Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Ahahaaah...
Upo sahihi,adui yako muombee njaa...
Ila pia usisahau,never underestimate your enemy..!
defintly, mpaka sasa City bado anapewa pointi nyingi kuchukua ubingwa na wacheza kamali na wachambuzi wazoefu UK hio sio bure mbali City anakikosi na wachezaji wenye uzoefu na kocha mzoefu wa kuchukua makombe tofauti...

Kwetu sisi Liverpool ni kuhakikisha kila mechi tunacheza kwa umakini ili kutoka na ushindi wa pointi 3 muhimu.

Ya City tuwaachie wenyewe tupambane na yetu.
 
Kweli kabisa...
Huu ndio muda wa wachezaji wa Liverpool kuwa mbali na social media...
Inabidi wawe focused kwelikweli,wasipobeba kombe msimu huu mashabiki wake watakuwadissapointed sana,maana mashabiki wengi wa Liverpool wanaamini kuwa huu ni mwaka wao(wana haki ya kuamini hivyo)..!
 

It's coming HOME!
YNWA.
 
Mkuu dalili zinaonyesha ni mwaka wetu kabisa ukizingatia matokeo uwanjani yapo vizuri kwa sasa..

Pep anajitahidi na kikosi chake wasikae mbali nasi ili tukiharibu tu hawa hapa kuchukua ushukani...

hapa ni kikosi chetu kukaza hizo mechi 15 zilizobaki kuhahakisha tunamaliza msimu huu na kicheko...

Klopp mzuri tunae, wachezaji wazuri tunao, mashabili nguli wanaosimama nyuma ya timu tunao, nia tunayo ya kulichukua kombe cha ziada ni kupambana kushikamana mpaka mwisho..

Media za UK japo wameshaanza yao ya kututia presha utawasikia "ooh presha back to Liverpool" n.k ..sisi tunapambana na yetu Kombe litue mazima kwa shangwe.
 

Mkuu usiwe na wasiwasi iwapo hili jinamizi la majeruhi halitoendelea kutuandama basi Liverpool ni Bingwa wa EPL 2018/19
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…