Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mimi naimani kabisa sisi sio wabaya hivyo kuna shida kidogo huwezi kuwa mwaka mmoja tu ukatoka team inayogambania mataji manne to zero hapana shida ipo lakini sio kubwa sana hata kuna mwaka tulipoteza sana mwelekeo watu wakawa wanasema basi tena lakini tukabadilika na hili litapita tu ila tunahitaji wachezaji kuongeza kila mwaka lazima tuongeze hata mchezaji mmoja na sio bora mchezaji ila anakuja na kuleta mabadiliko. Kumbuka hata Thiago alisemwa sana wakati tunapoteza mechi lakini leo hii bila Thiago hatuna amani. Hili litapita tu tushikamane na team yetu tuipende kwa dhati.
 
Mchezaji kutoka mfumo wa 433 kwenda 4231 sio tatizo kubwa, rahisi sababu profile zinafit, tatizo lipo (misprofile) kumtoa mchezaji 4231 to 433.
 
Mchezaji kutoka mfumo wa 433 kwenda 4231 sio tatizo kubwa, rahisi sababu profile zinafit, tatizo lipo (misprofile) kumtoa mchezaji 4231 to 433.
Ukiwa 433 unakuwa kama main attacker lakini 4231 unacheza kama kiungo fulani kusaidia attack ni kama Man city KDB alikuwa anacheza kama front 3 lakini leo unamuona ana support ndio sababu hasa ya watu kama kina Sterling kuuzwa kwa sisi mfumo huu wa 4231 hapo utaona watu wanaofit Diaz, lakini Mo na Firminho sio fit kucheza katika nafasi hizo sababu hawawezi ku track kusaidia beki lakini haina maana kuwa Mo ni mchezaji mbaya au Firm ni ile role zao zimebadilika kidogo leo hii sidhani kama Liver wata sign type ya wachezaji kama Mo au Firm kama wataleta basi lile shimo la 3 1 mtu kama Dybala angefit au Pulisic sana na winger yule wa Real Madrid mu uruguay japo kuna watu wanasema huwezi kumpata yule yuko Real lakini ukiona anaongelewa ujuwe watu wanajuwa analipwa nini kule mshahara mkubwa unamtoa tu mtu
 
🚨 BREAKING: Liverpool defenders Joel Matip and Trent Alexander-Arnold have both been ruled out for two weeks through injury. #lfc [james pearce - the athletic]
Afadhali mtoto wa watu TAA apumzike aisee
Huu mtimu ni mzigo aisee..unajituma ila wenzio wanakutumia kama mashine non stop.
 
I was against usajili wa Thiago sababu ya injury zake na mpaka sasa namkubali sababu hakuna plan B yake but huu usajili ulikua bonge la mistake maana boy earns 200k kwa wiki lakini rarely tunavyomhitaji utamuona... Thiago ni kama BMW kwa mswahili its that car you have ila sio kazi kazi all season kama magari ya Kijapan yenye maintenance cost ya chini popote... Ni kweli Thiago is class act lakini kwa Liverpool he is a luxury... Naamini kwa huo mshahara unapata 2 workaholics MFs young, stable, solid. Nwa haya Thiago tuyaache.

Mkuu jiulize tulisubiri miaka mingapi kupata kombe la EPL ndio utaelewa tuna hali mbaya maana wakati unawaza kujiimalisha sio kwamba wengine wamelala fofo.. Kumbuka Arsenal invincibles walivyokiwasha na baada ya pale kwao ubingwa ni ndoto hivyo tuelewane winning is addictive so doea losing... Hatuna plan B zaidi kukumbali are in deep shit kwa sasa sababu ya kukosa proper June incomings maeneo muhimu.

Kwa mpira wa sasa kasi ya EPL kikosi sasa ni wazi wazi ni dhaifu. Kama ulicheki gemu za hivi karibuni we are breaking under pressure yaaani hawajiamini wachezaji wetu its like tukishambuliwa wanasema here again comes kipigo sio TAA wala VVD nk mchezaji pekee anajua anachofanya ni sweeper keeper Allison hawa wengine ni janga kabisa na kwa mbali Nunez, Firmino na Diaz... Hatuna DM maana Fabinho yupo likizo sijui nini kimemkuta kama anakua over whelmed by the flow ya matukio uwanjani...

Lini ni wapi we will find our mojo back is still a mystery.

YNWA
 
Yaani bado huoni kama timu ina shida kubwa?😁
 
Yaani bado huoni kama timu ina shida kubwa?😁
Sijasema kama hakuna shida lakini siamini kwamba tunahitaji kujenga team kutoka zero mimi naamini tunapita kipindi kigumu lakini tutarudi sawa sio kwa ubingwa ila kwa nafasi 4. Leo humu tunasema mengi sababu tu hatufanyi vizuri lakini ni sisi tu mwaka jana miezi miwili tu ilipita tulikuwa kidogo ubingwa, FA, Cup na tulikuwa final ya UEFA tulikuwa tunafuraha hakuna mtu alisema hii team inahitaji wachezaji watani wapya hakuna. 20/21 tulipita kipindi kigumu sana lawama zote zikawa Ohh Thiago hafit lakini tukakimbiza mwishoni tukachukuwa nafasi ya 3. Tumeachwa mblai kidogo na City na Arsenal lakini sio nafasi ya 3 wala 4 uwezo upo. League imeisha May 2022 kidogo tubebe makombe manne league imeanza Aug baada ya miezi 2 tu ndio tumekuwa wabaya kiasi hichi? hapana hatuchezi vizuri na wala hatukuwa na pre season nzuri hilo halina ubishi lakini naamini tutakutana hapahapa na tutaongelea Liver tofauti unahitaji kushinda mechi kama 3 au 4 mfululizo na uwezo huo tunao. Shida wachezaji wabaya? hapana, Je hatuchezi vizuri kama team? Yes. Kumbuka silaha kubwa ya Liver ilikuwa tough Mid na fullback zetu zinapanda leo Rob mgonjwa na TA hana cover kama ilivyokuwa siku za nyuma kikubwa nadhani Hend sio kwa kuanza bahati mbaya hatukusajili Mid kuchukuwa spot ya Hend ndio udhaifu wetu.
 
Mimi nilikuwa mpenzi wa Thiago toka bado yuko Munich jamaa anajuwa mpira kupata viungo kama hawa leo hii nadra sana lakini Thiago sio mdogo ni jukumu la Liver kutafuta viungo kama wawili ukiniuliza nani wako sokoni sina jibu moja kwa moja lakini Belingham anatufaa. Fullback zetu ambao ndio silaha kubwa ya mafanikio yetu Rob mgonjwa na Trent hachezi vizuri japo naamini TA hapati cover kama alivyokuwa akipata siku nyuma sio kwa Hend wala Mo mpira wa siku fullback kama hapati support ni shida sana. Mimi naamini tukipata quality moja katikati kuchukuwa nafasi ya Hend tutakuwa vizuri tu winger moja wa kulia.
 
Basi Mimi Uefa na Epl sikuwa na furaha.
Tunabet Kwa kumtuma Gerrard akamfunge City na Real Madrid wanatufunga Kwa mara ya pili fainali halafu bado tunasema tuko Vizuri😁

Timu zote tulizokuwa tunazifunga zimeshajipanga,Si wale Tena wa msimu uliopita.
Sisi tupo vilevile,tumekariri kwamba tutashinda tu Kwa sababu tulishinda nyuma.
 
Lakini kumbuka hata hao Real Madrid team waliyoitumia ni ile ile kushinda hata kama walisajili ila nakubaliana na wewe tunatakiwa kuongeza nguvu na sio kujaza bench ila tukisajili tuwe na uhakika anakuja mtu kumuweka mtu nje sasa swali je wachezaji gani wako sokoni wanaweza kutufaa? Maana unaweza kuwa unataka wachezaji lakini hakuna au hawauzwi hiyo ndio shida, tuamini katika process hii changamoto tu tutarudi japo sio ubingwa lakini top 4.
 
Wee siyo ileile.
Kuna mabadiliko.


Kuanza kupambania top4 mashabiki hatutaki.
Tunachotaka sisi ni ubingwa.
 
Ubora wa Thiago is world class lakini kua tegemezi week in week out is the big ishu man...too bad we have ageing squad, sasa changanya ageing, loss of form, injuries, lesa confidence utaona how we are deep problems....

Kazi ngumu sana ndugu, kuanzia Klopp, wachezaji, mashabiki tuwe na subira wa kupokea yatakayanayo msimu huu..

YNWA
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…