Loose ends Kifo cha Martha Towo

Loose ends Kifo cha Martha Towo

Labda pia walifanya hivyo makusudi kwa kumfeed lies ambazo zitapindisha uchunguzi.

Lets say wametumwa na Boss wake wa kazini lakini wao wanaenda kusema wewe si unajifanya unatembea na waume za watu, sasa ukome. Alafu anaachiwa akiwa hajafa vizuri ili kichwani kwake kuwe na nadharia wauaji wangu wananishutumu nilikuwa natembea na mme wa mtu. So obvious hata huko hospital na kwa wazazi akatoa kauli hiyo hapo tayari uchunguzi unapindishwa
Uko smart
 
Macho yana lenzi ambayo hubaki na baadhi ya matukio ya mwisho, ndio maana kwenye mauaji baadhi macho hutobolewa ili kutoruhusu alama yoyote kuchukuliwa labda hauna ufahamu wa haya mambo au umefanya makusudi

Mkuu ulichoandika hapa beberu anaita optography. Hayo yameelezwa vizuri hapa:

Optography - Wikipedia

Almaarufu kwenye movies za kina James Bond huko.

Jiulize hizi image za mwisho zinakuwa wapi na zinakuwa retrieved na nini.

Kwenye case hii za mwisho ni zipi? Za moto, za kukimbia, Tumbi au za Muhimbili?
 
Wakati unamove kutoka Sumbawanga kwenda Kibaha tayari unaanza kuacha trace. Mwenye Boda utakayemtuma anaweza kutokuwa na Shaka pale ambapo yeye imethibitika kuwa hakuwahi kusafiri kipindi cha tukio. Pia ataeleza mazingira ya kuwa Kuna mtu alimsaidia tu kiutu. Pia kwa kuwa umekaa siku nyingi wanaweza kuanza kukutambua partial kwa jinsi tu ulivyo. Labda mfupi mweusi mnene (JAPO KWA MAZINGIRA YA BONGO HUYO BODA KAYAKANYAGA NA SIDHANI KAMA WANAFATILIA HIZI DETAILS). Baada ya hilo, wewe utakuwa ni unknown lakini kuna nuru inaanza kuonekana. Lakini kumbuka ulisafiri kwa njia gani? Labda usafiri binafsi, sawa twende umeshafika mjini. Wakati unakwenda tekeleza tukio unaweza kuwa umefikia wapi? Maana lazma usuke mpango wa kuchora ramani ya unayemtaka. Lain uliyosajiliwa inaweza toa ramani ni wapi ulipokuwa mara ya mwisho, umekaa kwa mda gani? Umefikia wapi. Yote haya yataanza kukufanya ujulikane kwa taratibu taratibu. Na hapo kwenye tukio bado kuna vitu vingi unaweza acha kama traces. Baam! Wamekukamata.

Muhimu Kabisa kwenye tukio lolote cha kwanza kabisa omba usishtukiwe maana unaweza kufatiliwa ama kufanywa namna ikakubidi uzungumze yote. Pia Unatakiwa ufanye tukio kwa ufanisi na kwa mda mfupi. Kadri unavyowazungusha kwenye kukung'amua ndivyo unavojiongezea muda ndivyo trails zinazidi kufutika.
Mkuu shida ni kwamba kwa nature ya tukio lazima lilihusisha watu wengi ila kama ingekuwa hit and run ingekuwa ngumu sana huyo mtu kudakwa.

Lets say, baada ya kutoka Kigoma unafika unafanya mawasiliano na chanzo chako then unamset atoke kanisani, akitoka anakula chuma then unapotea kusikojulikana unadhani ingekuwa rahisi kukamatwa??

Watabaki wakihangaishana na bodaboda kuelezea jinsi ulivyo lakini hiyo appearance yako ni wangapi wanayo Tanzania? Kosa ni kwamba ukija kukamatwa na boda akaletwa kukutambua hapo ndio inakula kwako. Lakini traces za kukukamata hazitakuwa ile simu bali vitu vingine kabisa
 
Usicheze na kahama na kahama kuna matajiri alafu wenye roho za ajabu?
Pili, huyu dada alikuwa mapepe?
Tatu, kabla ya kwenda kibaha alifukuzwa kwa sababu za kiofisi ijulikani ni utovu au mengine kiofisi.
Nne hakuwa na cheo hiko ni Afisa mikopo.
Tano, matukio ya kahama kesi za kufanyiana unyama zipo sana sio mapenzi,sio biashara na n.k.
Uzuri wa huyu dada inaonyesha alikimbia kuofia vitisho kwa mwanamke mwenzake au mapenzi?
Matajiri wengi wa huko wanautajiri bandia yaani utajiri wa ndagu.
Thus hawana ubunifu wowote nje ya biashara za kuigana tu.
Ukatili wao ni matokeo ya kujiconnect na nguvu za giza
 
Mkuu minara hata isome vipi, wewe ukishamaliza kazi simu inazimwa inatolewa line na kutulwa huko katikati ya msitu au hata kuchomwa moto.

Kumbuka huyo dogo aliyeenda kusajili hanifahamu zaidi ya kuniona sura tu. Huyo dogo atakuwa na msaada endapo nitakamatwa na yeye aletwe kubainisha nani alimsajilia line. La sivyo huyo dogo atasotea rumande na muuaji halisi asipatikane.
Hivi umeshawaona wale wabongo wanaochora picha za watu na zinatoka like picture za camera? Umeshawaza kama vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama vina watu wa namna hiyo? Akikaa na dogo wa bodaboda 8hrs nini kitatokea?
 
Kwao wapo wawili tu. Yeye na mdogo wake wa kiume. Lete uongo mwingine
Anaweza kua na ndugu wa baba mdogo na mkubwa ubini unakua ule ule, nimesoma comments karibu zote lakini ukweli hii kesi watuhumiwa kukamatwa ni rahisi sana sana. Marehemu kaishi siku 6, na wakati anaungua na kuokolewa aliweza hadi kukumbuka namba ya simu ya baba yake ili apigiwe, hapo tu inaonesha alikua na akili timamu hadi anapatwa na umauti. kingine, hao wauaji kitendo tu cha kutumia simu hilo ni big mistake.
 
Familia iko kwenye msiba mzito. Tunawapa pole. Ni kifo kinachotokana na mauaji hivyo hakiwezi kukosa mijadala na msingi wa hiki kifo cha mauaji lazima kiwe na sababu, kiwe na viashiria.

Kiwe na mhusika/wahusika wakuu
Kiwe na bajeti
Kiwe na watendaji/watimiza lengo. Kwa msingi huu wauaji
Kiwe na mpango kazi
Kiwe na fool proof
Kusiwe na dosari kuanzia kupanga, kutekeleza na hatimaye kutawanyika na kumalizana kama kuna malipo ya mwisho yalikuwa bado

Uchunguzi wa kifo hiki ni rahisi sana na si chini ya watu 20 wanaweza kuhusishwa nacho, ambapo watachujwa mpaka watabaki si chini ya watano .. Na ni uchunguzi rahisi kutokana na makosa mengi waliyofanya wauaji.. Hawakuwa wajuzi maana wajuzi huwa hawaachi alama! Japo kuna kosa moja dogo sana hufanya na kufumua mpango wote.

Uchunguzi wake utaanzia kazini kwake, maisha yake nje ya kazi, marafiki zake, wateja wake, mishe na dili zake, mawasiliano yake pamoja na mahusiano.. Hapa ni kwa ajili ya ku 'establish' Msingi wa kesi na 'motive' ya muuaji/wauaji.

Uchunguzi wa pili ni eneo lilikofanyika tukio.. Pori la Mitamba linalosifika kwa matukio ya mauaji, Mitamba halina tofauti sana na Mabwepande na kama linaweza kuchunguzwa vizuri kuna maiti ngingi mule zinaweza kuwa zimezikwa.

Mitamba liko Kibaha njia ya kwenda Bagamoyo eneo linaitwa Pangani.. Sehemu kubwa ya pori la Mitamba ni eneo la wizara ya mifugo na uvuvi na kuna kipindi matapeli wa viwanja Kibaha walilivamia na kuwauzia watu viwanja mpaka serikali ikaingilia kati.

Marehemu ni mkazi mwenyeji wa Kibaha Kwambonde kakulia hapo, kosoma Tumbi nknk. Wazazi wake wanaishi hapo mpaka sasa na ni watu unaoweza kuwaita maarufu eneo hilo na hata kanisani kwao Tumbi. Kwanini muuaji/wauaji wakachagua kuja kummaliza 'nyumbani kwao'?

Marehemu alisafiri salama salimini toka kituo chake cha kazi Shinyanga mpaka nyumbani Kwambonde Kibaha. Pengine alitumia ndege, usafiri binafsi au wa jumuiya lakini alifika salama.

Je, wauaji walikuwa wanamfuatilia kote huko?
Je, wauaji ndio walimuita aje Kibaha?
Je, lengo lake la kuja nyumbani Kibaha lilikuwa ninini?
Je, mpango wa kummaliza Kibaha pori la Mitamba ulikuwa mpango plan A au B?

Marehemu siku ya tukio alikuwa kanisani na ndugu zake.. Ni wazi alipata wito wa kuitwa nje mara moja ama kwa ishara ya mtu alikuwa ndani ya kanisa ama kwa simu kwakuwa mikoba yake aliacha alipokuwa kaketi. Hakurudi!

Ni wazi walimuita walikuwa nje kabisa ya kanisa barabarani! Kanisa la KKKT Tumbi liko pembezoni mwa barabara ya kuelekea Tumbi hospital. Ni wazi kulikuwa na gari ambalo ama alipanda kwa hiari ama kwa lazima/Kutekwa.

Ni wazi safari ilianza kuelekea Pangani pori la Mitamba.. Macho ya marehemu yata 'reveal' kilichotokea ndani ya gari kwa hicho kipindi chote mpaka kufika Mitamba kumwagiwa Petrol na kuchomwa moto!



Ukurasa wa pili juu ya mpango kazi ambao ninaamini ndio plan A.

Wauaji waliona eneo salama la kummaliza ni eneo la nyumbani alikozaliwa. Wauaji ni wenyeji wa Kibaha wanaofahamu vema jiografia ya Kibaha hasa eneo la Mitamba Pangani ambako hakuna doria za polisi, kuko kimya na mbali na makazi ya watu. Pia ni eneo lenye gate away nzuri kwahiyo ni rahisi kupoteza maboya mtu anayekufuatilia.

Unaweza kutokea Kimara
Unaweza kutokea Baobab
Unaweza kutokea Kibaha maili moja eneo la shell
Unaweza kutokea NIDA
Unaweza kutokea picha ya Ndege
Unaweza kutokea Loliondo nk na kote huko mtu asijue umetokea Mitamba Pangani

Kwa vyovyote mwenye mpango wake alikodi watu wa kumsaidia kuutimiza
  • Dereva
  • Mfuatiliaji aliyekuwa kanisani
  • Mtu aliyempatia sindano ya sumu
  • Backup
  • Hapa kuna watu wa kati hawakosekani
  • Malazi, kama watekeleza mpango walitoka mbali ni wazi walilala gesti za maeneo ya Kibaha ama jirani na Kibaha.
Loose ends/makosa ya kiutendaji yasiyotarajiwa
Wajuzi hufanya rehearsal hata zaidi ya mara tano kutegemeana na mlengwa na bajeti na kila rehearsal hugundua makosa kadhaa na kuyarekrbisha.

Je, makosa makubwa kwenye hili tukio ni yapi?

1. Mtandao wa mawasiliano simu na jumbe za sauti na maneno
2. Kuhusisha watu zaidi ya mmoja
3. Kutochagua wajuzi wa kazi
4. Kutofanya rehearsal
5. Kumchoma sindano ambayo haikuwa na sumu kali au ambayo haikuchomwa kwa usahihi
6. Kudhani amekwisha kufa hivyo kutengeneza fool proof ya kumchoma moto uliomzindua
7. Pengine kuondoka eneo la tukio haraka bila kuhakikisha ameungua vizuri
8. Macho kubaki salama, yalirekodi kila kitu

Kwa dondoo hizo hii kesi ni nyepesi kuliko ya bilionea Msuya ana yule mzungu wa tembo. Marehemu alibaki kuwa hai kuanzia tarehe 3 march mpaka 9 alipoaga dunia. Siku sita ni nyingi sana kuweza kupata na kujua mengi

Damu ya mtu ni nzito na inanuka! Harufu hukoma haki ikitendeka
ila kuna kitengo kule polisi cha shirki wakiona wanasumbua kuwapata wanawaweka kwenye chungu maalumu kuwachungulia na kuwazubaisha ufahamu hawatoki nje ya eneo walilofanya tukio au nje ya mipaka ya nchi waliyofanya tukio watabaki wanazunguka tu humu mpaka watakapokamatwa.. kazi za upelelezi noma sana..
 
Mkuu shida ni kwamba kwa nature ya tukio lazima lilihusisha watu wengi ila kama ingekuwa hit and run ingekuwa ngumu sana huyo mtu kudakwa.

Lets say, baada ya kutoka Kigoma unafika unafanya mawasiliano na chanzo chako then unamset atoke kanisani, akitoka anakula chuma then unapotea kusikojulikana unadhani ingekuwa rahisi kukamatwa??

Watabaki wakihangaishana na bodaboda kuelezea jinsi ulivyo lakini hiyo appearance yako ni wangapi wanayo Tanzania? Kosa ni kwamba ukija kukamatwa na boda akaletwa kukutambua hapo ndio inakula kwako. Lakini traces za kukukamata hazitakuwa ile simu bali vitu vingine kabisa
Ni kweli lakini vingi sijavizungumza. Nilichukua tu mfano wa scenario uliyoitoa. Hapo kwenye muhimu ndipo pana mantiki kubwa sana nimeijenga. Unaweza kulifanya tukio ukawa umeacha fingerprints ambazo zikipelekwa kwenye database kumbe upo Nida (natania). Tayari manjuga wanaanza kufurahia. Wanamleta boda anakuthibitisha. Wanakupeleka Lupaso unapokea dozi unaanza kutoa ramani yote ilivyokuwa. Unaenda mahakamani unapata wakili mzuri unashinda kesi. Case closed
 
Anaweza kua na ndugu wa baba mdogo na mkubwa ubini unakua ule ule, nimesoma comments karibu zote lakini ukweli hii kesi watuhumiwa kukamatwa ni rahisi sana sana. Marehemu kaishi siku 6, na wakati anaungua na kuokolewa aliweza hadi kukumbuka namba ya simu ya baba yake ili apigiwe, hapo tu inaonesha alikua na akili timamu hadi anapatwa na umauti. kingine, hao wauaji kitendo tu cha kutumia simu hilo ni big mistake.
Yes uko sahihi ni ndugu wa kiukoo.

Kwa jinsi Mzee alivyoongea kwa confidence vile lazima kuna clues zimepatikana. Na kwa kukazia alivyosema ni professional killers hapo binafsi siwezi ambatanisha professional killers na mapenzi. Lazima kuna kitu kikubwa pale kazini kwake kilifanyika.
 
Ni kweli lakini vingi sijavizungumza. Nilichukua tu mfano wa scenario uliyoitoa. Hapo kwenye muhimu ndipo pana mantiki kubwa sana nimeijenga. Unaweza kulifanya tukio ukawa umeacha fingerprints ambazo zikipelekwa kwenye database kumbe upo Nida (natania). Tayari manjuga wanaanza kufurahia. Wanamleta boda anakuthibitisha. Wanakupeleka Lupaso unapokea dozi unaanza kutoa ramani yote ilivyokuwa. Unaenda mahakamani unapata wakili mzuri unashinda kesi. Case closed
Na binafsi nilikuwa najenga hoja ya kutumia mawasiliano (simu) lakini usikamatwe kwa kupitia simu bali traces zingine tu kama hizo fingerprints na vitu zingine.

Muuaji smart akimaliza mauaji Kibaha angerudi Kigoma kumpoteza boda hata kwa njia ya ajali au uwizi wa bodaboda. Hapo tayari ushafuta side B ya upelelezi..
 
Nimesoma na mm Cuba nikaamia Venezuela
Ili kukuonesha kuwa wewe ni mwepesi, kwenye video iliowekwa hapa kwenye huu Uzi. Baba wa marehemu anasema baada ya wasamaria wema kuzima moto, Binti alitaja namba ya baba ake ili apewe taarifa.

Sasa kama mtu akiwa na majeraha ya moto aliweza kukumbuka namba ya simu ya baba ake!!
Vipi zile siku 6 alizoishi alikumbuka na kusema mangapi?
 
Back
Top Bottom