Lowassa afunika dar

Lowassa afunika dar

JK anawasiwasi kwamba akimrejesha jamaa anaweza kumgeuzia kibao.
PM anakuwepo kwa mujibu wa sharia labda akubaliane na fitna za akina Membe again...ila kwa sasa kama nchi tunamuhitaji Lowassa, ukiangalia kwa makini karibu kila wizara na idara zimeparalise... serikali iko likizo, PM PINDA hajui alifanyalo...
 
Kwa wenye akili ya senene lazima watasifia sana huyu Mwizi.
 
Ndo ivyo makamanda wenzangu.Sisi tuko bize na mabishano,mwenzetu anapita njia za panya.Jamaa kajipanga,yani hatanii amedhamilia kushika MADARAKA.Ameshajua udhaifu wa watanzania,sasa ndo anatumia vizur fulsa.MBOWE,SLAA,na makamanda wengine take care.DISCO LIMEINGIWA NA MMASAI.
 
Akigombea Lowasa 2015 ntahakikisha Mimi na rafiki zangu wapatao 100 tunampigia kura za Ndiyoooo
 
Laana ya mwlimu nyerere kwani nyerere ni mama ama baba wa lowasa? Nyerere sio Mungu, alikuwa n mazuri na mabaya yake. mojawapo ya baya ni kumhukumu lowassa on public hata bila ushahidi, na alipotakiwa apeleke ushahidi kamati kuu ya ccm, nyerere alishindwa akabakia kusema sina ushahidi lakini huyu kijana simtaki. Nyerere kama angekuwepo leo asingekuwa tofauti na mzee mtei kwa sababu bado alikuwa na nguvu ccm wakat hana cheo

Tatizo la nyerere alikua na wivu wa maendeleo... alipenda watz 2we masikini daima.
 
Wungwana....katika nchi ambayo kila mtu hata Mawaziri na W/mkuu aliyepo anailaumu SERIKALI...ni jambo la kushangaza na kustabisha kabisa.

Hata huko Ulaya au America walikopiga HATUA za maendeleo.... UONGOZI, USIMAMIZI SAHIHI au EFFECTIVE MANAGEMENT ndio SILAHA YAO KUU. Waweza kuwa na kuwa na MIPANGO BORA KABISA NA FEDHA ZA KUFANYA YOTE MAZURI...kama HII Serikali ya CCM ilivyo na mipango BORA na fedha....LAKINI KAMA HATUA NIDHAMU YA KAZI NA MATUMIZI YA HIZO FEDHA NI KAZI BUREEEEEEE.

Ni ajabu kumwona Waziri, au Mkurugenzi wa Halmashauri au wa shirika eti analaumu Serikali kwa kushindwa. HIVI SERIKALI NI NANI HASA?????

K
inachohitajika HAPA TZ ni KIONGOZI THABITI mwenye UWEZO wa KUVUNJA MFUMO HUU WA KUJUANA SERIKALINI na kuogopana uliodumu kwa zaidi ya miaka 50.

Hata akija Lowasa/Dr. Slaa/ Migiro /Mwakyembe au hata NANI UNAYEMJUA...bila KUVUNJA MFUMO HAKUNA KITU.

JK ameshindwa...
coz anateua watu kwa kuangalia mtandao/urafiki/undugu/ujirani/uchama n.k Hana uwezo wa kuwakemea kama alivyokuwa anafanya NYERERE na Sokoine.

Nchi inahitaji KIONGOZI JASIRI anayeweza kufanya maamuzi SAHIHI kwa wakati sahihi bila kuangalia mtu/urafiki/uchama n.k

Namkumbuka sana SOKOINE. Alikuwa mwananchi mzalendo sana.

Ni mtazamo wangu tu.
Nakubaliana na wewe ila kwa mujibu wako unaonekana unasema hakuna solution nchini. Mimi bado naamini kwamba mtu asiye rafiki wa hawa watu anaweza kuvunja mitandao yao. Kwa CCM ni Mwakyembe tu. Kina Dr. Slaa wanaweza maana wameonesha nia toka wako Bungeni, sasa sijui kwa nini sasa hivi tu doubt nia yao.

Lowassa ni mwizi tu. Anachokifanya ni kutafuta watu wepesi (cheap Tanzanians) kama boda boda...afu anasema boda boda oyeee! hivi katika karne hii unaweza kumwambia kijana wako kwamba bodaboda oyee??? kwamba tutafanya harambee hili kuongeza bodaboda? hii si sawa sawa na kuwambia wanafunzi kwamba tutaleta div. 5 hili kila mmoja ashinde ifikapo 2015? Huyu anaonga watu kwa njia ya kisasa. Anacheza na mawazo yao kwa sababu watu wenyewe hawajitambui. Dawa ya umaskini sio kumugawia kila mtu hela au gari au nyumba. Hili si tatizo letu Tanzania. Tatizo ni kwamba watu wachache, akiwemo yeye Lowassa, wanaliibia taifa na hivyo tunakosa maisha bora, yaani shule za kuandaa vijana kujitegemea, hospitali safi, barabara na matokeo yake tunakuwa na jamii ilojaa div.5 au madreva wa bodaboda...ambao Lowassa anawapenda (kwa mujibu wake). Huu ni ujinga at its best. Lowassa anatoa rushwa kwa watu cheap.

Nakuhakikishia watanzania mkifanya mistake, Lowassa atawafanya mumuone Kikwete kama geneous. Mkataeni haraka.
Nahisi anapoteza fahamu akiwa anaongea...angalieni video yake (bodaboda). Huyu mtu anahararisha umaskini.
 
Hivi watanzania sisi mazuzu nini? Hivi akili zetu ziko sawa kweli? Napata wasiwasi, acha niseme, mwenye kupinga alete hoja sio kubwabwaja tu.
Kwa akili ya kawaida tu tena isiyohitaji darasa, kiongozi anayetumia pesa au utajiri wake kupata uongozi anafaa kwa nchi kama hii? Kutumia pesa huenda isiwe tatizo, swali ni je, kama kiongozi, pesa yote hiyo anayotapanya kaipata wapi?? Hivi hatuwezi hata kufikiri kuwa ni kodi zetu hizi hizi zinazokatwa kwenye mishahara yetu au katika bidhaa tunazouza na kununua?? Unashabikia nini kama sio ujinga uliokithiri? Na kwa akili ndogo tu unadhani mtu huyu ana upendo saaana na watu hata atapanye pesa bila hesabu? Ujue kila shilingi anayotoa akipata nafasi anayotafuta atairejesha mahali pake na riba juu! Cha ajabu mtu anashabikia ujinga hapa bila kujua gharama za maisha source ni nini kwa huduma za msingi kama umeme kuwa ghali sana, mnadhani yeye anakisima cha pesa, ni hizo hizo kodi za masikini maana matajiri kodi hawalipi, wanalipa rushwa yenye discount. Nani aijenge nchi kama mawazo yetu ni mgando kiasi hiki pamoja na kwenda shule?
Hivi kwa akili ya kawaida tu, mwalimu JK aliposema umasikini wa mawazo ndo mbaya kuliko wote alimaanisha nini? Simple, alimaanisha katika hiki ambacho huyu mtu mnayemshabikia anacapitalise on, yaani fikra mgando.
Oh ni jasiri na anauthubutu, thibitisha. Acha kushabikia bila kutafakari, nchi hii ni tajiri lakini watu wake walio wengi ni masikini, hivyo usitegemee bepari akamkumbuka masikini.
Mwalim aliuliza Ikulu kuna biashara gani? Sasa ole wa TZ huyu mtu akipata nafasi hiyo, nawahakikishieni pesa zooote alizomwaga kwa viongozi uchwara wa dini wasiomjua Mungu na kwa watu au makundi ya watu tutazilipa mara 100 zaidi, hakuna tajiri anayetupa pesa, hayupo.
Kwa ujumla nchi hii bado haijapata mzalendo wa aina ya kizazi cha akina nyerere, sokoine, kawawa, n.k. ila tusubiri wakati utaamua, ila ushabiki wa kijinga kumsufia mtu anayejulikana public kuwa hafai, ambaye hata boss wake alimkataa waziwazi (mwalim JK), ni mawazo mgando yasiyo na tija kwa taifa letu.

Mkuu umemaliza kila kitu na sioni cha kuongeza!
Watanzania tu wavivu wa kufikiri na wasahaulifu wa kutupwa! Haiingii akilini kumshabikia mhalifu ambaye katika nchi za watu walio 'serious' na maendeleo yao alipaswa kuhukumiwa kunyongwa kwa madhira aliyoliletea taifa hili.
Ni Lowassa huyuhuyu aliyelitumbukiza taifa kwenye tatizo kubwa la umeme linalolisumbua taifa na litakaloendelea kulisumbua kwa miango mingi ijayo wakati yeye, familia yake na rafiki zake wakiendelea kunawiri! Watanzania wanalalamikia kupandishwa kwa gharama za umeme huku wakimshabikia 'mchawi' aliyesababisha madhira yote hayo! Lowassa na genge lake bado wanaendelea kupata migawo ya rushwa toka makampuni yaliyohusika na rushwa, na ni huyuhuyu; genge lake wakiwemo vibakauchumi mapapa walioko ndani ya chama lao la CCM walionunua pia hisa kwenye makampuni mbalimbali yakiwemo ya mawasiliano na kupata mgawo mkubwa huku wakiwakingia kifua wasilipe kodi! Wakati wenzetu jirani makampuni ya mawasiliano ndiyo yameshika usukani katika uchangiaji wa pato la taifa sisi huku hayamo hata katika ishirini bora! Yanapitwa hata na makampuni ya ulinzi kama Group 4!
Si kwamba hawalipi, ila wanagawana kodi yetu na wahalifu hawa.
Watanzania ni nani aliyeturoga?
Kwa ushabiki wa kijinga namna hii ipo siku nchi itaangukia mikononi kwa majambazi kama hili ambalo sehemu salama kwake ni Segerea, Ubena na magereza kama hayo.
Ushabiki umewahi kuiletea dunia matatizo yaliyoacha makovu yanayoonekana hadi leo kama pale kwa ushabiki wajerumani walipomweka Adolf Hitler kuwa kiongozi wao! Kilichotokea nadhani wengi tu tunakielewa. Na sasa kwa ushabiki wa kijinga huu huu tunataka kuiingiza nchi mikononi mwa majambazi na wauaji wakubwa!
 
Last edited by a moderator:
we kwanza nani kakupa ruhusa yakuchngia yasiyo kuhusu,manake we ni muahamiaji haramu,ile operation kimbunga bado haijakufikia,mambo ya nchi yetu tuachie sis watanzania tuamuwe,nenden kwanza mkasuluhishe ugomvi wenu na alshabab

mkuu tumia ubongo kufikiri. Huyu jamaa nyerere alimkataa, iweje leo mnashabikia?
Pia ujitambue kuwa mambo operation kimbunga si yakutolea mifano, maana imeacha sifa mbaya kwa viongozi
 
Nakubaliana na wewe ila kwa mujibu wako unaonekana unasema hakuna solution nchini. Mimi bado naamini kwamba mtu asiye rafiki wa hawa watu anaweza kuvunja mitandao yao. Kwa CCM ni Mwakyembe tu. Kina Dr. Slaa wanaweza maana wameonesha nia toka wako Bungeni, sasa sijui kwa nini sasa hivi tu doubt nia yao.

Lowassa ni mwizi tu. Anachokifanya ni kutafuta watu wepesi (cheap Tanzanians) kama boda boda...afu anasema boda boda oyeee! hivi katika karne hii unaweza kumwambia kijana wako kwamba bodaboda oyee??? kwamba tutafanya harambee hili kuongeza bodaboda? hii si sawa sawa na kuwambia wanafunzi kwamba tutaleta div. 5 hili kila mmoja ashinde ifikapo 2015? Huyu anaonga watu kwa njia ya kisasa. Anacheza na mawazo yao kwa sababu watu wenyewe hawajitambui. Dawa ya umaskini sio kumugawia kila mtu hela au gari au nyumba. Hili si tatizo letu Tanzania. Tatizo ni kwamba watu wachache, akiwemo yeye Lowassa, wanaliibia taifa na hivyo tunakosa maisha bora, yaani shule za kuandaa vijana kujitegemea, hospitali safi, barabara na matokeo yake tunakuwa na jamii ilojaa div.5 au madreva wa bodaboda...ambao Lowassa anawapenda (kwa mujibu wake). Huu ni ujinga at its best. Lowassa anatoa rushwa kwa watu cheap.

Nakuhakikishia watanzania mkifanya mistake, Lowassa atawafanya mumuone Kikwete kama geneous. Mkataeni haraka.
Nahisi anapoteza fahamu akiwa anaongea...angalieni video yake (bodaboda). Huyu mtu anahararisha umaskini.

sasa unalia liaa nn,manake hata familia yenu inamkubali lowassa,sema tu ww ndo umekuwa kicnwa ngumu,lakin hatushangai,manake ili jamii itwe jamii lazma watu kama ww wawepo
 
Msaliti huyo hafai kabisa anapenda sifa anauma anapuliza unakataa posho kumbe unavuta mkono wa pili huo si unafiki
 
Imedhihirika leo kwamba mh Edward Lowassa sio tu kwamba anapendwa bali pia ni tegemeo kubwa kwa watanzania wanyonge na wa hali ya chini.
Umati wa watu ambao haujawahi kuonekana pamoja na waendesha bodaboda wapatao elfu zaidi ya elfu ishiriki wamejumuika nae leo wakati alipokaribishwa kuwa mgeni rasmi wa chama chao.


Huyo ndiye Laigwanan Edward N. Lowassa.

Kusema kweli makundi ya vijana wanampenda. Ukipita vijiweni utasikia wakisema kwamba Lowassa ni jembe. Yeye na Magufuli ndio tegemeo la vijana wanaiunga mkono CCM na hata wasioiunga mkono.
 
Zito ni sawa na Mandela kwa kusimamia kile anachoamini. Mambo ya kusema usaliti hayana mashiko, mtu akipanga mkakati wa kutaka uongozi wa juu kidemokrasia anaitwa msaliti. Eti anataka kufanya mapinduzi! Mapinduzi ni ile hali ya kumwondoa mtu kwenye uongozi kabla ya muda lakini kama unapanga kuingia kwa njia ya kidemokrasia halafu unaita huo ni usaliti - Nadhani hicho kitu wanaweza kuelewa baadhi ya watu wa Kaskazini na misukule yao.
 
Back
Top Bottom