Lowassa afunika dar

Lowassa afunika dar

Huyu mtu alijiuzulu kwa ufisadi, habari ndiyo hiyo!

Hata apokelewe na kadamnasi ya watu, huo ni ukweli usiopingika.

Ni mchafu hasafishiki!!!
Mkuu,
Hebu isome vema avatar yangu, uielewe.
 
Lowassa ni fisadi tu, hana jipya. Anatumia pesa kununua kuungwa mkono na watu wenye fikra finyu. Ameshajua kuwa tatizo la watanzania ni njaa na akili finyu, ukiwamwagia pesa wanakulamba mpaka miguu.

Huyu ana laana ya Mwalimu Julius Nyerere. Hana maadili na uzalendo wa kuwa kiongozi ambaye Tanzania inamuhitaji. Ana husudu sana mali na wafuasi wake wakubwa ni kina Rostam Aziz, Andrew Chenge, Prof. Juma Kapuya, Deo Filikunjombe, Makongoro Mahanga, Vita Kawawa, Peter Serukamba na Zitto Kabwe.
 
Watanzania wote tupimwe akili huenda hatujitambui!

Mara hii ya Lowassa wameshayasahau!

Mkuu wewe ni mnyruanda? Watanzania ni tofauti na wananchi wa nchi nyingine, hawajawahi kumkataa mtu hata wewe ukitaka kuwa kama lowassa ma zitto, u can any time. Ndio maana unaweza kuona mtu kama mnyika, nassari hawakuwa na hela lakini watanzania wakawapokea.

Kilichomkuta lowassa ni ajali tuu ya kisiasa, kama ambavyo slaa amepotea ghafla hana umaarufu tena
 
Huyu mtu alijiuzulu kwa ufisadi, habari ndiyo hiyo!

Hata apokelewe na kadamnasi ya watu, huo ni ukweli usiopingika.

Ni mchafu hasafishiki!!!

Ni wazi hao waendesha bodaboda wamepewa pesa wajae mtaani kumuonesha Lowassa eti kama mtu anayependwa na wananchi. Hatujasahau ufisadi wa Richmond na mali za umma alizojilimbikizia, ikiwemo mahekaru lukuki masaki.

Ameona kuna mabadiliko ya baraza la mawaziri yanakuja ndio anajitokeza aonekane bado yupo JK amrudishe kwenye Cabinet. Kikwete ni mjanja sana, kamwe hawezi kudanganywa na hizi political gimmicks za kitoto za Lowassa wa ufisadi wa Richmond.
 
Lowassa ni fisadi tu, hana jipya. Anatumia pesa kununua kuungwa mkono na watu wenye fikra finyu. Ameshajua kuwa tatizo la watanzania ni njaa na akili finyu, ukiwamwagia pesa wanakulamba mpaka miguu.

Huyu ana laana ya Mwalimu Julius Nyerere. Hana maadili na uzalendo wa kuwa kiongozi ambaye Tanzania inamuhitaji. Ana husudu sana mali na wafuasi wake wakubwa ni kina Rostam Aziz, Andrew Chenge, Prof. Juma Kapuya, Deo Filikunjombe, Makongoro Mahanga, Vita Kawawa, Peter Serukamba na Zitto Kabwe.

Laana ya mwlimu nyerere kwani nyerere ni mama ama baba wa lowasa? Nyerere sio Mungu, alikuwa n mazuri na mabaya yake. mojawapo ya baya ni kumhukumu lowassa on public hata bila ushahidi, na alipotakiwa apeleke ushahidi kamati kuu ya ccm, nyerere alishindwa akabakia kusema sina ushahidi lakini huyu kijana simtaki. Nyerere kama angekuwepo leo asingekuwa tofauti na mzee mtei kwa sababu bado alikuwa na nguvu ccm wakat hana cheo
 
Rtz, humpendi huyu mtu ? Sijakuona ukichangia, mwana CCM mwenzako katokelezea.
 
Ukitulia na kutafakari kwa kina, unaweza usiamini kama Lowasa leo hii anaweza akapigiwa debe namna hii.
 
Nishasema zengwe lolote atakalo fanyiwa Lowassa ndani ya CCM ktk mbio zake za urais ni sawa na kumpitisha Slaa bila kupigiwa kura.
 
Duh naitishwa na harakati za lowassan lakini nimejifunz jambo kutoka kwa huyu bwana, kuhusu uvumilivu

Naungana na wewe, EL ni mvumilivu sana ila sina hakika na roho ya kusamehe na kutolipiza visasi.
 
...hata mimi ningekuwa na bodaboda ningeenda kuchukua mafuta ya bure na mkwanja nisogeze siku,kula ccm kura cdm kamakawa...
 
Mwana jamvi mmoja amewahi kusema: "PCCB imchunguze Lowassa kwa tuhuma za ufisadi. Sheria inasema kuwa kiongozi yeyote wa umma akiwa na utajiri wa mashaka (unexplained wealth) anatakiwa kupelekwa mahakamani kujibu mashitaka ya ufisadi. Je, Lowassa amedeclare mali hizi kwa Tume ya Maadili ya Uongozi? Je, Lowassa amepata wapi mali za mabilioni ya shilingi alizojilimbikizia wakati yeye ni kiongozi wa umma?" '

Nakubaliana kabisa na hoja hii, waendesha bodaboda wamsindikize Lowassa mpaka TAKUKURU ili ajisalimishe mwenyewe, kwani Dk. Edward Hoseah wa TAKUKURU kashasema yeye hana ubavu wa kuwapeleka mahakamani viongozi wakuu wastaafu (au waliojiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond kama Lowassa).
 
Back
Top Bottom