwa nini unasema EL kaonewa. Pia kuisoma ripoti ya mwakyembe na ukifuatilia footage za bunge ktk hansard utagundua kuwa hizo doubt zako zilitolewa ufafanuzi ktk majumuisho ya kamati. na pia kama una maswali zaidi nadhani ukienda ktk ofisi za Bunge watakusaidia kwa nini kamati haikumhoji EL.
Kila kitu kipo wazi ila watu ni wagumu kuelewa wanapenda kusikia au kuambiwa ila hawataki kuona na kutambua
 
Nimeisoma Riport Ile...
Ninachosema Kama Hakuewa Fursa Ile Anahaki Ya Kujitetea Kwani Hakuwa Na Pakuongelea Jamani!!

Mkuu Pope,

Uwe muangalifu sana usijejipaka matope wakati unataka kumwosha mtu.

1. Kama umesoma vizuroi ripoti ya bunge (maana kuna uvivu sana wa kusoma ile, hata RA aliambiwa asome yeye akarukia jambo lingine) utaona kwamba kuna sababu kwa nini hakuhojiwa. Kama wawakilishi wa wananchi walijiridhisha na ripoti ile, wewe inabidi ujenge pointi za maana sana ili tukusikilize.

2. Edo alifanya jambo la ajabu sana kutumia nafasi aliyopewa bungeni achangie mjadala unaomhusu, nafasi ambayo angeweza kujitetea, kuwa alisingiziwa kwa sababu hii na ile, badala yake yeye akatangaza kwa jazba kuwa ana resign. Amefika wapi?

3. Amegundua sasa kuwa uamuzi wake utagharimu maisha yake yote yaliyobaki kisiasa, na ameanza kukuru kakara kuanza kujitetea, tena kwa kuwasingizia wenzake.

4. Lakini ukweli ni kuwa, hata ripoti haijasema yeye alihusika kwa namna unayoielezea...soma ripoti uelewe, na ujue kuwa we are watching guys like you who comes up with attractive threads to cleanse the Richmond scandal guys. Tumejadili kwa mapana sana juu ya mambo ya Lowasa et al, kabla hujajiunga hapa.

5. Edo ameshindwa hata kujitetea jana kwenye TvT. Alichoongea kwa kweli hakina mantiki kwa ku settle dust la Richmond. Huwezi kusema sasa umegundua Edo alionewa na kamati, na ukatupa sababu za maana.

Tu convince kwa hoja tukuelewe, si kwa blah blah tu, Mkuu. Karibu sana.
 
Mkuu Mbalamwezi

Nakubaliana na wewe asilimia 100%, kama ameonewa basi alikuwa na muda mzuri sana wa kujitetea kuanzia bungeni yeye alichofanya ni kukimbilia kujiuzulu. Agesimama kidete na kujitetea na baadaye labda angeweza kusafishwa...sasa maji yalishamwagika anajitahidi sana kuyarudisha...je ataweza.

Sawa wanasema ameonewa...na je yeye kaonea wangapi bila hata kuwa nafasi ya kujitetea.
a)Kumbuka ya kina mhandisi wa Temeke alivyoumbuliwa na vyombo vyote vya habari vikimulika.
b) Yule mama mkurugenzi wa same...naye aliumbuliwa mbele ya watendaji wake.
c) Mkuu wa wilaya mmoja kule mwanza naye aliumbuliwa eti EL anaikataa ripoti yake aliyokuwa anaiwasilisha wakati wa ziara yake...tena yule mkuu wa wilaya na alijitetea kwa kusema "Mkuu uwezi kuniambia kwamba mimi siwezi kazi" -nampongeza kwa sababu aliweza kukaa kidete.
d)Kule kigoma nako aliwatia kashikashi jamaa kuanzia kwa RAS na wengine.

Hayo ni baadhi ya aliyokuwa akifanya ambayo hayaonyeshi uongozi...sasa yeye anatuletea deko...kumbuka mtoto mkorofi mara nyingi yeye anasemaga kaonewa wakati wote....

Kama ni kujimaliza amejimaliza mwenyewe hakuna aliyemuonea...yale mahojiano TVT hapakuwepo na kitu pale.

Tumwombee atulie vizuri jimboni kwake afanye kazi ya uhamasishaji wakati akisubiri kuletwa mbele ya mkondo wa sheria...
 
Anawajibika kwa kosa la uzembe ,au nini maana ya kuwa Waziri Mkuu ,kama alishaona hivyo na kuachia watu wengine wafanye watakavyo basi ni wazi alikuwa goigoi na kushindwa kutumia wazifa wake kuzuia,kukataza na kupiga marufuku mwendelezo wa mkataba huo. Na kama kujiuzulu kwa nini asijiuzulu tokea mwanzo mpaka alipoona watu wamishabadilika rangi.Basi mambo bado akumbuke ile hadithi ya daraza la saba jamaa alipoambiwa ..Hayo utasemea polisi...na ire hadithi ya Sungura na ndizi aliposema sizitaki mbichi hizi ,ila sasa kama anataka mali ataipata shambani.
 
2. Edo alifanya jambo la ajabu sana kutumia nafasi aliyopewa bungeni achangie mjadala unaomhusu, nafasi ambayo angeweza kujitetea, kuwa alisingiziwa kwa sababu hii na ile, badala yake yeye akatangaza kwa jazba kuwa ana resign. Amefika wapi?

3. Amegundua sasa kuwa uamuzi wake utagharimu maisha yake yote yaliyobaki kisiasa, na ameanza kukuru kakara kuanza kujitetea, tena kwa kuwasingizia wenzake.


5. Edo ameshindwa hata kujitetea jana kwenye TvT. Alichoongea kwa kweli hakina mantiki kwa ku settle dust la Richmond. Huwezi kusema sasa umegundua Edo alionewa na kamati, na ukatupa sababu za maana.

Tu convince kwa hoja tukuelewe, si kwa blah blah tu, Mkuu. Karibu sana.
[/QUOTE]

Ndugu Kishaju,

Karibu sana JF. Una maana gani hapo juu? Kuna kitu kinaitwa plagiarism, unakifahamu?
 
...na ujue kuwa we are watching guys like you who comes up with attractive threads to cleanse the Richmond scandal guys. Tumejadili kwa mapana sana juu ya mambo ya Lowasa et al, kabla hujajiunga hapa...
[/QUOTE]

Sina nia ya kumsafisha mtu la hasha ila napenda kujua upande wa pili hasa nilikuwa na hamu kusikia kutoka kwake, na kujua na wengine wanalionaje ningeyajuaje yote haya mnayosema...
 
kwa hiyo ktk mahojiano ya tvt mkuu el aliamua kutueleza kwa nini hakupaswa kushiriki uwajibikaji wa pamoja?? na ni kwa nini aende vyombo vya habari kuanza kujipaka matope zaidi?? nadhani ccm kwa hili wamechemsha maana inaonesha kuna watu nyuma ya el ambao ndio wanamshauri what to do at what time.

nawaasa wapinzani waboreshe demokrasia ktk vyama vyao kwani ndio muda muafaka wa kupewa dhamana ya kutuongoza au la sivyo bado tutakuwa mikononi mwa mafisadi milele.
Kiongozi akichafuka amekichafua chama, haiwezekani kiongozi aende nje ya maadili halafu chama kikabaki salama kwa matendo ya kiongozi huyo. na kwa kuwa ccm haijatoa tamko la kuunga au kupinga maamuzi ya Bunge ni dalili kuwa utabiri wa Nyerere (RIP) utatimia kuwa siasa ya kweli itakuja nchini. Alijua jinsi chama chake kilivyopandikiza watu upinzani ili wafanye maigizo kisha tuone tuna demokrasia.

ndugu pope angalia sana unapochangia uwe unaweka stand au la hatutakuelewa hata kidogo
 
Tumwamini nani? Tume , Lowasa au watetezi wake? Tafuta riport ya Mwakyembe.

Na kwa kukandamiza zaidi ni kwamba ripoti ya Mwakyembe pamoja na muhtasari wake tunayo hapa JF, pitia kiungo hiki, "http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=832" waisome kwa makini na kuelewa sababu za kutokuitwa kwa Lowassa mbele ya tume, zimeainishwa waziwazi.
Nyie endeleeni kumtetea tu, tutawafukua na ninyi pia, kwani "Birds of feather fly together"
 
...na ujue kuwa we are watching guys like you who comes up with attractive threads to cleanse the Richmond scandal guys. Tumejadili kwa mapana sana juu ya mambo ya Lowasa et al, kabla hujajiunga hapa...

Sina nia ya kumsafisha mtu la hasha ila napenda kujua upande wa pili hasa nilikuwa na hamu kusikia kutoka kwake, na kujua na wengine wanalionaje ningeyajuaje yote haya mnayosema...[/QUOTE]

Kwa hiyo, baada ya kumsikiliza huko, umepata point gani hasa? Hebu zi sum hapa.
 


Ndugu Kishaju,

Karibu sana JF. Una maana gani hapo juu? Kuna kitu kinaitwa plagiarism, unakifahamu?[/QUOTE]


Ndugu yangu samahani yaani nilikuwa najaribu ku-quote kumbe pale juu nikafuta ndo maana ikaonekana kama vile imetoka kwangu...sikuwa na nia ya kuifanya kama "my original idea" Nilikuwa nataka nichambue baadhi ya vipengele ambavyo nimeviona vinanifurahisha.

Kwa hiyo ndugu yangu usinielewa vibaya...nina masaa chini ya 24 tangu nimeingia hapa...bado niko kwenye kujifunza...

Bila shaka umenielewa...hivyo sikuwa na nia ya kuiweka kama "original idea" yangu...nilikuwa nataka kuonyesha msisitizo...hivyo ni tatizo la kiteknologia si nia yangu kufanya hivyo...
 
Ndugu Kishaju,

Karibu sana JF. Una maana gani hapo juu? Kuna kitu kinaitwa plagiarism, unakifahamu?


Ndugu yangu samahani yaani nilikuwa najaribu ku-quote kumbe pale juu nikafuta ndo maana ikaonekana kama vile imetoka kwangu...sikuwa na nia ya kuifanya kama "my original idea" Nilikuwa nataka nichambue baadhi ya vipengele ambavyo nimeviona vinanifurahisha.

Kwa hiyo ndugu yangu usinielewa vibaya...nina masaa chini ya 24 tangu nimeingia hapa...bado niko kwenye kujifunza...

Bila shaka umenielewa...hivyo sikuwa na nia ya kuiweka kama "original idea" yangu...nilikuwa nataka kuonyesha msisitizo...hivyo ni tatizo la kiteknologia si nia yangu kufanya hivyo...

Ndugu Kishaju,
Pole kwa tatizo la kushindwa kunukuu.
Ukitaka kumnukuu mtu, (quote) fanya hivi,
1. bonyeza "Quote",iliyo chini ya posti ya huyo unayetaka kumnukuu maoni yake.
2. Kutakuwa na maandishi uliyonukuu, sasa wewe andika chini kabisa ya maandishi hayo pahala penye nafasi tupu.
3. Ukishamaliza kuandika maoni yako, Bonyeza "Post reply"Mpaka hapo utakuwa ushamnukuu mtoa maoni na maoni yako yataonekana chini yake.
 
Ndugu Idimi, nashukuru sana kwa maelekezo yako...yatanisaidia sana...bila shaka na Mbalamwezi atakuwa ameelewa kwamba sikuwa na nia mbaya ni katika kujifunza...
 
Ndugu Idimi, nashukuru sana kwa maelekezo yako...yatanisaidia sana...bila shaka na Mbalamwezi atakuwa ameelewa kwamba sikuwa na nia mbaya ni katika kujifunza...

Bila shaka ndugu yangu Kishaju!
Hakuna aliyeingia hapa JF na kujua kila kitu kwa siku moja, utagundua kwamba kadri unavyizidi kuwa hapa ndio unajifunza jambo jipya kila siku. Hii ni kawaida kabisa.
Sasa basi ili kuthibitisha kama umenielewa, hebu ninukuu mimi kwa kufuata maelekezo hayo hapo juu
Good luck!.
 
Pope,
Hata kichaa anaweza kuona kuwa kujitetea kwa Lowassa sio majibu yanayotakiwa na wananchi hata kidogo...
1. Anapodai kusikia minong'ono mitaani kwani hakujua kulikuwa na nyaraka zinazojieleza wazi zaidi ya minong'ono?...soma report ya Mwakyembe.
2. Alipowaita wakuu wa Idara ni maelezo baada ya mkataba kuwa signed, sisi tunachouliza na hata hiyo report inachokizungumzia ni nani walioshinikiza Richmond kupewa Tender hali hiyo ni kampuni bandia.
3. Huo mwezi September na October anaodai ktk maelezo yake tayari, Richmond walishakubaliwa kuingiza generators nchini..Nini mchango wake kabla ya hapo?
4. Alipoulizwa bungeni kuhusiana na Mkataba wa Richmond, kwa mdomo wake aliliambia bunge hakuna matatizo yoyote ktk mkataba wa Richmond hata baada ya vyombo vya habari kufichua ukweli kuhusu Richmond...Hivyo basi ni wakati gani alitumia nafasi yake kama Waziri mkuu kupata uhakika wa mkataba ule badala ya minong'ono...
5. Je, siii yeye aliyesema kwamba Kamati imetumia minong'ono kumsulubu walitakiwa kumwita yeye?.. mbona yeye pia ktk utekelezaji wa kazi yake alitumia Minong'ono kutengua Utafiti wa Wataalam kuhusiana na uwezo wa Richmond. Je, aliwaita wataalam hao kupata uhakika kimaandishi?... No! mbali na Taarifa ya Mwakyembe kudai kuwa zaidi ya mara mbili ofisi yake iliandikiwa barua.

He is guilty as hell!.. tena kama PrimeMinister ndio asiseme kabisa maanake anazidi kujichimbia kaburi...
 
Bila shaka ndugu yangu Kishaju!
Hakuna aliyeingia hapa JF na kujua kila kitu kwa siku moja, utagundua kwamba kadri unavyizidi kuwa hapa ndio unajifunza jambo jipya kila siku. Hii ni kawaida kabisa.
Sasa basi ili kuthibitisha kama umenielewa, hebu ninukuu mimi kwa kufuata maelekezo hayo hapo juu
Good luck!.

Ahsante sana kwa maelekezo...naituma kuona kama nimeweza kuelewa...kwa pamoja tutaushinda ufisadi Tanzania.
 
Pope,
Hata kichaa anaweza kuona kuwa kujitetea kwa Lowassa sio majibu yanayotakiwa na wananchi hata kidogo...
1. Anapodai kusikia minong'ono mitaani kwani hakujua kulikuwa na nyaraka zinazojieleza wazi zaidi ya minong'ono?...soma report ya Mwakyembe.
2. Alipowaita wakuu wa Idara ni maelezo baada ya mkataba kuwa signed, sisi tunachouliza na hata hiyo report inachokizungumzia ni nani walioshinikiza Richmond kupewa Mkataba.
3. Huo mwezi September na October anaodai ktk maelezo yake tayari, Richmond walishakubaliwa kuingiza generators nchini..Nini mchango wake kabla ya hapo?
4. Alipoulizwa bungeni kuhusiana na Mkataba wa Richmond, kwa mdomo wake aliliambia bunge hakuna matatizo yoyote ktk mkataba wa Richmond hata baada ya vyombo vya habari kufichua ukweli kuhusu Richmond...Hivyo basi ni wakati gani alitumia nafasi yake kama Waziri mkuu kupata uhakika wa mkataba ule badala ya minong'ono...
5. Je, siii yeye aliyesema kwamba Kamati imetumia minong'ono kumsulubu walitakiwa kumwita yeye?.. mbona yeye pia ktk utekelezaji wa kazi yake alitumia Minong'ono kutengua Utafiti wa Wataalam kuhusiana na uwezo wa Richmond. Je, aliwaita wataalam hao kupata uhakika kimaandishi?... NO! mbali na Taarifa ya Mwakyembe kudai kuwa barua zaidi ya mara mbili ofisi yake iliandikiwa barua.

He is gualty as hell!.. tena kama PrimeMinister ndio asiseme kabisa maanake anazidi kujichimbia kaburi...


Heshima kwako Mkuu,
Kulikuwa na ushahidi wa kujitosheleza sana kwa tume kumhusu Lowassa (nasisitiza kwamba wanaobisha hili wasome ripoti ya Mwakyembe hapo juu). Nisiongee zaidi kwa sababu umemaliza kila kitu hapo juu!
 
Back
Top Bottom