Lowassa afunika dar

Lowassa afunika dar

Baadhi ya Watanzania vichwa vyao vipo kama vya samaki!wanakaangwa na mafuta yao wao wanaendelea kusifia Lowasa Jembe! Inashangaza hawajiulizi hao watu wanaochanga hizo hela wanazipata wapi?hwajiulizi atazilipaje? Kama anauwezo alipokuwa PM mbona shida hizi hizi zilikuwepo? Machinga mlifukuzwa kariakoo wakati akiwa PM?Wamasai wenyewe huku munduli wanakunywa maji kwenye madimbwi, maji wengine wanafuata zaidi ya kilomita 5 au 10. Mnaota tu Lowasa asahau uraisi. Lowasa hana nia njema na nchi hii. Sijaona raisi anayegawa rushwa aitendee nchi meme. Ikipita harambee watoa rushwa wanafuatia. Acheni ujinga, mnaomsifia Lowasa sijaona tofauti na Wale Jamaa zangu wa CCM walioambiwa vichwa Kama samaki na Mheshimiwa Karume. Naamini CCM watamchinjia mbali na atatokwa na machozi siku hiyo. Lowasa akiwa raisi nchi hii itakuwa kama Mexico, wauza unga watatumaliza.

kumbe naww una wivu kama mama yako mzazi!!!!!!!
 
Njaa na ujinga vitatumaliza,,wanasiasa wanatumia mwanya huo na pesa za wizi kutupata,nilishangaa ila wenye akili wanajua
 
We jamaa usitudanganye lowasa haku sign deal ya richmond..aliwajibika kwa namna mchakato ulivyoendeshwa..mkuu wako..ukitaka jua uwezo wa lowasa angalia kipindi chake xha uwaziri mkuu nchi ilikua vp...na kama unadai ni fisadi leta data za ufisadi wake sio porojo tu..jamaa ni jembe na unao uwezo wa maamuzi ambao mkuu wenu hana..na km akiwa na afya njema nn hakika akigombea anapata sio kwa sababu anapendwa bali anaweza.
Na kilichomfanya ajiuzuru ni nini? Utatwambia aliacha sheria ichukue mkono wake au alipisha upelelezi. Ila ntaongeza swali lingine, kwani upelelezi umeisha? si aendelee kupisha upelelezi? Mbona anakuja?
 
Na kilichomfanya ajiuzuru ni nini? Utatwambia aliacha sheria ichukue mkono wake au alipisha upelelezi. Ila ntaongeza swali lingine, kwani upelelezi umeisha? si aendelee kupisha upelelezi? Mbona anakuja?

tulia ww upakatwe acha wivu
 
Ufisadi wa Lowassa huu hapa:

1. Kununua jumba la kifahari London, Uingereza, lenye thamani ya zaidi shilingi bilioni 1 za Tanzania

Metropolitan police wa Uingereza wanachunguza suala hili. Wamewasiliana na anti-money laundering unit ya Tanzania kuchunguza suala hili.

2. Ufisadi wa Nyumba ya Sanaa

Lowassa ni mhusika mkuu wa kufanya uporaji wa ardhi ya Nyumba ya Sanaa iliyopo karibu na Serena Hotel (zamani Movenpik Hotel). Nyaraka zinaonesha yeye ni mmiliki wa kampuni inayojenga gorofa kubwa kwenye eneo hilo la Nyumba ya Sanaa.

3. Kujilimbikizia mali kwa kutumia ofisi ya umma


Akiwa kama kiongozi wa umma, Lowassa amejilimbikizia mali nyingi sana za thamani ya mabilioni ya shilingi. Mali alizo nazo haziendani na kipato chake kama kiongozi wa umma. Sheria ya kupambana na rushwa Tanzania iko wazi kuwa kiongozi wowote wa umma mwenye utajiri usioendana na mapato yake halali anastahili kufikishwa mahakamani. Kutokana na sera za kulindana na kuogopana, Lowassa, Andrew Chenge, na viongozi wengine wa umma hawajafikishwa mahakamani kwa kosa hili na PCCB. Pia kwenye fomu za kila mwaka za kutaja mali, Lowassa haja declare assets zake zote. Ana miliki Alphatel, Alpha Schools, Alpha House, apartment blocks Dar es Salaam, Arusha na nje ya nchi.

4. Land grabbing

Alipokuwa Waziri wa Ardhi enzi za utawala wa Mwinyi alihusika na uporaji mkubwa wa ardhi sehemu mbali mbali nchini.

5. Richmond

Lowassa ndiye aliyeagiza TANESCO waporwe madaraka ya kusimamia tenda ya umeme kinyume na sheria ya manunuzi, PPRA. Aliunda kamati ya makatibu wakuu na kusimamia kwa karibu majadiliano ya kamati hii na nRichmond na kuagiza wapewe tenda wakati Tanesco waliikataa Richmond kuwa haifai. Lowassa ndiye mhusika mkuu wa kashfa ya ufisadi ya Richmond ndio maana alilazimika kujiuzulu.


6. Need I say more?

Lowassa ni mchafu wa maadili. Anapenda sana mali, amejilimbikizia utajiri kuliko kipato chake halisi. Wafuasi wake wanamfanananisha na Jacob Zuma wa Afrika Kusini. Tofauti ya Zuma na Lowassa ni kuwa Zuma alifikishwa mahakamani na kusafishwa na mahakama. Lowassa apelekwe kortini kujibu shutuma za ufisadi, akishinda kesi ndio atakuwa amesafishwa kweli. Si kwa kutumia vyombo vya habari, viongozi wa dini mamluki, waendesha bodadola walio hoi na waandishi wa habari wenye njaa.
 
Ufisadi wa Lowassa huu hapa:

1. Kununua jumba la kifahari London, Uingereza, lenye thamani ya zaidi shilingi bilioni 1 za Tanzania

Metropolitan police wa Uingereza wanachunguza suala hili. Wamewasiliana na anti-money laundering unit ya Tanzania kuchunguza suala hili.

2. Ufisadi wa Nyumba ya Sanaa

Lowassa ni mhusika mkuu wa kufanya uporaji wa ardhi ya Nyumba ya Sanaa iliyopo karibu na Serena Hotel (zamani Movenpik Hotel). Nyaraka zinaonesha yeye ni mmiliki wa kampuni inayojenga gorofa kubwa kwenye eneo hilo la Nyumba ya Sanaa.

3. Kujilimbikizia mali kwa kutumia ofisi ya umma


Akiwa kama kiongozi wa umma, Lowassa amejilimbikizia mali nyingi sana za thamani ya mabilioni ya shilingi. Mali alizo nazo haziendani na kipato chake kama kiongozi wa umma. Sheria ya kupambana na rushwa Tanzania iko wazi kuwa kiongozi wowote wa umma mwenye utajiri usioendana na mapato yake halali anastahili kufikishwa mahakamani. Kutokana na sera za kulindana na kuogopana, Lowassa, Andrew Chenge, na viongozi wengine wa umma hawajafikishwa mahakamani kwa kosa hili na PCCB. Pia kwenye fomu za kila mwaka za kutaja mali, Lowassa haja declare assets zake zote. Ana miliki Alphatel, Alpha Schools, Alpha House, apartment blocks Dar es Salaam, Arusha na nje ya nchi.

4. Land grabbing

Alipokuwa Waziri wa Ardhi enzi za utawala wa Mwinyi alihusika na uporaji mkubwa wa ardhi sehemu mbali mbali nchini.

5. Richmond

Lowassa ndiye aliyeagiza TANESCO waporwe madaraka ya kusimamia tenda ya umeme kinyume na sheria ya manunuzi, PPRA. Aliunda kamati ya makatibu wakuu na kusimamia kwa karibu majadiliano ya kamati hii na nRichmond na kuagiza wapewe tenda wakati Tanesco waliikataa Richmond kuwa haifai. Lowassa ndiye mhusika mkuu wa kashfa ya ufisadi ya Richmond ndio maana alilazimika kujiuzulu.


6. Need I say more?

Lowassa ni mchafu wa maadili. Anapenda sana mali, amejilimbikizia utajiri kuliko kipato chake halisi. Wafuasi wake wanamfanananisha na Jacob Zuma wa Afrika Kusini. Tofauti ya Zuma na Lowassa ni kuwa Zuma alifikishwa mahakamani na kusafishwa na mahakama. Lowassa apelekwe kortini kujibu shutuma za ufisadi, akishinda kesi ndio atakuwa amesafishwa kweli. Si kwa kutumia vyombo vya habari, viongozi wa dini mamluki, waendesha bodadola walio hoi na waandishi wa habari wenye njaa.

haya yote uliyo yaaandka umeongozwa na wivu wa kike na chuki dhidi ha lowassa,kwa haraka haraka hapa tunasema hapa utakuwa umetumika kuja kumchafuwa Lowassa.Watanzania waote hakuna asiye juwa kuhusu issue ya richmond hili niww tu umejiondoa akili na kuendelea kuwa na kichwa kigumu kisicho elewa,lowassa alisha simamama kweny vikao vya ccm kuzungumzia suala la richmond,kama si busara za mzeee mkapa leo na wazee wengne wa ccm leo ingekuwa ni nadithi nyngne tunazungumzia,hizo hoja nyngne ulizo andka ni upuuzi mtupu ambao hata mtoto mdogo akisoma atajuwa tu kjwa punguani ndiye aliye andkam,suala lz lowassa kumiliki nyumba uingereza siyo zambi na hili mtoto wake alishazungumzia hili,na aksema hata kama nikweli wanamiliki nyukmba uk hizo shea wanazomiliki kwenye kampuni ya vda zenyewe tu zinztosha kununuwa nyumba uk,mbna mbowe ametumia fedha za ruzuku kununulia nyumba uk,s,afrika,usa,nairob hili ajawhi simama na kukanusha amebaki na makengeza yake kila siku kumwandama zitto kisa aliskia issue ya ukaguzi,hakuna aliyemsafi kiivyo mzee mtei mwenyewe ni kati ya watu waliohujumu uchumi wa nchi,nenda pae tengeru uwone alivyo jilimbikizia ardhi kuanzia tengeru analo shamba kubwa linalo fika hadi usa
 
Afunika kwa gharama za umeme kupanda?
akiya mungu lowasa analeta umaskini nchi hii,
 
Acha kujifurahisha tu ndugu yangu. Lowasa hana lolote. Hana vision wala mission. Yupo tu kugawa hela za rushwa ili awe raisi. Hela ni zaidi ya uraisi. He is the dead wood. Alipokuwa waziri mkuu niambie amefanya nini?Taja list ya mambo aliyoyafanya?

kama mpaka leo hujui lowassa aliyoyafnya akiwa wazir mkuu bs ww inabdi tukuchunguze hyo akili,cijui ndo zile division five za mulugo
 
Kwa maoni yangu, kwa mfumo wetu wa utawala wa demokrasia hii ya kurukia, yenye kujaa fitna, umbeya, ushabiki na chuki, hakuna mwenye uwezo wa kuthubutu atakayesimaa. Maige alithubutu kuwanyima wazungu vitalu. Maige alithubutu kufunga biashara ya wanyama hai na hivyo kuokoa twiga wetu. Walioathirika na maamuzi hayo wakampiga fitna na kwa nguvu ya mchezo mchafu kwa kamati, yakamkuta yaliyomkuta na leo watanzania wanaitikia chorus hiyo kuwa Maige alisafirisha twiga wakati yeye ndiye aliyewaokoa.

Kwa hakika, tusipokuwa na mfumo mzuri wa kuchunguza tuhuma kabla ya hukumu zinazoratibiwa kwa mob bungeni, kwa kushadidiwa na wabunge ambao wengi wao wamethibitika kuwa si waadilifu (kwani wapo wanaochukua posho bila kusafiri na wengine wanaiba hata mikufu!!!), hakuna atakeyesimama.

Maamuzi yoyote magumu huumiza watu. Lazima uwepo mfumo wa kujiridhisha pale tuhuma zinapozuka kwa mtu, kwani mara nyingi wengi wanaoathirika na maamuzi hayo ya viongozi wazalendo hupanga njama za kuwaangamiza wachapakazi.


Leo tunamkumbuka sana Sokoine (kwa vita ya uhujumu uchumi na ulanguzi) na Mzee Kawawa kwa operesheni vijiji. Wote hawa walisababisha madhara makubwa kwa watu. Wapo watu waliotupa mali zao kwa kumwogopa Sokoine. Kama mfumo ungeruhusu majungu, Sokoine angepigwa jungu moja tu na asingesimama tena!!

Kawawa kadhalika, watu waliliwa na simba porini na wengine waliteseka kwa kuvunjiwa nymba zao na kuishi chini ya miti wakinyeshewa mvua, lakini kwa kutokuwepo akina Hellen Kijo Bisimba, alipona. Ajaribu leo tuone!!! Hatamaliza wiki.

Kwa kuwa nyakati zimebadilika, nasi lazima tubadilike, vinginevyo, wazuri wote wataisha, watabaki wasanii wenye kwenda na wakati na upepo!! Pale wazee wakitaka gesi yote ivunwe na wageni wataimba wimbo huo kwa nguvu zao zote, lakini akija mtu akasema anataka watanzania wapate kipaumbele kwenye gesi yao, nao watageuka na kuimba wimbo huo kwa nguvu zao zote!!

Tunahitaji watu ambao they are solid na wazalendo wa kweli!??

lakini kumbukeni
Wungwana....katika nchi ambayo kila mtu hata Mawaziri na W/mkuu aliyepo anailaumu SERIKALI...ni jambo la kushangaza na kustabisha kabisa.

Hata huko Ulaya au America walikopiga HATUA za maendeleo.... UONGOZI, USIMAMIZI SAHIHI au EFFECTIVE MANAGEMENT ndio SILAHA YAO KUU. Waweza kuwa na kuwa na MIPANGO BORA KABISA NA FEDHA ZA KUFANYA YOTE MAZURI...kama HII Serikali ya CCM ilivyo na mipango BORA na fedha....LAKINI KAMA HATUA NIDHAMU YA KAZI NA MATUMIZI YA HIZO FEDHA NI KAZI BUREEEEEEE.

Ni ajabu kumwona Waziri, au Mkurugenzi wa Halmashauri au wa shirika eti analaumu Serikali kwa kushindwa. HIVI SERIKALI NI NANI HASA?????

K
inachohitajika HAPA TZ ni KIONGOZI THABITI mwenye UWEZO wa KUVUNJA MFUMO HUU WA KUJUANA SERIKALINI na kuogopana uliodumu kwa zaidi ya miaka 50.

Hata akija Lowasa/Dr. Slaa/ Migiro /Mwakyembe au hata NANI UNAYEMJUA...bila KUVUNJA MFUMO HAKUNA KITU.

JK ameshindwa...
coz anateua watu kwa kuangalia mtandao/urafiki/undugu/ujirani/uchama n.k Hana uwezo wa kuwakemea kama alivyokuwa anafanya NYERERE na Sokoine.

Nchi inahitaji KIONGOZI JASIRI anayeweza kufanya maamuzi SAHIHI kwa wakati sahihi bila kuangalia mtu/urafiki/uchama n.k

Namkumbuka sana SOKOINE. Alikuwa mwananchi mzalendo sana.

Ni mtazamo wangu tu.
 
mh maige tunaomba kwa heshima ya jamvi,utueleze ile move ya twiga ilikuwaje?
 
Back
Top Bottom