Vikao vya Harusi
JF-Expert Member
- Sep 19, 2012
- 532
- 165
Wewe mkono wako ni wa mjinga. Unaandika popote na lolote. Wewe familia yangu unaijua? Tumkubali Lowassa kwa lipi? Huyu angekuwa China angeishanyongwa, angekuwa Marekani, angekuwa jela na asingeingia kwenye siasa tena. Hapa Tanzania anategemea huruma ya watu kama wewe and the likes.
Najua unalipwa kuandika hivi ila watoto wako hawatalipwa na watakuwa watumwa kwenye taifa lao endapo huyu mtu atapata anachokitafuta. Natumia maneno ya waziri mstaafu, Fredrick Sumaye, "watanzania msipokuwa makini mtawakabidhi nchi wauza msdawa na mitandao yao" hels wanazogawa kwenye nyumba za ibada wanazipata kwa njia hizo na watazirudisha pindi wakimweka mwenzao. Sasa mimi na familia yangu tukubali nini hapo?
Kumbuka huyu mtu alishajiuzuru kwa kukubali kuliingiza taifa gizani hili ajipatie hela, ndugu yangu wewe ndo unaona ni mtu shujaa huyo?
Lakini si nyie nyie mlopewa kofia na kanga mkaona JK anawapenda? Endeleeni kuchimba ksburi. Kumbuka yupo Mungu pia.Kwa Mungu, Anayeliibia taifa mammilion kwa siku, anayepokea kofia na kanga, anayepewa boda boda, wote ni sawa....hivyo msidhani mtamnyooshea kidole Lowassa baada ya mambo kugeuka. Kama Mungu akimwadhibu Lowassa, hatawaacha ninyi pia.
Nchi ya Haiti maovu ya kushabikia ujinga kama huu yalikuwa yamefika mwisho. Watu kama Lowassa, wewe walikuwa wamejaa huko. Ilitumia sekunde 35 tu kuleta kilio kwa taifa lile. Sekunde 35. Si mtoto, si baba, si mama, si mzee....hakukuwa na kuchagua. Wote waliangamia.
Si huko tu, taifa za Burundi na Rwanda. Hawa nao ujinga wa chuki uliwafikisha kukatana mapanga na hakuna taifa lililoingilia kuwaokoa mpaka wakachoka.
Rafiki yangu, sidhani kama unaelewa naandika nini kwa jinsi ninavyokuona. Kina Lowassa wakishaipata nchi wataweka watu wao kuabzia usalama taifa hadi balozi wa nyumba kumi. Kama alivyofanya JK. Angalia usalama ulivyo sasa hivi.
Wakishafanya hivyo, hiyo pesa yao itarudi na wewe na mimi ndo tutailipa. Hutalalamika kwa sababu wao hawatatoa kucha na meno tu, watakuwa wanaua live hili hela yao irudi. Umeme tutalipa kwa bei wanayoitaka wao. Haitakuwa nchi tena. Kama unadhani sasa hivi nchi yetu inasifika kwa kuuza madawa, subiri hawa nashujaa wako waje. Watakuwa wanayasafirisha wenyewe na kwa sababu hiyo, tofauti kati ya tajiri ja maskini itakuwa kubwa muno. Hii ndo italeta machafuko nchini kwa sababu hata ukipewa buku 7, hazitakusaidia lolote kutokana na mfumuko wa bei. Utawala wa Lowassa hautakuwa na wapinzani. CDM, CUF na wengine, mkifanya mchezo huu ndo mwisho.
Sasa mimi na familia yangu kama unavyosema, tujue haya na tumkubali Lowassa? Hata inchi moja. Naipenda nchi yangu, napenda watu wake na zaidi naipenda familia yangu na kumwogopa Mungu, hivyo namkataa Lowassa kaka.
China ipi,? Ile yenye lilie kundi ovu la YAKUZA,ambao ni twin brothers na redbrigade