Mbowe anapanda jukwaani.
Mbowe:
Namshukuru sana mwenyenzi Mungu, kwamba leo tumekutana tena kuzungumza mustakbali wa taifa letu.
tumekutana juzi na jana na viongozi takriban mia tatu, tumekutana arusha kufuatia azimio la chama chenu, kwamba mapambano dhidi ya ccm, kwamba tubadilishe mbinu.
tumwongeza nguvu bungeni, tumeongeza nguvu kwa madiwani, tumebakiwa na mbinu moja muhimu, ambao tunaita mbinu shirikishi.
Mbinu ambayo kila moja ataweka maslahi ya taifa mbele kuleta ukombozi.
kwa miaka 20 ambayo chadema ilikuwepo, mapambano yote yamekuwa yakipangwa daresalama, sasa tunapiga chini kwa chini, na kazi ya chama itaendelea kufanywa ki silencer.
Watanzania walio wengi hawajaelewa sera za majimbo.
Watanzania hawana kauli juu ya rasilimali zao.
watanzania hawana kauli juu ya hatima ya maisha yao.
maamuzi yanafanywa na watu ambao watanzania hawakuwachagua.
Tulipiga kura kuwachagua madiwani, wabunge, lakini hakuna aliyepiga kura kumchagua mkuu wa mkoa wala mkuu wa wilaya.
Mimi Mkuu wa mkoa simwogopi, kikwete simwogopi.