Kutoka FB
JE UNAJUA?
Liverpool FC wanaweza kuvunja rekodi nane za Premier League msimu huu.........
Hebu tusome baadhi ya rekodi nilizowaandalia zitakazoweza kuvunjwa msimu huu na #LFC
Mustarger Coutinho



️
1- ALAMA NYINGI
- Liverpool wanaweza kuvunja rekodi ya alama nyingi kwa msimu. Msimu wa 2017/2018, Man City walifikisha alama 100...Kimahesabu tunaweza kufikisha alama 112.
2- MECHI ZA KUTOFUNGWA
- Kila mmoja anaijua Arsenal isiofungwa (Arsenal Invincibles). Hawakupoteza mchezo wowote katika michezo 49 kati ya mwaka 2003 & 2004. Tupo katika mbio za kuvunja hio rekodi. Hadi sasa hatujafungwa katika mechi 43.
3- TOFAUTI YA ALAMA NA TIMU YA PILI
- Man City walikua na alama 19 mbele ya Man Utd msimu wa 2017-2018. Tayari tumewaacha Man City kwa alama 25. Na utofauti huo utaweza kuongezeka kama Liverpool wakiendelea kuwasha moto huu huu. (Hii rekodi tushaivunja na sasa imeshakua ya kwetu) Tunasubiri wengine waje kuongoza ligi kwa alama 25 kama sisi.
4- USHINDI MFULULIZO
Mwaka 2017, Man City walienda mechi 18 mfululizo wakishinda. Sasa tumeshinda mechi 17 mfululizo. Wapinzani wetu wanaofata ni West Ham na Watford. Haka karekodi kashavunjwa asee.
5- SIKU YA KUTANGAZWA MABINGWA
- Man Utd (2001) na Man City (2018) walitangazwa mabingwa mechi 5 kabla msimu haujaisha. Kwa uwiano huu, tutakua Mabingwa mechi 7 kabla msimu haujaisha. Na tutaweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kutangazwa Mabingwa mapema kabisa. Mechi zitakazobaki zitakua za kuvunja rekodi.
6- MECHI NYINGI ZA USHINDI
- Katika misimu miwili iliopita, Man City walipata ushindi katika mechi 32. Tayari tumeshinda mechi 25 na mechi 12 zikiwa zimebaki msimu uishe. Hii itakua rekodi nzuri sana kwetu kuifikia.
7- SARE CHACHE
- Man City na Tottenham walikua na sare 2 msimu uliopita. Sasa hivi tuna sare 1 tu. Dhidi ya Man Utd (1-1) Old Trafford!
8- KUMALIZA MSIMU BILA KUFUNGWA
- Tutaweza kuvunja rekodi ya Arsenal. Arsenal hawakufungwa mechi yoyote msimu wa 2003-2004. Na tuna mechi 12 zimebaki.
NOTE: LIVERPOOL FC WATAKUA MABINGWA KWA KUWEKA REKODI AMBAZO KUJA KUVUNJWA ITACHUKUA MUDA SANA. Acha tuenjoy football asee.
What a time to be alive as a Liverpool fan
Sent using
Jamii Forums mobile app