Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Screenshot_20220409_093957_com.android.chrome_edit_609068412034664.jpg


Ana goli 20 EPL na hajafunga tangu February anaemfuatia ni Son ana goli 14.

Kesho akifunga itapendeza sana arudishe makali yake ugenini kwa Kipara.

YNWA
 
LIVERPOOL VS MAN CITY TATHIMINI
by Robbie Mlatino Jr

Mwambie mkeo, mwambie bebi wako, waambie wanao ambao hawapendi mpira, usisahau kumshitua konda wa hiyo gari uliyopanda asilale sana kituoni, waambie watoto wawahi kulala baba utachelewa kidogo kurudi, washitue Man U, Chelsea, Arsenal na wengine wawahi siti za mbele coz Klopp na Pep watakua wanatoa somo bure la namna ya kushinda mechi..we mblack list mchuchu baada ya mechi hutokosa cha kumwambia bana...twendeni Etihadi ni matajiri wa mafuta vs Wabishi wa jiji Kesho kutwa saa 12 jioni. ..

PEP ATAMSUPRISE WAPI KLOPP.
Kama kawaida ni kwenye lile eneo kati ya beki wa kati na beki wa pembeni. Kwenye utatu wa mbele wa City hua wanaweka watu wanaotumia miguu asilia pembeni. Yaan Mahrez anatumia kushoto atakaa kushoto na hivyo hivyo kwa atakae kaa kulia..nini Faida yake? Ni kutembea kwenye y chaki kuwavuta mafullback wa Liverpool na kutoka karibu na Mabeki wao wa kati ili upatikane uwazi kati ya beki wa kati either VVD na Matip dhidi ya TAA na Robbo halafu Viungo wa City KDB na Silva wanakua wanazishambulia hizo nafasi zilizobaki wazi...

Pia hutega mtego wao kwa namba tisa wao wa uongo kati ya KDB, Jesus au Foden ambao wanakua wanashuka hadi katikati at kuomba mpira...hapa hua kuna swali gumu sana kwa walinzi wa kati..either atoke amfuate huyo no 9 wa uongo na kuacha shimo kwenye ulinzi ambalo City hua wanalitumia haraka kwa no 10 wake wawili kat ya KDB na Silva ili kutengeneza 1v1 kati yao na beki wa kati aliyebaki..au beki wa kati asiende abakie eneo lake na kuruhusu 4v2 au 4v3 kati ya viungo 3 wa City jumlisha huyo mshambuliaji wa uongo dhidi ya viungo wawili au watatu wa Liverpool watakaokua wamebaki katikati ..VVD, Klopp na Matip nadhani wako maabara wanapika dawa ya hili tatizo.

Mwisho City watajaribu kurisk kwa kuwaambia washambuliaj wake wa pembeni wabaki nyuma ya Robbo na TAA ambao hupenda sana kwenda kuwanga hii ni risk pote kama Liverpool wakiwa na mpira watatengeneza 3v1 yaani fullback, mshambuliaji wa pembeni na kiungo mmoja v fullback mmoja wa City...Kipara ataruhusu hili?, sijui..Nini faida yake sasa? Pale ambapo City wakipora mpira wakafanikisha kuuvusha haraka kwenye eneo la katikati basi watakua huru kuzishambulia space ambazo zimeachwa na mafullback wa Liverpool ...mboga moto, Ugali moto. Akili kumukichwa ukizubaa utaachwa sheli.

KLOPP ATAMUULIA WAPI PEP.
Press hadi tone la mwisho.. press hadi iume, press hadi miguu ife. Sio mali yako hiyo ni mali ya Liverpool alishawahi sema Billy Shankily Wafanye City wasiwe comfortable kuanzisha mashambulizi kuanzia nyuma wafanye wawe na kigugumizi cha wapi wapige pasi, wafanye wakupe mpira karibu na eneo lao la hatari. Hakikisha mpira hauendi kwa Rodri, hakikisha KDB anakua kisiwani, hakikisha Benardo network hapatikani pale atakapokua kasimama...hakikisha option pekee ya Stone na Ake au Laporte ni kupiga mbele. Hakikisha mipira yote ya juu mnaicheza..hakikisha mnaokota mipira yote ya juu hakikisha mnarudi fasta golini kwao.

Mipira ya kutenga.
Mna VVD, mna Matip, mna Fabinho, mna Hendo..si wana vimo vizuri sio? Mna wataalam wa mipira ya kutenga TAA na Robbo fanyeni kitu kimoja fanya City walipie kila pigo huru...

City wanatabia ya kuacha Mabeki watatu nyuma kipindi wanashambulia..wawili kati ya Mane, Diaz na Salah wabaki juu kuwatishia nyau wakina Laporte. Hendo awe fasta kule kulia ili atengeneze wingi wa wachezaj ule upande kipindi wanashambulia..wamlazimishe Joao Cancelo alinde zaidi badala ya kushambulia coz yeye pia mtega dawa njia panda kipindi wachawi wa PEP wakiwa wanachawi. Salah ndo jukumu lake..


Mwisho Klopp afunge na kusali kesho Hendo na Mmoja kati ya Keita au Thiago atakaenda kwenye kiungo na Fabinho wawe na mafuta ya kutosha kwenye tank Lao sio mafuta ya vibaba asee...wakimbie mno kuziba zile nafasi kati ya beki wa kati na beki wa pembeni...wakate mirija yote ya chakula kati ya washambuliaj wa pemben na wale no 10 wawili au no 8 wawili acha wakina KDB walale njaaa ili wawalazimishe watumie kross kulifikia goli la Liva.. urefu wa washambuliaj wa City sio kitu mbele ya akina VVD. Wawafanye City wakimbilie pembeni kupiga kross....hadi hapa gem itakua ngumu kwa Pep... subiri nilitaka kusema kitu hapa Klopp awakumbushe Salah na Mane huu Ni mwezi mtukufu wa Ramadhan kama mtaani tunafuturu kwenye mkeka mmoja kwann wao wasipeane Pasi wakati hiyo ifutar ni ya wana Liva wote?

Battle za kuangalia..
Salah vs Cancelo
Mane vs Stones na Laporte
Fabinho vs KDB.
Diaz vs Walker
Sterling vs TAA
Hendo vs Mikimbio ya Silva
Robbo vs Mahrez.

Nidondoshe utabiri wanguCity 2-3 liverpool...

Tutafuturu saa 3 hiyo Jumapili na home tutaeleweka ...
Tchaoooo.
Hii game ni draw Tena ya 0-0 ....

City tutaendelea kukaa top of the table
 
View attachment 2181272

Aisee wasubiri ligii iishe ndio haya mambo tuyaanze kuona namna gani.

Benzema kwa sasa yupo juu.

YNWA
Sioni hoja ya kusema Benzema yupo juu kuliko lewandowsk mi naona labda tuseme anatrend kwa kupiga hat trick back to back dhidi ya timu zinazofatiliwa sana uefa lakini hapo lewa ni the best....
Uefa Lewa ana goli 12 na bundasliga ana goli 31
Benzema yeye ana goli 11 na laliga ana 24...
Mi naona ni muda muafaka wa kumpa Lewa ballon dor wamemzungusha kwa muda mrefu sana...
Salah hapo anakaa nafasi ya tatu coz hapa katikati ameflop maybe kama ataregain ubora wake na ukizingatia kashindwa kufuzu kombe la dunia ndo basi tena
 
Hana pressing huyu awezi Kuja Liverpool
Under Klopp atabadilika.

Kingine Klopp sasa anabadilika kimfumo kulingana na mpinzani tofauti na zamani tulikua ni 4 3 3 period.

Kama bei itakua rafiki atatufaa sana tumekua wasteful muda mwingi pale golini lakini tukipata real poacher mambo yatabadilika.

YNWA
 
Sioni hoja ya kusema Benzema yupo juu kuliko lewandowsk mi naona labda tuseme anatrend kwa kupiga hat trick back to back dhidi ya timu zinazofatiliwa sana uefa lakini hapo lewa ni the best....
Uefa Lewa ana goli 12 na bundasliga ana goli 31
Benzema yeye ana goli 11 na laliga ana 24...
Mi naona ni muda muafaka wa kumpa Lewa ballon dor wamemzungusha kwa muda mrefu sana...
Salah hapo anakaa nafasi ya tatu coz hapa katikati ameflop maybe kama ataregain ubora wake na ukizingatia kashindwa kufuzu kombe la dunia ndo basi tena
Lewandoski namuona La Liga next season aisee kwa kweli akitua kule na akaedeleza ubora wake basi Ballon inamhusu.

Muda kwa Salah upo kurudisha makali katika gemu zilizobaki azidi kua na utulivu ajitume na umakini uwepo apatapo nafasi na magoli yatakuja tu.

YNWA
 
Natamani miaka irudi nyuma nikutane na wale mashabiki wa Nyumbu enzi hizo za kidato cha kwanza miaka ya 2009 nilipize kuwacheka
 
My line ups for tomorrow


1. Alison


66. Trent. 32. Matip. 4. Virgil. 3. Robertson.



14. Henderson (C). 3. Fabinho. 6. Alcantara.




11. Salah. 9. Firmino. 10. Mane
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom