Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Nawashukuru sana FSG wametutoa mbali na kutufikisha hapa tulipo.
Lakini niwe mkweli sina Imani nao hawa Matajiri wetu wa FSG kwa sababu tu ya sera yao ya Sell to Buy.
 
Hadi leo hii ni siku ya 21 toka dirisha la usajili lifunguliwe mabeki wote wako wodini lakini tumelizika tu na kunyamaza kimya kwa sababu Fabby na Hendo wapo, hahahahahah matokeo yake stability ya timu inakosekana kabisa mpaka manure wanatoka na point Anfield, haya ni maajabu makubwa sana
 
Gini anaondoka bure, kutokana na sera ya Mabosi wetu ya Sell to Buy Basi kuna haja ya kuwauza MATIP, KEITA, OX, SHAQIRI, NAT PHILLIPS, HARRY WILSON, GRUJIC na ORIGI ili kufunds New CB na AM na Winger.
 

Mkuu kumbuka tuna sera ya Sell to Buy wakati January hii hatujauza yeyote sasa tutasajili vipi?
Subiri kwanza tumuuze Origi ndiyo tununue.
 
Kwani hii mechi ya juzi ni ya kwanza kwa Mane na Salah kuwekwa mfukoni na FB wa United?..si ni kawaida tu?.

Bissaka kwenye kukaba ni ishu nyingine,shida yake ni his offensive play...

Huu ni mwendelezo wa Ego iliowajaa nyie Scousers mkiongozwa na Klopp wenu..Wewe unadhani Mane anaweza kumgeuza geuza AWB kama Trent alivyogeuzwa na Rashford kwenye ile game ya 2-1 OT?
 

MosDef yuko sawa tu mkuu kwa upande wangu,


Kwasababu vvd Na gomez wakiwepo Fabinho angesogea mbele na Fabinho akiwa hapo kati sidhani kama atamaliza msimu bila kufunga,lakini kwa sasa hawezi kufunga.

Na kutokuwepo kwa vvd sasa hivi hatua uwezo wa kufunga magoli ya kona ,mipira ya kona wapinzani hata hawatuogopi siku hizi,na hata sisi kufungwa magoli ya kona inakuwa kawaida kabisa,vvd angekuepo mipira yote ya kona anaokoa yeye.

Timu yetu haiko vizuri kwenye mido,mido ikicheza vizuri siku hiyo wapinzani wataoga magoli.
 

VVD na GOMEZ ni moja ya factor kwenye Midos ambayo inaathiri system ya Timu ya uchezaji, but kwenye uwezo binafsi wa wachezaji (Front 3) Mkuu wameshuka sana kiasi ya kwamba hawawezi kushot golini wala kutoa pasi kwenye mashambulizi.
 

Mkuu No 2 hapo, unamlaumu bure Mane, AWB sio boya kaka, elites wengi tu wameshindwa kufuruka. So mpe heshima yake.


Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
VVD na GOMEZ ni moja ya factor kwenye Midos ambayo inaathiri system ya Timu ya uchezaji, but kwenye uwezo binafsi wa wachezaji (Front 3) Mkuu wameshuka sana kiasi ya kwamba hawawezi kushot golini wala kutoa pasi kwenye mashambulizi.

Mkuu Front 3 kuwa butu hilo liko wazi,kwa kawaida huwa wanabadilishana Mechi hii asipofunga mane salah anafunga au wasipofunga firmino anafunga,kwa sasa imekuwa hawafungi wote.

Halivyokuwa jota alikuwa anAtubeba anafunga yeye.jota kaumia majanga.

Kwa sasa front 3 yetu inatia hasira sana.
 
You're right but Nyinyi LIVERPOOL HALISI spana sio kwa Hendo kwasababu katupa CL na EPL kwani bila ya yeye tusingebeba Makombe.
Spana tuwachie sisi Liverpool PEP.

Hendo kampita hadi Gerrard, sasa kwa nini tumseme?

Kwa miaka zaidi ya 30 hakujawahi kuwa na captain bora kuliko Hendo, sasa kama Klopp na Southgate wanamkubali, nyinyi Liverpool PEP ni nani mmseme? Kwanza hamna football management.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…